Ajira zote za jeshi la polisi zianzie ngazi ya Diploma

Ajira zote za jeshi la polisi zianzie ngazi ya Diploma

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ili kuboresha utendaji na weledi wa Jeshi la Polisi nchini ni vyema serikali ikaweka kigezo cha elimu kama kipaumbele kwa ngazi zote za polisi.Hii ni kutokana na umuhimu na unyeti wa kazi za ulinzi wa usalama wa raia na mali zao.

Waajiriwe vijana waliomaliza diploma, digrii na masters tu katika jeshi la polisi. Hakuna sababu tena ya kuendelea kuajiri watu ambao hawajafika kiwango hicho cha elimu kama tunajinasibu tunaipa elimu kipaumbele katika nchi yetu, pia vijana wa ngazi hizo za elimu wamejaa mitaani wakizurura na bahasha zao kutafuta ajira na wengine wameanza kuendesha boda boda kitu ambacho ni matumizi mabaya ya rasilimali watu.

Tulifanye jeshi la polisi kuwa la kisasa kwa kuipa elimu kipaumbele katika ajira zake kwani inawezekana.
 
Aisee

Screenshot_20210405-074523~2.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha ubinafsi. Kwa kuwa wewe umefikia kiwango hicho ndio unaona wale ambao hawakufika level hiyo hawapaswi kupata ajira hizo,unajiangalia wewe tu kama mtu mwenye pesa anapendekeza watu watoe mchango mkubwa kuliko uwezo wao kwa kuwa yeye anaumudu, waache wanaomaliza form four wapate pa kuanzia maisha zamani watu walikuwa wanamaliza la saba wanapata ajira ndio waliokufikisheni hapa mlipo.

Huko katika jeshi la polisi wenye hizo diploma, degree na masta wewe unadhani hawapo au umeamua kuwadharau polisi Tz.
 
Kiwango hicho cha elimu kiwe kwa ngazi zote, sio maofisa tu.
Acha ubinafsi. Kwa kuwa wewe umefikia kiwango hicho ndio unaona wale ambao hawakufika level hiyo hawapaswi kupata ajira hizo,unajiangalia wewe tu kama mtu mwenye pesa anapendekeza watu watoe mchango mkubwa kuliko uwezo wao kwa kuwa yeye anaumudu, waache wanaomaliza form four wapate pa kuanzia maisha zamani watu walikuwa wanamaliza la saba wanapata ajira ndio waliokufikisheni hapa mlipo.

Huko katika jeshi la polisi wenye hizo diploma, degree na masta wewe unadhani hawapo au umeamua kuwadharau polisi Tz.
 
Kazi pekee ya kujitolea ni kanisani au msikitini. Haya mawazo yako yalikuwa ya enzi za ujima.

Kazi ya jeshi ni kazi ya kujitolea Kama ilivyo kada ya ualimu

"Kazi kubwa maslahi madogo"

Ukiweka wasomi wengi wataangalia maslahi yao kuliko kuangalia kazi
 
Police kuna graduate wa kutosha na dip nyingi sana. So kwenye mgawanyo wa majukumu lazima F4 nao wawepo
 
kwa taarifa tu Polisi Tanzania ndio jeshi lenye wasomi wengi Tz.

Tatizo ni moja ya kazi za Amri
 
Mbona hilo lilishawekwa wazi kuwa asilimia kubwa ya majeshi yana hitaji watu wenye elimu ndogo ya form 4, kwani ndio wenye majukumu mengi kwenye majeshi kulinganisha na hao wasomi, hao wasomi huwa ni wasumbufu sana, mtu anatafuta kazi kama kujiegesha tu, huko anakosubiria penye maslahi mazuri tu pakitiki anakimbia, kingine wanakuwa wasumbufu sana kudai maslahi, mala kwenda kutaka kuongeza elimu.

Lakini ukimchukua form 4, hadi aje ajiendeleze apate digrii sio leo, kama ni kwata ameshapigishwa sana, na huwa wanakuwa wavumilivu.
 
Kuna mengi usiyoyajua katika majeshi, sio kosa lako.
 
Polisi/jeshi ni kazi za amri na sio kazi za kutumia akili nyingi, mtu yeyote mwenye akili timamu, mkakamavu na mwenye uzalendo anaweza kua polisi/mwanajeshi.
 
Mkuu F4 ndio hawa wanaolinda mabenki usiku na magetini

Wenye ma degree huwa hawalindi wanakaa ofisini tu saa 8 huyo kaondoka zake.
 
Hivi mtu mwenye digree ukampe kazi ya kulinda atm bank kweli si bora nibaki stendi napiga debe?

Tena hii kuajiri wasomi wasomi kwenye vyombo vya ulinzi ndio wanasababisha maadili yanapungua maana mtu ana elimu yake utamwambia nini.

Mi naona waajiri wala ma feria kabisa ili wawapelekeshe vizuri maana wanakuwa na adabu na utii na nidhamu ya kazi kuliko hiyo misomi alafu kicwani hamna kitu.

Angalia wastaafu wote kwenye vyombo vya ulinzi wale wa enzi za mwalimu walivyo na nidhamu na weledi huko mtaani alacu ulinganishe na hawa wa saa hivi uone tofauti
 
Hao wenye diploma wataweza kukaa magetini? Kulinda benk?

Kufukua makaburi kama kuna kesi za mtu kuuwa na kuzika?
 
Kama wanaweza kuendesha bodaboda na kuwa wamachinga kwa nini washindwe kulinda benki na kufukua makaburi.
Hao wenye diploma wataweza kukaa magetini?Kulinda benk?

Kufukua makaburi kama kuna kesi za mtu kuuwa na kuzika?
 
Wasomi wengi ni ngazi za maafisa, huku chini ni form 4 ndio wengi.
kwa taarifa tu Polisi Tanzania ndio jeshi lenye wasomi wengi Tz.
Tatizo ni moja ya kazi za Amri
 
kwa taarifa tu Polisi Tanzania ndio jeshi lenye wasomi wengi Tz.
Tatizo ni moja ya kazi za Amri
Zaidi ya Polisi 20 ni PhD holders
Zaidi ya Polisi 100 wana masters
Zaidi ya Polisi 6000 Tanzania wana digrii,
Zaidi ya Polisi 1000 wana diploma
Zaidi ya Polisi 4000 ni form VI

Waliobaki ndo form iv na Std VII wasiozidi 500 kwa sasa.

Kama unaona polisi wanafanya vibaya si kwa sababu wote hawana Elimu, ila ni kwa sababu si chombo huru toka kwenye mikono ya wanasiasa. Hao uliosikia wameteliwa jana wanakwenda kutoa amri kwa Polisi kufanya chochote wanachoona wao kinafaa, na kama OCD husika hajiongezi ndo utakuta madudu na mafyongo kama ya Kaliua juzi ambako DC anasema "familia ilipanga mtoto wao afe kwa moto ili kuikomoa serikali".
 
Back
Top Bottom