Ajizi nyumba ya umaskini na siio njaa!

Ajizi nyumba ya umaskini na siio njaa!

Mkandara

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2006
Posts
15,806
Reaction score
9,011
Wanabodi,

Leo hii baada ya kutafakari kwa kina juu ya swala zima la Katiba mpya likifuatiwa na kile wanachokiita changamoto juu ya Muungano na kero zake kwa wananchi wa pande mbili za Muungano. Kusema kweli nawashangaa sana wasomi wa nchi yetu, wengine ni Maprofesa na watu wanaojiamini ama kuaminiwa kuwa wanaweza kutupatia katiba bora inayotokana na wananchi hivyo wazitumie elimu zao ipaswavyo lakini sivyo!.

Baada ya kusikiliza hili bunge la Katiba na wajumbe wake wakipewa fursa ya kuzungumzia hoja zao juu ya muundo wa Muungano. Kwanza kabisa nimegundua kwamba sii wajumbe wengi wanafahamu asili ya muungano wetu, wengi wao wana maswali zaidi ya kuwa wao ndio walochaguliwa kupata ufumbuzi wa swala la katiba mpya. Ni madakatari wasojua ugonjwa huu ila wapo kujifunza na kujua ukweli wa gonjwa hili la Muungano. Na kinachochefua zaidi hasa kwangu mimi mwananchi msikilizaji, ni pale mjumbe wa baraza hili anaposimama na kuzungumzia mapungufu ya upande wa pili lakini asiweze kuzungumzia mazuri ya kile anachoki support kuwa ndio mbadala wa mahitaji ya wananchi wa pande zote mbili.

Ndio kusema hata wale wanaosema serikali 2, wameshindwa kueleza ni mabadiliko gani yatafanyika ili kuondoa kero zilizopo ama pia wale wanaotaka serikali 3 wameshindwa kuelezea mazuri ya serikali hizo 3 pasipo kunukuu (copy and Paste) rasimu ya katiba ilopendekezwa na tume ya Warioba. Na isitoshe wajumbe wote hawafahamu ya kwamba dhumuni kubwa la kurusha kongamano hili la baraza la Katiba live ktk luninga -TBC television ni kuwapa fursa hawa wajumbe kuwashawishi wananchi juu ya pendekezo lao la katiba hii ili siku itakapo pelekwa kwao wataiunga mkono kwa asiliimia kubwa.

Kibaya zaidi, na ajabu kubwa sana ni kwamba, hawa wajumbe hawa wanaodai serikali 3, wanashindwa kueleza ukweli ya kwamba ili serikali ya Tanganyika iundwe upya yaani itoke ktk tumbo ya Tanzania na kuwa hai ni lazima Muungano uliopo uvunjwe maana Tanganyika ipo na wanakubali uwepo wa Tanganyika ndani ya katiba tulonayo.. Pili, na ili muungano uwe wa Ushirika (Federation) ktk serikali 2 au 3 ni lazima muungano huu (political Union) ufe kwanza na waasisi wake hawatakuwa tena Mwalimu Nyerere wala Karume maana sababu zile za miaka ya 60's hazipo. Je ni sababu zipi? wananchi hatuzijui!.

Sasa nizungumzie, AJIZI hii kuwa nyumba ya UMASKINI.

Muda mrefu sana sisi wote tumekuwa tukijiuliza maswali kwa nini Tanzania ni maskini? hao hao wasomi wamekuja na kila aina ya sababu lakini sababu zote zimekuwa amakutokana na kero wala sii wao wahusika ila kundi jingine iwe CCM au wananchi wenyewe wavivu wa kazi, kumbe ukweli unabakia kuwa UMASKINI wetu unatokana na UVIVU wa sisi sote KUFIKIRI,Uvivu wa ubunifu na tafakari za kina juu ya mahitaji ya wananchi isipokuwa kero zinazoweza kuwaondoa ktk uongozi ama majukumu walokabidhiwa - Kero zimekuwa sababu. Hivyo ndio kusema uvivu wa kufikiri ni nyumba ya njaa na nyumba ilokuwa na njaa hujiwa na UMASKINI!.

Nitawapeni mfano mdogo sana niloushuhudia hapa Dar es Salaam.
Majuzi tu Manispaa zote za mkoa wa Dar es Salaam zilifanye Operation Usafi wa jiji hili. Ni wazo zuri sana tena hakuna jambo zuri ktk afya na usalama wa mwanadamu kama usafi. Na hakika mji wa Dar ulikuwa na kila sababu ya kufanya operation hii ili kuusafisha mji. Hakuna mtu anayependa Uchafu isipokuwa ni tabia ya baadhi ya watu kutokuwa na ustaarabu wa kuelewa athari za uchafu.

Sasa itazame ajizi ya Mtanganyika. Maamuzi yalofikiwa kuusafisha mji ilikuwa kuwafukuza watu wote wenye vibanda pembezoni mwa nyumba hata za biashara. Nilishuhudia watu wakivunjiwa majiko yao, mali zao zikitupwa na nyingine zikikusanywa kama uchafu wa mji lakini baada ya zoezi hili kubomoa vibanda vyote sikuona gari hata moja la kusafisha sehemu ile walobomoa mabanda yale ili kutoa mfano wa usafi!.

Nitarudia tena, USAFI wa mji ni kuondoa uchafu wa bidhaa zilizokwisha tumika ama kuuzwa, usafi ni kusafisha mazingira wanayofanyia kazi hawa wachuuzi na sii kweli kabisa kwamba uchafu wa mji ni hizo BIDHAA wanazouza kwa wananchi ili kukidhi wahitaji ya wananchi. Demand ipo kubwa lakini hatuna masoko ya kutosheleza. Zaidi ya hapo hawa wachuuzi kama wangesisitizwa kusafisha maeneo yao kila baada ya kazi, mji huu usingekuwa mchafu, hivyo Ajizi ya Mtanganyika ipo ktk kufikiri, kubuni na kutoa maamuzi yanayokidhi hoja ama mahitaji yaliyopo isipokuwa wepesi wa kuhofia kero!.

