Ajira Portal inahitaji mabadiliko, inakatisha ndoto za vijana wengi kwenye kuomba ajira

Ajira Portal inahitaji mabadiliko, inakatisha ndoto za vijana wengi kwenye kuomba ajira

singojr

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2014
Posts
5,313
Reaction score
6,895
Niende moja kwa moja kwenye point. Lengo la hii mifumo ni kurahisisha process ya kuomba ajira na kuongeza umakini katika kuhakiki taarifa za mwombaji. Kwenye mfumo mtu anawajibika kuupload copy za vyeti zilizokuwa certified. Kwanini mfumo usiwe intergrated na necta directly.

Kwanini sehemu ya vyuo isiwe intergrated na TCU iwe tu mtu kuingiza namba yake the rest system inamaliza.

Hakuna option ya kudelete, ukiupload ukufanya error yoyote inayohitaji kudelete hiyo option hakuna.

Slowness, kwenye kuupload na kudownload data system inalemewa kwanini hawajawaza kuiongezea uwezo?

Naamini haya mambo yanarekebishika kama mkiamua kuwapunguzia mzigo watumiaji wa system yenu.

Huu mfumo unaratibiwa na watu wa aina gani? Kwanini mnazuia vijana wasiweze kurekebisha au kudelete academic qualifications walizoziweka?

Halafu mbona mkiandikiwa email hamjibu? Pia sehemu ya feedback mmeweka recaptcha iliyo case sensitive lakini wakati wa kuandika mmeweka automatic upper case kwahiyo muda wote inakataa.

Rekebisheni haya matatizo.

Mliyowahi kuapply kupitia mfumo wa ajira portal mlifanyaje mkafanikiwa maana mimi nagomewa.

Lakini pia kwenye kipengele cha academic qualification Hamna option ya kufuta qualification zingine msaada wenu jaman

Hivi kweli hiki chombo mhimu ya Ajira nchini kina Wabobezi wa IT?

Yaani Website yao Iko hovyo sana linapo kuja suala la ku apply. Website, appearance ina vutia kwa nje. Ila sasa ingia ndani ktk ku chakata taarifa, ni website ya hovyo!!

Inawezeka kabisa kutokana na poor design ya Website hii, vijana wengi wenye sifa wakawa wana kosa ajira kisa kuondolewa na mfumo mbovu automatically. Mfumo utamwambia hana sifa, haja timiza vigezo, nk ili hali vigezo vyote anavyo. Baadhi ya matatizo nili kumbana nayo leo.
Kuna ajira ni lazima uombe kupitia ajira portal cha ajabu ukisign in kwa app yao inagoma hapo hapo ukisign up inaandika invalid email address na kila mtu hii inamkumba.

Kiujumla sahivi huwezi kuaccess ajira portal na hapo deadline ya maombi unakuta ni after few days.

Huu ni mkakati wa maksudi tu ili watu wasiombe wawekane wenyewe kwa wenyewe hawa ma-IT wa serikali na wanaosimamia hizi app na tovuti walipaswa wawe wamefukuzwa kazi.
Wakuu naombeni msaada, kila ninapojaribu ku update picha naona ina load tu lakini haibadiliki.

Picha iliyopo sasa hivi niliiweka wakati nipo certificate, sasa haikuwa ya passport size ilikuwa ni picha ya kawaida tu ya photo shoot.

Kwa anaejua namna ya ku update picha nyingine naomba anisaidie maana kila nikijaribu inagoma, msaada wakuu tafadhali.
Hivi kwanini ajira portal wanabana sana system ya kuomba kazi utumishi yaani mtu ana vyeti vyote kaweka kwanini wasimpe uhuru wa kuapply tu na sio kuoverqualify yaani wanafanya maisha yanakuwa magumu kabisa mtaani wakati mtu ana uwezo kabisa wa kuomba lakini system walivyoibana sio poa kabisa.
 
Nimekumbwa na hili tatizo ninapojaribu kufanya application naambiwa error; please update your asce/ cse index numbers na hapo nimetoka ku update tayari.

Screenshot_20211103-015914.jpg


Screenshot_20211103-015914.jpg
 
Mkuu nimefanya hivohivo ila bado tatizo lipo palepale inaniandikia error unable to save your data.. multiple records for index number existView attachment 1996588
Anhaa, hapo umeingiza form four index number mara nyingi so ndio maana inakwambia, multiple record for index number chakufanya badilisha email ktk usajili lkn hakikisha email iko valid. Jaribu hvyo mkuu ila form iv index number ni hiyo hiyo yako, ww badilisha email na anza kujisajili upya kwa kujaza information zako, kumbuka majina yawe kama yanavyoonekana ktk cheti cha form iv
 
Anhaa, hapo umeingiza form four index number mara nyingi so ndio maana inakwambia, multiple record for index number chakufanya badilisha email ktk usajili lkn hakikisha email iko valid. Jaribu hvyo mkuu ila form iv index number ni hiyo hiyo yako, ww badilisha email na anza kujisajili upya kwa kujaza information zako, kumbuka majina yawe kama yanavyoonekana ktk cheti cha form iv
Nashukuru sana mkuu kwa kujali kwako... niliwapigia sjmu kwa bahati nzuri wakapokea kama ulivyoniambia nilijaza mara nyingi vyeti so amenirekebishia,kwa kuzifuta.. na saahv nimecheki iko poa.. shukran sana chifu
 
Ni kwa sababu ni over qualified, umepindukiza vigezo system imekuwa designed kwa kuchanganua vigezo husika kwa maana huwezi kuomba chini ya vigezo ulivyokuwa navyo inaangalia kigezo cha juu zaidi, kama vile huwezi kuomba nafasi ya kazi isiyoendana na elimu yako.

Alaf sidhan kama utaweza ku delete cheti chako uombe nafas ya diploma au chini yake, system pia inakataa hvyo, ukiwa cheti cha degree umeweka.
 
Back
Top Bottom