mwanyaluke
JF-Expert Member
- Jan 22, 2015
- 704
- 2,435
Observation hii nimeifanya kwa muda mrefu, nimeongea na watumishi waliojiriwa na kufanya kazi private sector Kisha wakajiriwa serikalini, waliofanya kazi maisha yao yote private sector na wafanyakazi waliojiriwa serikalini kisha wakajiriwa private sector na waliojiriwa na kufanya kazi maisha yao yote serikalini nilichojifunza na kukiona hiki.
1. Miaka ya mwanzo mnapoajiriwa private sector na serikalini, mfanyakazi wa private sector anakuwa na maisha mazuri zaidi na anafurahia maisha ya ajira
2. Inapofika miaka mitano kwenda mbele , mfanyakazi wa serikali ananza kupata raha ya kazi , wakati huo private sector anaanza kuichukia kazi (hapa sababu ni kupandishwa madaraja na ongezeko la mishara serikalini na wengi wafanyakazi wa serikali wanakuwa wamekaribia kumaliza Deni Leo la Kwanza alilokopa)
3. Inapofika miaka 10 na kuendelea , private sector wengi huwa wanajuta na kuwa na makasiriko mengi na upande wa pili wale wa serikalini wanakuwa wamegain momentum kwenye safari ya maisha, ( huyu private anagundua hana security, mshahara hauongozeki, hana fursa ya kuteuliwa au kupandishwa cheo, na upande wa pili huwa ni watu wenye kujiamini( job security ni kubwa, amepandishwa daraja, Kama yupo idara nzuri ameisha piga mipigo ya hela, deni la pili linakuwa limeisha, hapa anakuwa ametimiza tayari ndoto ya Mtanzania ya kuona mafanikio ni nyumba na gari, watoto wanasoma, kama alikuwa ni mjanja kamradi flani alikoanza tayari kanaenda na ana uwezo w kufinance, huyu wa private sector muda huo ananza kutafta matangazo ya ajira ya serikalini na wengine wanajikuta wamekosa vigezo shida umri.
4. Inapofika miaka 15 wengi wanakuwa Wana miaka 40 and above, kipindi hicho watumishi wengi huwa hawaoni fahari Wala hawajisifu kisa eti tu ni mfanyakazi (ukiambiwa life begins at 40 ndipo unaelewa huo msemo chanzo chake ilikuwa ni nini) kipindi hiki Kila binadamu hujikagua mwenyewe na kugundua amefanikiwa au bado, the same kwa wafanyakazi huwa hawaoni sifa sijui kumiliki nyumba na gari , kipindi hiki mada kubwa huwa ni ada za watoto wao, ni kipindi hicho ambacho wafanyakazi wa private sector huwa ni watu wenye makasiriko Sana, waoga mno kwa maboss wao , wengi huwa wanajuta Sana hapa kwa Nini sikuajiriwa serikalini, hapa ndipo wafanyakaz hata wa serikali huanza kuchukia kazi zao Tena na wengi huchukia kama hakuteuliwa au kupandishwa cheo, wengi hapa huchukia mfumo wa utawala na chama tawala kuona kama kimejaa rushwa hasa inapotokea vijana wadogo kwake wanapokuja kuwa boss wake kazini na hususani wana elimu sawa, hapa wafanyakazi wengine huacha kabisa kufuatilia Mambo ya nchi na siasa
5. Inapofika miaka 50 hofu huwa kubwa sana kwa wafanyakazi wote,private sector hujiona ni mtu mwenye mikosi, hakuchukua hatua stahiki kwenye maisha, wengi huwa wanaujiuliza Sana kwa Nini sikuacha kazi na kujiajiri mwenyewe?