Mnaweza kusema hawa wachuuzi hawasikii lakini tazama basi, hivi kweli Manispaa za mji zinawezaje kukusanya tozo la siku kwa hawa hawa wachuuzi kila siku lakini washindwe kusimamia usafi? Je haiwezekani manispaa hizi hizi kuwatoza faini kubwa wale waloshindwa kuacha sehemu zao za kazi safi? Isipokuwa jibu rahisi kwao ni kubomoa vibanda vyote vya wachuuzi bila kujali gharama walizoingia ama kusababisha upungufu zaidi wa bidhaa hizona upandaji wa bei za mazao na matunda kwa walaji. Hivi kweli zoezi hilo litaleta Usafi mjini ama ndio linaongeza matatizo zaidi hata kwa walaji?

Tazama swala la Usafiri, Hivi kweli ili kuuweka mji wetu safi unaweza kufukuza Bodaboda na daladala zote toka mjini bila kuhakikisha kwamba kuna usafiri wa kutosha kutoka mjini hadi vitongoji vyake? leo hii wananchi wanalipa hadi Tsh 1000 hasa saa za jioni kutokana na maamuzi ya viongozi kuondoa Kero na msongamano na misululu ya magari mjini. Lakini basi ndio kusema wananchi wanakosa usafiri hivyo kuchelewa kurudi makwao hadi usiku mkuu. Hivyo ndio kusema makosa makubwa ya Mdanganyiika ni katika kufikiri na ubunifu ktk maamuzi yanayojenga na sii kubomoa. Leo hii ukiweka mabus ya kutosha kwa jiji la Dar es Salaam, bila shaka hizo Daladala na Boda boda zitapotea zenyewe. Nai anapenda kubanana ndani ya hizi daladala ama kupakiwa na bodaboda ambazo usalama wake ni kwa rehma ya Mungu! Hivyo hivyo uchafu wa mji ni Taka zinazotupwa hovyo mabaraabani iwe na wanunuzi, walaji ama wachuuzi wenyewe ndio dawa ya usafi wa mji sio bihaa inayouzwa..

Nini basi sababu ya kutumia mifano hii kuhusiana na kichwa cha mada hii AJIZI NYUMBA YA UMASKINI.

Wazungu wanasema hivi:- Necessity is the mother of invention - Mahitaji ni mama wa ubunifu.
Hii ni methari nzito sana na kwa ujumla wake ndio siri ya MAENDELEO na UTAJIRI wa mtu, watu na nchi. Ni sehemu inayokidhi hoja zote za huduma, kiuchumi, kisiasa na hata maisha ya kila mmoja wetu. Ila sote tunatofautiana ktk ubunifu na maamuzi ktk kukidhi mahitaji haya, na hapo ndipo sisi tunakwama kwa sababu tunashindwa kufikiri, tumeshindwa ubunifu ila huchukua njia rahisi zaidi kuondoa kero zilizokuwepo.

Kwa nini basi tunachukua njia rahisi? nimekuja gundua kwamba sisi Watanzania ama waafrika tuna hulka ya kutokidhi MAHITAJI. Huacha mahitaji hayo yawe ktk hali liyopo hadi inapokuwa KERO. Tazama jiji la dar linavyokuwa ilihali sewerage system yake ni ya toka mwaka 1950..Akili kweli?..Majengo yanapanda juu tu huku chini kunanuka! iNa ikisha fikia kilele za kero hutafuta njia na mbinu za kuondoa KERO hizi na sii MAHITAJI yalozaa KERO hizo. Hivyo unaweza kuondoa kero kwa muda lakini hutaweza kuondoa mahitaji (necessity) kwa kutumia suluhisho la Kero. Ni sawa na mgonjwa wa Malaria anapokunywa Panadol kutuliza homa ya kichwa!

Itaendelea
 
Mkandara, unapolaani wanaotaka Tanganyika kwa kuangalia factor chache na kufumbia macho zingine hutendi haki. Ningesema kuwa kabla ya mchakato kura ya maoni na mkutano wa kitaifa kuamua hatima na mwelekeo wa taifa ingeanza.

Hapo ndipo tungepata muafaka wa kuwa na Union, Federation au confederation and in worst case scenario kugawana mbao.
Nadhani umechagua pa kuongelea hukusema kwa ujumla au udhati wake

Kuhusu usafi wa Jiji, tatizo halipo kwa serikali wala wananchi. Tatizo lipo kwa viongozi wa taifa hili. Si mara moja au mbili kampeni zimefanyika.
Kumbuka kuwa usafi ni utamaduni mtu anao ukuta akizaliwa na kukua nao.

Leo ukija kwa wenzetu mtoto hawezi kutupa takataka kwasababu hakuzoea na anajua ni kitu kibaya. Tanzania hata kujisaidia bara barani ni jambo la kawaida.

Kila usafi unapodanyika kuna watu wanaoitwa viongozi wa CCM wanasema ni kero kwa wananchi. Kuna viongozi wa serikali waliopo bize ku-score political point' zaidi ya kutenda kwa uhalisia.

Machinga complex ni mokawapo ya uchafu ulioletwa na viongozi tena wajuu wan chi hii.

Lazima tukubaliane kuwa nchi inaongozwa kwa utaratibu. Kuondoa boda boda sidhani kama ni jambo baya. Ubaya ni pale zoezi linaposhughulikiwa na wahuni na kwa uhuni

Juzi kumetokea mafuriko Dar, kiongozi anasema hawezi kuzuia mvua. Kiongozi aliyepaswa kuwa in the ground akitoa logistic na management ya maafa yupo kwingine

Kusafisha jiji ni jambo zuri, ubaya ni kuwa halifanyiki kitaalam ni siasa tu zinaendelea.
Hakukuwa na maandalizi yanayohusisha shughuli hiyo na huenda hata bwana afya wa jiji hajui operesheni hiyo.

Wapi twende?
Kwanza ni kuhakikisha kuwa tunafumua status quo, tunaleta discipline kama maeneo yote na tunajifunza utamaduni wa kufikiri na kutenda.
Hatuwezi kubaki hapa tulipo tukitegemea matokeo tofauti.
 
