Ajira za wageni kurahisishwa Ujerumani

Ajira za wageni kurahisishwa Ujerumani

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Serikali ya Ujerumani hapo jana umetia saini mpango wa kuwasajiri wakazi wasio katika Umoja wa Ulaya kwa lengo la kuziba pengo la wataalam katika sekta ya ajira.

Hatua hiyo inatekelezwa baada ya mkutano wa kilele uliowakutanisha wawakilishi wa makampuni na vyama vya wafanyakazi. Rasimu ya makubaliano iliyoridhiwa mwishoni mwa mkutano huo imetaja mipango ya kufuta ukiritimba sugu wa taratibu za Kijerumani na kulifanya taifa kuwa rafiki zaidi kwa wafanyakazi wa kigeni.

Mpango huo utatoa usaidizi kwa wafanyakazi wapya kupata mafunzo ya lugha ya Kijerumani, kutafuta eneo la kuishi. Na makampuni pia yatatoa nafasi zaidi za kazi zitakazo walenga wageni.

Serikali kwa upande wake imekubali kuongeza kasi ya kutoa viza kwa haraka ili kuwawezesha wafanya kazi kuanza majukumu yao haraka. Kwa hivyo kutambua sifa za mfanyakazi wa kigeni kutarahisishwa.

Ujerumani inahitaji wahandisi katika fani ya umeme, wataalamu katika sekta ya vyuma, upishi, uuguzi, huduma za wazee na fani ya kopyuta.
 
Germany is developed country sidhani kweli kama wanahitaji wataalamu katika fani Tajwa muda mwengine mambo huwa yanawekwa kisiasa ili kwa outsiders Waone kama Germany ni nchi inayosapoti wageni

Mfano mdogo kunawanafunzi flani from Germany walikuja tukafanya nao kozi fupi pindi nilipokuwa chuo walituonesha ukaribu wa hali ya juu, they were charming and very friendly na contacts zetu wakachukua tukabadilishana contacts sasa banaaa hahaha program ilipoisha walivyoondokaa ndo kimoja hata ukimtext aliyekuwa mtu wa karibu kipindi cha ile kozi hakujibu sio WhatsApp wala calls hawapokei hahahahaaa.... yaani hata Hi...! How are you friend? Wanaiblue tick then kimyaaaaaa

Nahisi kuna mambo yanawekwa kisiasa zaidi refer kozi za Petroleum ( mafuta na gesi) kwa hapa nyumbani kipindi cha Kikwete.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali ya Ujerumani hapo jana umetia saini mpango wa kuwasajiri wakazi wasio katika Umoja wa Ulaya kwa lengo la kuziba pengo la wataalam katika sekta ya ajira.
Ujerumani inahitaji wahandisi katika fani ya umeme, wataalamu katika sekta ya vyuma, upishi, uuguzi, huduma za wazee na fani ya kopyuta.
Wanatafuta cheap labour .
 
Back
Top Bottom