Upande wa pili huwa pia ni watu wenye hofu Sana na wengi huwa wanajiuliza sana hapa hivi Niki stafu itakuwaje, hivi ntaishi wapi, hawa watoto wadogo bado wanasoma dah sijui ntasomeshaje ? Kiufupi wengi hapa huwa na watu wa ibada Sana
6. Miaka 55 (umri wa kustafu kwa hiyari) private sector huwa ni watu hatari sana hapa, akitazama umri wake, akitazama alichokifanya maishani, akijilinganisha na wafanyakazi wa serikali, akiwaza kiasi kidogo cha fedha (pension) Atakayopata baada ya kustafu, hiki kipindi ndicho wafanyakazi waliokuwa smart kimavazi, mentality yao huwa ni mbovu na wengi hujikuta wapo rafu eti haogopwi kufukuzwa
Upande wa pili serikalini Pia huwa ni wenye hofu sana na huwa ni wafanyakazi wenye nidhamu sana, ni kipindi ambacho ukiwa mkuu wa wilaya unaweza kwenda ofisini ukawacharaza viboko na bado watakusifu, wengi waliokuwa wanoko kwa wafanyakazi wenzao unoko unaisha wanabaki ni watu wa imani sana, wengi hapa hufikiria atatumia pension yake vipi? na wale ambao hawakujipanga huanza kufikiria miradi hii kulima, na kufuga , kununua gari ya biashara na duka na hujaribu kufanya hivyo na wanapochemka hujutia Sana, ni kipindi pekee ambacho kila mfanyakazi huwa ni msikilizaji mzuri, unaweza mshauri chochote na akakusikiliza, maisha ya utumishi ni safari ndefu na ngumu Sana, ni Safari yenye furaha kidogo na majuto mengi.
Ushauri wangu kwa vijana pambana sana kupata kazi serikalini, ukipata kazi pambana sana kuwa na kazi nyingine nje ya ajira yako na pambana Sana kipato cha nje ya ajira kiwe ni kikubwa kuliko kipato cha ajira, mlioko serikalini kopa sana na wekeza, maisha ni Safari na wewe ni msafiri safiri ukijua siku zote ajira haiwezi kukupa raha ya maisha, ila ajira inauwezo wa kukupa starting capital, usiache kazi kwa kutamani maisha ya wengine, uhuru na raha ya maisha ipo kwenye kujiajiri huko nako kuna changamoto zake, ntaleta uzi wake siku moja, uzi huu nii matokeo ya Mimi kufanya kazi private sector, sasa nipo serikalini miaka kama sita, na daraja langu E, nimeajiajiri kwenye kilimo na ufugaji na nafanya biashara ya mazao ya kilimo na mifugo.
1. Miaka ya mwanzo mnapoajiriwa private sector na serikalini, mfanyakazi wa private sector anakuwa na maisha mazuri zaidi na anafurahia maisha ya ajira
2. Inapofika miaka mitano kwenda mbele , mfanyakazi wa serikali ananza kupata raha ya kazi , wakati huo private sector anaanza kuichukia kazi (hapa sababu ni kupandishwa madaraja na ongezeko la mishara serikalini na wengi wafanyakazi wa serikali wanakuwa wamekaribia kumaliza Deni Leo la Kwanza alilokopa)
3. Inapofika miaka 10 na kuendelea , private sector wengi huwa wanajuta na kuwa na makasiriko mengi na upande wa pili wale wa serikalini wanakuwa wamegain momentum kwenye safari ya maisha, ( huyu private anagundua hana security, mshahara hauongozeki, hana fursa ya kuteuliwa au kupandishwa cheo, na upande wa pili huwa ni watu wenye kujiamini( job security ni kubwa, amepandishwa daraja, Kama yupo idara nzuri ameisha piga mipigo ya hela, deni la pili linakuwa limeisha, hapa anakuwa ametimiza tayari ndoto ya Mtanzania ya kuona mafanikio ni nyumba na gari, watoto wanasoma, kama alikuwa ni mjanja kamradi flani alikoanza tayari kanaenda na ana uwezo w kufinance, huyu wa private sector muda huo ananza kutafta matangazo ya ajira ya serikalini na wengine wanajikuta wamekosa vigezo shida umri.