Kwa Mtanzania kila kitu kwake ni DILI, awe raia wa kawaida au kiongozi wote wanafanana. Hata usalama wa nchi na uhai wa watu wanaufanya kuwa dili kwa maslahi yao binafsi, hasa political gains. HATUTAFIKA!
Hili ni suala la Mindset, na chanzo kikubwa kabisa cha Fikra hizo Mfu ni systems kutanguliza KITU kama determinant ya thamani ya mtu badala ya UTU. Kipaumbele ni KITU, watu ndicho wanachotafuta kujenga heshima, awe mwanasiasa ama mkulima ama mfanyabiashara, KITU KWANZA!
Mbele ya KITU hakuna kinachoshindikana kuwa dili kwao, iwe Utanganyika, ama afya za watu, usalama wa taifa, hata uhai wetu, kwao ni KITU KWANZA hadi IKULU kwao ni dili! Ni Ulimbukeni na Upuuzi tupu!
Katiba nayo imefanywa kuwa dili la watu, HATUTOKI. Ubunifu haujawahi kufika mwisho. Tukae chini tuumize vichwa. TUNAWEZA. Nguvu yetu ni Umoja na Kuthubutu!
Anaita sasa!
 
Mkandara, unapolaani wanaotaka Tanganyika kwa kuangalia factor chache na kufumbia macho zingine hutendi haki. Ningesema kuwa kabla ya mchakato kura ya maoni na mkutano wa kitaifa kuamua hatima na mwelekeo wa taifa ingeanza.

Hapo ndipo tungepata muafaka wa kuwa na Union, Federation au confederation and in worst case scenario kugawana mbao.
Nadhani umechagua pa kuongelea hukusema kwa ujumla au udhati wake

Kuhusu usafi wa Jiji, tatizo halipo kwa serikali wala wananchi. Tatizo lipo kwa viongozi wa taifa hili. Si mara moja au mbili kampeni zimefanyika.
Kumbuka kuwa usafi ni utamaduni mtu anao ukuta akizaliwa na kukua nao.

Leo ukija kwa wenzetu mtoto hawezi kutupa takataka kwasababu hakuzoea na anajua ni kitu kibaya. Tanzania hata kujisaidia bara barani ni jambo la kawaida.

Kila usafi unapodanyika kuna watu wanaoitwa viongozi wa CCM wanasema ni kero kwa wananchi. Kuna viongozi wa serikali waliopo bize ku-score political point' zaidi ya kutenda kwa uhalisia.

Machinga complex ni mokawapo ya uchafu ulioletwa na viongozi tena wajuu wan chi hii.

Lazima tukubaliane kuwa nchi inaongozwa kwa utaratibu. Kuondoa boda boda sidhani kama ni jambo baya. Ubaya ni pale zoezi linaposhughulikiwa na wahuni na kwa uhuni

Juzi kumetokea mafuriko Dar, kiongozi anasema hawezi kuzuia mvua. Kiongozi aliyepaswa kuwa in the ground akitoa logistic na management ya maafa yupo kwingine

Kusafisha jiji ni jambo zuri, ubaya ni kuwa halifanyiki kitaalam ni siasa tu zinaendelea.
Hakukuwa na maandalizi yanayohusisha shughuli hiyo na huenda hata bwana afya wa jiji hajui operesheni hiyo.

Wapi twende?
Kwanza ni kuhakikisha kuwa tunafumua status quo, tunaleta discipline kama maeneo yote na tunajifunza utamaduni wa kufikiri na kutenda.
Hatuwezi kubaki hapa tulipo tukitegemea matokeo tofauti.
Mkuu wangu itabidi nianze na hoja yako kwanza kabla sijaendelea..

Mimi nimezungumzia kwa ujumla wake, sikuwatenga wa serikali 3 dhidi ya 2 au 1, isipokuwa nachojaribu kuelezea hapa ni kile nilichogundua miye baada ya kusikiliza hoja za wabunge na kwa bahati nzuri sana nipo mujini nawasikia wananchi wakidai serikali 2 au 3 kwa kutazama KERO pasipo kujua ya kwamba KERO zote ni matokeo ya kutotosheleza MAHITAJI muhimu ya Muungano huu kwa zaidi ya miaka 30 na wala wasijiulize hayo mahitaji tuloyaacha kwa muda mrefu sana ni yapi yana uzito zaidi!.

Kwa maana ya kwamba usipotosheleza mahitaji - (DEMAND)kwanza na wakati inapohitajika basi fahamu kinachofuata ni KERO kwa wananchi. (kumbuka wakati wa foleni ya sukari na chunvi) na kama utaumiza kichwa chako kukidhi kero hizi ndio hapo utakapo fikia kupata majibu na maamuzi hovyo kabisa kama inavyotokea huko Bungeni. Hata huo usafi wa jiji la Dar ni matokeo ya kuficha aibu ya kero za uchafu wetu wenyewe. Nenda Ulaya utakuta wenye maduka wanaweka bidhaa zao nje ya duka na tofauti baina yao na sisi ni Usafi tu. Wao wakisha funga maduka yao huhakikisha mali yote imerudi ndani na sehemu imesafishwa. Leo hapa kwetu hata mwenye Hotel analazimishwa kuchoma nyama choma (barbeque) ndani ya jengo pasipo kujali safety kwa wakazi wengi maana moto wa jiko la Barbeque ni hatari ndani ya nyumba na rahisi kabisa kutateketeza nyumba nzima. Uliona wapi Barbeque uinafanyika ndani ya Hotel pasipo ventilation system _ wateja wakilia na moshi mkali wa viungo?.

Sasa leo kina sisi ambao kwanza hatuna vifaa vya kutosha, hatuna maduka ya vyakula ya kutosha, hatuna hata soko kuu la kutosheleza ugawaji kwa kila wilaya, Hatuna Hospital za nguvu kila wilaya na kadhalika..Tunafikia maamuzi ya kuvunja vibanda kutokana na KERO za uchafu ambao unaweza kutokana na wanunuzi wenyewe ama halmashauri yenyewe kutokuwa na vifaa vya kutosha kukusanya uchafu wa mji mitaa yote kwa usiku mmoja!. Maajabu ya Mussa katika zoezi hili kina Mama ntilie hawaguswi! Hii ndio Ajizi ya Mdanganyika!

Mji sehemu kubwa unanuka, pengine wenzangu wamezoea hizi harufu lakini mtanisamehe kwa hilo! Na hizi mvua zimekuja kutuadhirisha zaidi yaani ukiona uchafu ulokusanywa huko Jangwani, Mabibo, Ilala, Buguruni, Kigogo na sehemu zote za mafuriko na masoko inatisha..Hii ni Kutuonesha kwamba Uchafu wa mjii huu hautokani na mabanda ya wachuuzi isipokuwa ni uchafu na mabaki ya taka zilizoachwa pasipo kukusanywa na kupelekwa kunakostahiri. Uwezo wa manispaa mdogo na kwa bahati mbaya mila ya Mdanganyika haina ustaarabu wa usafi zaidi ya kuficha uchafu uvunguni maana wanajua hakuna huduma wala mahala pa kuutupa uchafu huo ila kuuchoma moto.

