Ajira za ualimu zimeendelea kuwa kokolo kwa kusomba hata wasiofaa

Mshinga

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
3,532
Reaction score
1,126
si kila aliyesoma ualimu na kuhitimu toka chuo chochote iwe cha serikali ama private ana uwezo wa kufundisha akaeleweka, sasa hapa wote waliofauru wameajiliwa bila mchujo wakupata wanaoeleweka. ifikie wakati tuangalie kinachotakiwa, masomo ya sayansi yataendelea kusumbua hasa physics na mathematics maana yanahitaji walimu wanaoeleweka zaidi na kama hawaeleweki basi hawana msaada sawa na kwamba wanafunzi hawana mwalimu
 

True say...ila unadhani hao wanaopata high marks na degree first class wanataka kufanya kazi ya ualimu? Inabidi serikali ije na mpango mwingine madhubuti wa kuhakikisha sekta ya elimu hasa kwa ngazi za juu zinakuwa na watu proffesion na wenye uwezo wa kutosha
 

ngoja waje ...!@wakali hao
 
mimi navyojua ualimu ni uwezo binafisi mtu aliozaliwa nao, kumwelekeza mtu akaelewa ni zaidi ya first class, mfumo uwatambue wale tu wanaoeleweka vizuri kwa wanafunzi hata kama wanaufaulu wa kawaida
 
Wivu tu umewajaa!Fyuuuu.....
wivu nimuonee nani? mimi nina wivu kwa mpenzi wangu pekee. hapa naongelea mambo ya kitaifa kwa faida ya taifa ya sasa na ijayo ya wana wa tanzania
 
mtoa mada umesoma HRM nini mbona umeumia sana?
naheshimu kozi zote japo zingine zina umuhimu hafifu. hata hivyo sijasoma HRM japo nawaheshimu waliosoma kozi hiyo sawa na wengine wote.
 
Ni roho tu inakuuma watu kupata ajira ww ulitakaje? Kwahyo walimu wa masomo yakiswahili wasiajiliwe mana wa masomo ya sayansi hakuna au ulitaka waajiliwe walimu wa Physics tu!
 

Kama hujawahi kupata utindio wa ubongo basi upo mbioni kuupata. This is so because i understand the whole process a student teacher goes untill the last drop to his /her appointiment. What kind of selection would you like to propagate to the ministry of culture and education? Do you really understand what does the vocabulary ASSESSMENT stands for?
 
mimi navyojua ualimu ni uwezo binafisi mtu aliozaliwa nao, kumwelekeza mtu akaelewa ni zaidi ya first class, mfumo uwatambue wale tu wanaoeleweka vizuri kwa wanafunzi hata kama wanaufaulu wa kawaida

Uelewa wa wanafunzi umetofautiana. Huyu anaelewa zaidi, huyu kawaida, huyu japo kidogo. Hakuna mtu anayeeleweka kwa wote. Je mwalimu wa hesabu anaeleweka? Ualimu sio kumjaza mtoto material bali ni kumwelekeza afikie talanta yake. Na pia kufaulu sana si hoja. Kuna watu wanapata maksi za kawaida lakini uelekezaji wao na umakini wao utaupenda.
 
ndugu sisi wengine hata hilo kokolo halijatubebelea watu kama 300+hatupo kwenye hayo majina toka sjut-dom,hivyo hi mada yako inatuuma sana?
 
Usilolijua ni sawa na ucku wa giza.kazi ya mwl nikuelekeza mwl anamchango 20ASILIMIA 80 ya mwanafunzi.j
 
kazi ya ualimu inaitaji moyo.watoto wazazi na serikali wakorofi.watoto wapo fb kila wkt wakitafuta marafiki.wangesoma wp
 
Ni roho tu inakuuma watu kupata ajira ww ulitakaje? Kwahyo walimu wa masomo yakiswahili wasiajiliwe mana wa masomo ya sayansi hakuna au ulitaka waajiliwe walimu wa Physics tu!
nataka mchujo sahihi kwa walimu wanaoajiliwa wala sina wivu na mtu na nilikataa kusoma ualimu kwa sababu walimu hawathaminiwi, nachotaka taifa lipate walimu ambao wakifundisha watoto wanaelewa na si aina hii ya ajira ambapo hata wasioeleweka kwa wanafunzi wanaajiliwa huku wakitafuna hela na wanafunzi hawaelewi
 
mbona unajadili kwa jaziba na mitusi? hii ni ishara kuwa huna hoja na unauelewa mdogo sana. assessment ni sehemu ya masomo kwenye kozi zote na si ualimu peke yake, hakuna ajira yoyote inayopimwa kwa assessment na ndio maana hata engineer anafanya interview na assessment walifanya
 
tatizo una uelewa mdogo sana wa kusoma na kuelewa nilichoandika, hao wenye ufaulu wa kawaida na wanaeleweka ndo wanaofaa, ina maana hujawahi kuona mwalimu anakataliwa na darasa zima kuwa haeleweki ama hajui kwa lugha ya wanafunzi? hao walimu wako lundo na ndio hatuwataki
 
ndugu sisi wengine hata hilo kokolo halijatubebelea watu kama 300+hatupo kwenye hayo majina toka sjut-dom,hivyo hi mada yako inatuuma sana?
haya malalamiko ni ya msingi na ninadhani anaepaswa kutoa majibu ni wizara, ama ndo ulikuwa mchujo wao wakaamua kuchuja chuo kizima?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…