4. Inapofika miaka 15 wengi wanakuwa Wana miaka 40 and above, kipindi hicho watumishi wengi huwa hawaoni fahari Wala hawajisifu kisa eti tu ni mfanyakazi (ukiambiwa life begins at 40 ndipo unaelewa huo msemo chanzo chake ilikuwa ni nini) kipindi hiki Kila binadamu hujikagua mwenyewe na kugundua amefanikiwa au bado, the same kwa wafanyakazi huwa hawaoni sifa sijui kumiliki nyumba na gari , kipindi hiki mada kubwa huwa ni ada za watoto wao, ni kipindi hicho ambacho wafanyakazi wa private sector huwa ni watu wenye makasiriko Sana, waoga mno kwa maboss wao , wengi huwa wanajuta Sana hapa kwa Nini sikuajiriwa serikalini, hapa ndipo wafanyakaz hata wa serikali huanza kuchukia kazi zao Tena na wengi huchukia kama hakuteuliwa au kupandishwa cheo, wengi hapa huchukia mfumo wa utawala na chama tawala kuona kama kimejaa rushwa hasa inapotokea vijana wadogo kwake wanapokuja kuwa boss wake kazini na hususani wana elimu sawa, hapa wafanyakazi wengine huacha kabisa kufuatilia Mambo ya nchi na siasa
5. Inapofika miaka 50 hofu huwa kubwa sana kwa wafanyakazi wote,private sector hujiona ni mtu mwenye mikosi, hakuchukua hatua stahiki kwenye maisha, wengi huwa wanaujiuliza Sana kwa Nini sikuacha kazi na kujiajiri mwenyewe?
Upande wa pili huwa pia ni watu wenye hofu Sana na wengi huwa wanajiuliza sana hapa hivi Niki stafu itakuwaje, hivi ntaishi wapi, hawa watoto wadogo bado wanasoma dah sijui ntasomeshaje ? Kiufupi wengi hapa huwa na watu wa ibada Sana
6. Miaka 55 (umri wa kustafu kwa hiyari) private sector huwa ni watu hatari sana hapa, akitazama umri wake, akitazama alichokifanya maishani, akijilinganisha na wafanyakazi wa serikali, akiwaza kiasi kidogo cha fedha (pension) Atakayopata baada ya kustafu, hiki kipindi ndicho wafanyakazi waliokuwa smart kimavazi, mentality yao huwa ni mbovu na wengi hujikuta wapo rafu eti haogopwi kufukuzwa
Upande wa pili serikalini Pia huwa ni wenye hofu sana na huwa ni wafanyakazi wenye nidhamu sana, ni kipindi ambacho ukiwa mkuu wa wilaya unaweza kwenda ofisini ukawacharaza viboko na bado watakusifu, wengi waliokuwa wanoko kwa wafanyakazi wenzao unoko unaisha wanabaki ni watu wa imani sana, wengi hapa hufikiria atatumia pension yake vipi? na wale ambao hawakujipanga huanza kufikiria miradi hii kulima, na kufuga , kununua gari ya biashara na duka na hujaribu kufanya hivyo na wanapochemka hujutia Sana, ni kipindi pekee ambacho kila mfanyakazi huwa ni msikilizaji mzuri, unaweza mshauri chochote na akakusikiliza, maisha ya utumishi ni safari ndefu na ngumu Sana, ni Safari yenye furaha kidogo na majuto mengi.
Ushauri wangu kwa vijana pambana sana kupata kazi serikalini, ukipata kazi pambana sana kuwa na kazi nyingine nje ya ajira yako na pambana Sana kipato cha nje ya ajira kiwe ni kikubwa kuliko kipato cha ajira, mlioko serikalini kopa sana na wekeza, maisha ni Safari na wewe ni msafiri safiri ukijua siku zote ajira haiwezi kukupa raha ya maisha, ila ajira inauwezo wa kukupa starting capital, usiache kazi kwa kutamani maisha ya wengine, uhuru na raha ya maisha ipo kwenye kujiajiri huko nako kuna changamoto zake, ntaleta uzi wake siku moja, uzi huu nii matokeo ya Mimi kufanya kazi private sector, sasa nipo serikalini miaka kama sita, na daraja langu E, nimeajiajiri kwenye kilimo na ufugaji na nafanya biashara ya mazao ya kilimo na mifugo.