Nirudi ktk swala la wale wanaotaka serikali 3, Hadi leo hii zaidi ya Lipumba na Zitto sikusilkiliza hoja yoyote yenye mvuto kwangu. Lakini pamoja na hoja yenye mvuto mkubwa ya Lipumba kamalizia vibaya sana kuonesha wazi kwamba Muungano wetu wa serikali 3 unaweza fikia hatma kama ilotokea leo bungeni!. NI uhuru huo huo walokuwa nao wa mamlaka ya vyama na taasisi umetufika hapo. Hivyo ni dhahiri pande mbili zisizokubaliana ni rahisi kabisa moja kujikata maana RUKSA imetolewa kikatiba na wala sii ndugu tena . Ni rahisi sana kwa mZanzibar au Tanganyika kusema siutaki muungano huu maana nalindwa kisheria na hakika nchi zetu sii moja ila ni mkataba wa shirikisho.

Na labda nigusie tu kusema ya kwamba hawa wabunge wote wa bunge hili la Katiba wanazungumzia KERO za muungano wakasahau kwamba KERO ni matokeo tu ya kukosekana ufumbuzi wa MAHITAJI muhimu ka muda wa miaka 50 na ndio maana yakawa kero sasa. Hivyo uamuzi wa wajumbe wote kuhusu serikali 1, 2 na 3 ni suluhisho la KERO sio MAHITAJI yalosababisha hizi kero. Kwa hapo nampongeza sna Kiongozi Zitto wka kusema wazi kwamba serikali 1, 2 wala 3 sio tatizo la Muungano wetu ila yapo maswla muhimu sana tumeyaacha kwa miaka 50 hadi yamekuwa kero.

Sasa kama kweli hawa wasomi wanajua wapi pa kuanzia wasingepoteza mabillioni ya fedha kuandika rasimu, kuunda bunge na kadhalika ili kuandika katiba mpya ambayo kwa miujiza kabisa swala la Muungano limeingizwa. Hii akili kweli? Leo hii tunajadili KERO badala ya kufikiria ni MAHITAJI yapi yalokosekana kwa miaka 50 ambayo yanatakiwa kurekebishwa iwe ktk katiba hii ama kimkataba maana katiba na mikataba wa Muungano ni vitu viwili tofauti kabisa.

Ni ujinga olioje leo hii viongozi wetu wanachukua muda mrefu sana kujadili KERO hali wakijua fika kwamba Muungano sio sababu ila ni kero yaani matokeo ya kudharau mahitaji yetu kwa muda mrefu.?.. Maana hata ukiunda serikali 3 bado tutakuwa na serikali kuu ambayo nina hakika viongozi wa bara watakuwa dominant. Sasa ikiwa hivyo bado Bara haitawanyima Zanzibar fursa zile zile walizozikosa wakati wa serikali 2 maana serikali kuu ndio huomba mikopo kwa kutumia jina la Taifa na si nchi shiriki.

Angalia basi imefikia watu kusema rais wa Jamhuri asiwe na mamlaka makubwa zaidi isipokuwa kwa wizara za Muungano. Jamani eeeh nchi za wenzetu, kweli wqanafanya hivo? hivi kweli Obama hana mamlaka makubwa? maana serikali inayotolewa mfano ni shirikisho la Marekani wasijue shirikisho hilo limepatikanaje!

Na serikali inaposema mambo yasiyokuwa ya muungano ni sheria ambazo kila nchio itachagua kufuata kwa mfano Afya! tazama Marekani kila state ina shughulikia maswala yake ya AFYA lakini haina maana hata mapato yake hayakusanywi ktk serikali ya Muungano. Eklimu bado ni wizara ya Taifa (serikali ya Muungano isipokuwa kila nchi inapewa mamlaka kamili ya kuendesha wizara hiyo. Canada vile vile ukienda Quebec utakuta sheria za Afya na kodi zake tofauti na Ontario lakini fedha ya mauzo ya huduma zake asilimi 8 inakwenda serikali kuu, hakuna swala lisilokuwa la Muungano isipokuwa malamka ya kutoa huduma hiyo ndio maana ya maneno haya.

Sisi na hiyo rasimu yetu tunapendekeza nini? ati leo kuna mjumbe mmoja wa Znz (serikali 3) anadai ya kwamba Waziri wa Kilimo wa serikali kuu toka bara anapokwenda Zanzibar kuzungumzia Kilimo, anahoji - inahusu?. Sasa nambie hii kweli ndio serikali 3 mnayoitaka? yaani waziri wa kilimo wa taifa asifike Zanzibar kwa sababu tu ni mtu Bara ati wanajitosheleza ni akili hii?! Je, what if (ikiwa) waziri huyo ni Mzanzibar itakuwaje? naye Bara asifike japo ofisi yake iko bara?..

Huu ujinga huu ndio mimi naulaani maana kwa kila navyowasikiliza wajumbe wote nimegundua kwamba wanatumia akili na elimu zao kuondokana na KERO, na hakika njia zote zinaweza kuwa safi lakini sii gonjwa tulonalo. Hii ndio AJIZI NYUMBA YA UMASKINI.. tusijiulize sana kwa nini sisi maskini, lisikilize sana bunge hili utagundua sababu za umaskini wetu maana zipo wazi kabisa...
 
Angalia basi imefikia watu kusema rais wa Jamhuri asiwe na mamlaka makubwa zaidi isipokuiwa kwa wizara za Muungano. Jamani eeeh nchi za wenzetu, serikali inaposema mambo yasiyokuwa ya muungano ni sheria ambazo kila nchio itachagua kufuata kwa mfano Afya! tazama Marekani kila state ina shughulikia maswala yake ya AFYA lakini haina maana hata mapato yake hayakusanywi ktk serikali ya Muungano. Eklimu bado ni wizara ya Taifa (serikali ya Muungano isipokuwa kila nchi inapewa mamlaka kamili ya kuendesha wizara hiyo. Canada vile vile ukienda Quebec utakuta sheria za Afya na kodi zake tofauti na Ontario lakini fedha ya mauzo ya huduma zake asilimi 8 inakwenda serikali kuu, hakuna swala lisilokuwa la Muungano isipokuwa malamka ya kutoa huduma hiyo ndio maana ya maneno haya.
Naomba nichangie nikidokoa dokoa ili kukidhi haja ya mjadala.
Mkuu Mkandara, Quebec siyo nchi ni jimbo nchini Canada.
Lina waziri wa jimbo(Premier) lakini si waziri mkuu Prime minister. Kuna sheria zinazotambulika kila jimbo, hata leseni zinatofautiana kwa viwango na usajili wake.

Znz ni nchi ina wimbo wake, bendera, Bunge na kila kitu kwa mujibu wa katiba ya 2010.
Quebec hawana mamlaka ya kuhoji uhalali wa katiba ya Canada au hawana uhalali wa kuondoa jambo au kuongeza bila federal government kujua. Zanzibar wanaweza kuzuaia hoja za JMT

Kuhusu Uchangiaji, Quebec kama jimbo wanachangia federal government kama majimbo mengine.Znz kama nchi haichangii chochote katika muungano.

Kama unafuatilia habari Quebec waliataka kujitenga wakati wa Pierr Trudeau.
Referendum ikapendelea kuwepo kwa shirikisho.

Nao kama znz kelele haziishi ingawa ni jimbo masikini. Wanapata ruzuku kutoka majimbo mengine kama Zanzibar na mchango wao ni almost nil kama Zanzibar.

Tofauti na Zanzibar Quebec wanachangia kile walicho nacho kidogo kama ishara ya kuwajibika, Zanzibar ikiwa ni nchi zaidi ya jimbo la Quebec inachukua hata isichostahili wala haijishughulishi kujua gharama za muungano zaidi ya kudai mapesa na vyeo kila uchao

Uchaguzi wa premier wa Quebec majuzi ulileta kizaazaa, kama ulifuatilia habari za media.
Hoja ya kujitenga ikajirudia tena.

Majimbo mengine ya Canada yakasema sasa inatosha, Quebec ni wategemezi lakini hawaishi gubu kama Zaznibar. Kama wanataka kuondoka to hell waende zao.
Majimbo yamechoka kama ilivyochoka Tanganyika.

Hivyo kuna similarity za Quebec na Znz kitabia, gubu, kuchukua na kutokutoa.
Kuna tofauti kati ya Quebec na Znz kwasababu moja ni jimbo na nyingine ni nchi.
Mfano wako haujakidhi na haujitoshelezi.
 
Naomba nichangie nikidokoa dokoa ili kukidhi haja ya mjadala.
Mkuu Mkandara, Quebec siyo nchi ni jimbo nchini Canada.
Lina waziri wa jimbo(Premier) lakini si waziri mkuu Prime minister. Kuna sheria zinazotambulika kila jimbo, hata leseni zinatofautiana kwa viwango na usajili wake.

Znz ni nchi ina wimbo wake, bendera, Bunge na kila kitu kwa mujibu wa katiba ya 2010.
Quebec hawana mamlaka ya kuhoji uhalali wa katiba ya Canada au hawana uhalali wa kuondoa jambo au kuongeza bila federal government kujua. Zanzibar wanaweza kuzuaia hoja za JMT

Kuhusu Uchangiaji, Quebec kama jimbo wanachangia federal government kama majimbo mengine.Znz kama nchi haichangii chochote katika muungano.

Kama unafuatilia habari Quebec waliataka kujitenga wakati wa Pierr Trudeau.
Referendum ikapendelea kuwepo kwa shirikisho.

Nao kama znz kelele haziishi ingawa ni jimbo masikini. Wanapata ruzuku kutoka majimbo mengine kama Zanzibar na mchango wao ni almost nil kama Zanzibar.

Tofauti na Zanzibar Quebec wanachangia kile walicho nacho kidogo kama ishara ya kuwajibika, Zanzibar ikiwa ni nchi zaidi ya jimbo la Quebec inachukua hata isichostahili wala haijishughulishi kujua gharama za muungano zaidi ya kudai mapesa na vyeo kila uchao

Uchaguzi wa premier wa Quebec majuzi ulileta kizaazaa, kama ulifuatilia habari za media.
Hoja ya kujitenga ikajirudia tena.

Majimbo mengine ya Canada yakasema sasa inatosha, Quebec ni wategemezi lakini hawaishi gubu kama Zaznibar. Kama wanataka kuondoka to hell waende zao.
Majimbo yamechoka kama ilivyochoka Tanganyika.

Hivyo kuna similarity za Quebec na Znz kitabia, gubu, kuchukua na kutokutoa.
Kuna tofauti kati ya Quebec na Znz kwasababu moja ni jimbo na nyingine ni nchi.
Mfano wako haujakidhi na haujitoshelezi.
Quebec ni nchi ina bendera yake, mahakama zake, na serikali yake kama ilivyo ktk majimbo mengineyo yote ya Canada. Marekani ni vivyo hivyo, states zote ni nchi na zina mamlaka kamili ya kuendesha shughuli zao isipokuwa ktk sheria zipo za Muungano na zipo zisizokuwa za muungano ila mapato ya states zote huchangia mfuko wa Taifa. Hakuna kodi usokuwa usokuwa na kisu cha asilimia ya serikali ya Muungano. Uliza yeyote..
Swala la wimbo halina mshiko maana hata sisi wakerewe tuna wimbo wetu wa Kikerewe ku identify Ukerewe wetu..
 
Mkandara: Sisis na hiyo rasimu yetu tunapendekeza nini? ati leo kuna mjumbe mmoja wa Znz (serikali 3) anadai ya kwamba Waziri wa Kilimo wa serikali kuu toka bara anapokwenda Zanzibar kuzungumzia Kilimo, anahoji - inahusu?.

Sasa nambie hii kweli ndio serikali 3 mnayoitaka?
yaani waziri wa kilimo wa taifa asifike Zanzibar kwa sababu tu ni mtu Bara ati wanajitosheleza ni akili hii?! Je, what if (ikiwa) waziri huyo ni Mzanzibar itakuwaje? naye Bara asifike japo ofisi yake iko bara?..
Mkandara alichosema huyo mjumbe ni kweli na naweza kusema ana akili sana.

Ni kweli waziri wa kilimo wa JMT hawezi na hapaswi kwenda kufanya kazi znz.
Ili kuweza kufanya kazi Zanzibar, kwa mujibu wa katiba 2010 ni lazima mtu awe mkaazi na apewe kibali cha kufanya kazi.

Mtanganyika hana haki hiyo ni sawa na Mnigeria au Mfilipino awapo znz.
Kwanini waziri aende kuomba kibali cha ukaazi na kazi ili aweze kuhimiza kilimo?

Waziri huyo akiwa mzanzibar atakuwa na nusu haki. Ni mkaazi haihitaji kibali cha ukaazi. Lakini anahitaji kibali cha kufanya kazi za consulting kutoka Tanganyika.

Ni kwa mantiki hiyo huyo mjumbe anajua kutumia logic, ana akili na ana maono. Tume ya Warioba ikasema mambo yawe 7 mengine kila mmoja awe na lake.

Lakini pia jiulize huyu waziri wa JMT anasababu gani za kwenda kuhimiza kilimo znz? Kuhimiza si maneno ni pamoja na kutoa mchango, pembejeo, mbole na wataalam. Huyu hajulikani znz sasa anakwenda kutoa nini?
wamba atoe pembejeo au wataalam znz badala ya Mwanza kunako mhusu.

PM Pinda anahitaji kibali kufanya kazi znz seuse waziri wa Kilimo!

Wewe unamuona mjumbe ni mjinga kwasababu kuna mahali hujaelewa.
Nina uhakika hata yeye anakuona hivyo kwa kuzingatia sababu hizi.;

Kilimo si jambo la muungano. Hakuna sababu za kutafuta kibali kwenda kufanya kazi nchi jirani.

Wewe unadhani ni waziri wa JMT ambayo znz wapo, ukweli ni kuwa huyu ni waziri wa Tanganyika. Unaishi kwa hisia ndio maana huuoni ukweli huo.

Upo katika state of denial hata pale wznz wanapokutupia virago, wewe unabaki kusema ni nduguzo.

Kilimo si suala la muungano, hivyo waziri wa JMT ni popo hajulikani kama ni ndege au mnyama.

Vipi, unaonaje kama tutatengeneza utaratibu wa kujua huyu ni kwelea kwelea na yule ni Eagle.

Huwezi kuwa na utaratibu huo kama una serikali 2.
Lazima utakuwa na kwelea kwelea na popo, halafu Mkandara analalamika kwanini popo haailikwi mkutano wa ndege, kwa upande mwingine anasema kikao cha jana cha wanyama popo ni mtovu hakuhudhuria. Unamuonea popo, mtafutie kundi.
 
Quebec ni nchi ina lake, mahakama zake, na serikali yake kama ilivyo ktk majimbo mengineyo yote ya Canada. Marekani vivyo hivyo..Swala la wimbo halina mshiko maana hata sisi wakerewe tuna wimbo wetu wa Kikerewe ku identify Ukerewe wetu..
Hapana Quebec ilikuwa ni nchi kama ilivyokuwa Ontario, New Bruzwinsk, zikajiunga Alberta, Nova Socatia na kutengeneza ferderation. Tofauti ni kuwa Quebec ilikuwa na Mfaransa zingine zikiwa ni Dominion chini ya Malikia.

Kwasasa kila jimbo lina kila kitu chake lenyewe. Premier wa Quebec hana uwakilishi UN na wala katika mambo mazitio kama ulinzi hana jeshi. Znz Rais wake ana jeshi, na katiba yake inayomtambua kwa ukuu mbele ya JMT.

Quebec hawana nafasi ya kuchezea katiba ya Canada, Zazibar wakiamua watu 50 wanaoitwa baraza la wawakilishi wanakaa na kunywa chai wakifikira nini wachomoe nini waongeze katika katiba ya JMT
 
Hapana Quebec ilikuwa ni nchi kama ilivyokuwa Ontario, New Bruzwinsk, zikajiunga Alberta, Nova Socatia na kutengeneza ferderation. Tofauti ni kuwa Quebec ilikuwa na Mfaransa zingine zikiwa ni Dominion chini ya Malikia.

Kwasasa kila jimbo lina kila kitu chake lenyewe. Premier wa Quebec hana uwakilishi UN na wala katika mambo mazitio kama ulinzi hana jeshi. Znz Rais wake ana jeshi, na katiba yake inayomtambua kwa ukuu mbele ya JMT.

Quebec hawana nafasi ya kuchezea katiba ya Canada, Zazibar wakiamua watu 50 wanaoitwa baraza la wawakilishi wanakaa na kunywa chai wakifikira nini wachomoe nini waongeze katika katiba ya JMT
Mkuu Nguruvi3, huu Muungano wetu hauwezi kufananishwa na muungano wowote hapa duniani kwa sababu hau"make" sense kwa namna yoyote ile. Nimekutana na watu wengi kutoka sehemu mbali mbali wakitaka niwafafanulie huu muungano unavyofanya kazi. Nasikitika kusema kwamba sijampata mtu hata moja aliyeonesha hata kachembe cha uelewa ninaongelea nini na hasa hapa tulipo hivi sasa. Sana sana response ninayopata ni kama hizi;

  1. What? you must be joking!
  2. Come on now you arent serious, are you?
  3. What kind of Union is that?
  4. Two Presidents, One United Republic?
  5. Are you kidding me?
Kusema kweli watu wanaona kama vile hatunazo...two constitutions, two Heads of State, two Parliaments etc...in a United Republic? Hata Canada wanaye Waziri Mkuu moja, United States of America wanaye Raisi moja na hata iliyowahi kuwa USSR walikuwa na Raisi moja. Sisi hapa United Republic of Tanzania tunao Maraisi wawili, Manaibu Raisi watatu, Waziri Mkuu/Waziri Kiongozi wawili, Katiba mbili, Mahakama Kuu mbili, Amiri Jeshi Wakuu wawili...cha ajabu ni eti tuna chama tawala kimoja, CCM. Mtu mwenye akili ataelewaje mkanganyiko huu? Halafu unamkuta mtu na akili zake timamu kwenye hii karne ya 21 anadai tundelee tu na huu mkanganyiko; nadhani tunahitaji kupimwa akili.
 
Mkandara alichosema huyo mjumbe ni kweli na naweza kusema ana akili sana.

Ni kweli waziri wa kilimo wa JMT hawezi na hapaswi kwenda kufanya kazi znz.
Ili kuweza kufanya kazi Zanzibar, kwa mujibu wa katiba 2010 ni lazima mtu awe mkaazi na apewe kibali cha kufanya kazi.

Mtanganyika hana haki hiyo ni sawa na Mnigeria au Mfilipino awapo znz.
Kwanini waziri aende kuomba kibali cha ukaazi na kazi ili aweze kuhimiza kilimo?

Waziri huyo akiwa mzanzibar atakuwa na nusu haki. Ni mkaazi haihitaji kibali cha ukaazi. Lakini anahitaji kibali cha kufanya kazi za consulting kutoka Tanganyika.

Ni kwa mantiki hiyo huyo mjumbe anajua kutumia logic, ana akili na ana maono. Tume ya Warioba ikasema mambo yawe 7 mengine kila mmoja awe na lake.

Lakini pia jiulize huyu waziri wa JMT anasababu gani za kwenda kuhimiza kilimo znz? Kuhimiza si maneno ni pamoja na kutoa mchango, pembejeo, mbole na wataalam. Huyu hajulikani znz sasa anakwenda kutoa nini?
wamba atoe pembejeo au wataalam znz badala ya Mwanza kunako mhusu.

PM Pinda anahitaji kibali kufanya kazi znz seuse waziri wa Kilimo!

Wewe unamuona mjumbe ni mjinga kwasababu kuna mahali hujaelewa.
Nina uhakika hata yeye anakuona hivyo kwa kuzingatia sababu hizi.;

Kilimo si jambo la muungano. Hakuna sababu za kutafuta kibali kwenda kufanya kazi nchi jirani.

Wewe unadhani ni waziri wa JMT ambayo znz wapo, ukweli ni kuwa huyu ni waziri wa Tanganyika. Unaishi kwa hisia ndio maana huuoni ukweli huo.

Upo katika state of denial hata pale wznz wanapokutupia virago, wewe unabaki kusema ni nduguzo.

Kilimo si suala la muungano, hivyo waziri wa JMT ni popo hajulikani kama ni ndege au mnyama.

Vipi, unaonaje kama tutatengeneza utaratibu wa kujua huyu ni kwelea kwelea na yule ni Eagle.

Huwezi kuwa na utaratibu huo kama una serikali 2.
Lazima utakuwa na kwelea kwelea na popo, halafu Mkandara analalamika kwanini popo haailikwi mkutano wa ndege, kwa upande mwingine anasema kikao cha jana cha wanyama popo ni mtovu hakuhudhuria. Unamuonea popo, mtafutie kundi.
Kama unayoyasema ni kweli na nafsi yako inaamini hivyo ndio maana nikasema AJIZI nyumba ya UMASKINI!.

Mkuu wangu mnataka serikali 3, ilihali wewe unaamini kuwa waziri wa kilimo wa serikali ya Muungano hana mamlka ya kwenda Zanzibar kuzungumzia maswala ya kilimo bora, sasa huoni kama mnapotosha hata muundo wa hizo seriali 3 na kwamba haiwezi kuwa suluhisho la umaskini wetu (mahitaji muhimu) bali mnafanya maamuzi haya kwa sababu ya kuondokana na KERO ?

Nchi zote za shirikisho na hata muungano wa kisiasa, Waziri wa wizara yaJamhuri ana mamlaka taifa (nchi) nzima. Iwe Marekanii, Canada Uingereza na kadhalika. Sasa huu mfano wenu wa hizo serikali 3 mnazozitaka unaweza kunipa mfano wa nchi yoyote hata moja ilofanikiwa kuendelea na muungano kwa kutumia mfumo huu ambao waziri wa Kilimo wa Taifa hana mamlaka nje ya kule alikotoka?

Kama itakuwa hivyo, nini hasa lengo na sababu ya kuwepo serikali kuu maana kila nchi inajitoshelezaq na inaweza jitegemea pasipo serikali kuu na ndio maana Wazanzibar wanasema hata hilo Jeshi kubwa la Taifa hawalitaki maana hawana watu wengi kiasi cha kuwa na jeshi kubwa kama lililopo. Hawana maadui walowazunguka zaidi ya bahari..tutafika kweli?

Kwa maneno yako na mwenye kuelewa atapata jibu rahisi kabisa ya kwamba pendekezo lenu mnataka tugawane Umaskini. Hii ni sawa na familia wanaogombana kwa jambo dogo kabisa wamefikia kugawana mirathi kisha wanasema bado wanapendana na ni ndugu wa damu lakini undani wa mgawanyiko wowote wa mirathi mara zote huwa kuna mmoja wao anadhulumiwa hivyo kuanza kudai share yake halali. Matokeo yake nyumba huuzwa kama zilivyouzwa Kariakoo na wakagawana umaskini. Hakuna kati yao alotoka na wengi hata undugu umekufa hukutana tu kwenye misiba na mazishi ya wana familia.

Mimi nataka kuwauliza hivi hizi serikali 3 zitanikomboa nini mimi Mtanzania? ni sheria zipi zitakazo ongezeka kunipa fursa zaidi dhidi ya matatizo ufisadi, ajira, maradhi, elimu na adha kadhalika tulokuwa nazo leo. Ni katiba gani ya Tanganyika itakayo niwezesha mimi Mtanganyika kuwa na haki zaidi ya hii iliyopo? maana mnapendekeza serikali 3 lakini hamunionyeshi hityo katiba ya Tanganyika itakuwa na fursa zipi ili niunge mkono serikali ya tanganyika zaidi ya kuwepo jina la Tanganyika.i Yale yale ya Muislaam lazima uitwe Abdulrahman ukiitwa Joseph huwezi kuwa Muislaam ilihali imani ya dini sii ubatizo wa jina la Kiarabu. Joseph anaweza kuwa Muislaam safi kuliko huyo AbdulRahman.

Sasa kwa kutokuelewa kwenu kuhusu athari za serikali 3 maana hamna mfano wake, na kutoelewa ulazima wa kuwa na serikali kuu ya shirikisho mnalodai, ndio maana hata JK aliposema muundo huu - Jeshi litachukua ncjhi! mkaanza kudai ni upotoshaji, Lakini hamna majibu vile vile maana hamjui matokeo wala hamna mfano. Nakwambia tu ya kwamba kuna Ukweli mkubwa sana pale serikali kuu inapokuwa haina mamlaka juu ya nchi shiriki. Na ikiwa kilimo ni swala la mambo yasokuwa ya muungano, madini na mafuta ambavyo vyote huchangia asilimia kubwa ya pato la taifa hiyo serikali kuu itapata wapi fedha za kujiendesha? nani atakaye changia mfuko huo ikiwa waziri wa Kilimo Kitaifa hana mamlaka Zanzibar?

Na kuhusu waziri mkuu kutokuwa na mamlaka Zanzibar ndio kero, huyo wa serikali 3 atakuwa na mamlaka hayo? maana kinachokukera lazima kipewe suluhisho ktk muundo mnaopendekeza. Alikuwa hana mamlaka sasa apewe mamlaka ili usikereke na sio kuzuia kote. Nambieni kipi kitabadilika kama sii kussusiana halafu bado mnadai sisi ni ndugu na Muungano hautavunjika.
 
Mkuu Nguruvi3, huu Muungano wetu hauwezi kufananishwa na muungano wowote hapa duniani kwa sababu hau"make" sense kwa namna yoyote ile. Nimekutana na watu wengi kutoka sehemu mbali mbali wakitaka niwafafanulie huu muungano unavyofanya kazi. Nasikitika kusema kwamba sijampata mtu hata moja aliyeonesha hata kachembe cha uelewa ninaongelea nini na hasa hapa tulipo hivi sasa. Sana sana response ninayopata ni kama hizi;

  1. What? you must be joking!
  2. Come on now you arent serious, are you?
  3. What kind of Union is that?
  4. Two Presidents, One United Republic?
  5. Are you kidding me?
Kusema kweli watu wanaona kama vile hatunazo...two constitutions, two Heads of State, two Parliaments etc...in a United Republic? Hata Canada wanaye Waziri Mkuu moja, United States of America wanaye Raisi moja na hata iliyowahi kuwa USSR walikuwa na Raisi moja. Sisi hapa United Republic of Tanzania tunao Maraisi wawili, Manaibu Raisi watatu, Waziri Mkuu/Waziri Kiongozi wawili, Katiba mbili, Mahakama Kuu mbili, Amiri Jeshi Wakuu wawili...cha ajabu ni eti tuna chama tawala kimoja, CCM. Mtu mwenye akili ataelewaje mkanganyiko huu? Halafu unamkuta mtu na akili zake timamu kwenye hii karne ya 21 anadai tundelee tu na huu mkanganyiko; nadhani tunahitaji kupimwa akili.
Niulize mimi basi maana sijawahi kuulizwa. Yaweke maswali yako kwa namba halafu nitakujibu mtazamo wangu ambaio sii lazima uwe sawa na wanaopendekeza kuendelea na mfumo wa serikali 2.
 
Mkuu Mkandara
Niweke kauli sawa na naomba usipindishe.

Waziri wa kilimo wa JMT ya sasa hapaswi kufanya kazi znz kwasababu hana kiballi cha ukaazi wala kufanya kazi.

Unapokuwa na serikali 3 wiizara husika hazina mawaziri katika serikali shirikishi. Kwa maana kuwa waziri wa ulinzi ni mmoja tu na anakuwa na uwezo wa kufanya kazi kama waziri wa ulinzi wa JMT.
Waziri wa kilimo wa Tanganyika hapaswi kwenda znz au kinyume chake.

Ndivyo ilivyo huko Canada, kwamba kuna mbunge wa Jimbo, bunge la jimbo, serikali ya jimbo na mhakama za jimbo.
Hakuna waziri wa ulinzi wa jimbo isiokuwa yule wa federal goverment.

Kuna mambo ya federal na mengine ni ya province.
Kwa mfano sera ya afya ni federal matter, lakini namna gani kila jimbo linahudumia watu wake kwa sera ile ile ni suala la jimbo.

Kwa mfano, kuna wanaotoza familia kiasi fulani cha fedha kwa mwezi. Lipo jimbo linalotoza kupitia kodi za bidhaa kwamba kwa kila bidhaa kuna senti kadhaa za afya. Kuna majimbo ambayo hutoza kwa pay cheque.


Lakini, narudia tena sera za afya ni jukumu la federal government na waziri ni mmoja tu.

Kuna ulinzi wa ndani, wanakitu kinaitwa Royal Police, halafu kila jimbo lina Polisi wake na kila jiji ndani ya jimbo lina polisi wake. Kuna mambo yanahusu Police wa federal na mengine ya majimbo na majiji.

Hoja yangu kuhusu waziri a kilimo ilijikita kwa mazingira ya sasa na si ya serikali 3.
Tafadhali soma vema hoja kwasababu upotoshaji si jambo jema.

Kama unataka nikueleza kuhusu Marekani, Australia au India naweza pia, tena kuanzia katika federal level hadi ward. Nina ushahidi wa kujitosheleza na kile ninachozungumza.

Nitakueleza jinsi Scotland Yard na London Police wanavyofanya kazi.
Jinsi FBI, NYPD au LAPD na Sheriff wanavyofanya kazi kule Marekani
Nitakuleza jinsi RCMP, OPP na local police wanavyofanya kazi
Nitakueleza jinsi Melbourne, Brisbane, Perth n.k. zinavyofanya kazi kama washirika.

Mimi sidanganywi na JK kuwa uwepo wa federal government utasababisha jeshi liasi.
Namcheka sana JK kwa kudhani sote ni ndondocha.


 
Niulize mimi basi maana sijawahi kuulizwa. Yaweke maswali yako kwa namba halafu nitakujibu mtazamo wangu ambaio sii lazima uwe sawa na wanaopendekeza kuendelea na mfumo wa serikali 2.
Bahati mbaya sina cha kukuuliza maanake nimesoma maelezo yako mareefu, sijaelewa unazungumzia nini...hebu come out and say it, sema uko upande gani tuzungumze. Na hata hapo juu nilikuwa narespond tu kwa post ya Nguruvi3 kwa sababu sijaona cha kurespond katika maelezo yako. Maybe I am thick lakini nakiri nimeshindwa kuelewa unatetea nini na unapinga nini zaidi ya story and for that am sorry, I aint that good at story telling...to me a spade is a spade! Hivi sasa tunatakiwa tuitumie hii fursa adimu kujenga msingi imara kwa taifa tunalolitaka na ni msingi huo imara utakaotoa dira namna tutakavyoweza kujikwamua na changamoto ambazo zimedumaza maendeleo yetu kama taifa kwa miaka zaidi ya 50.
 
Mkuu Mkandara
Niweke kauli sawa na naomba usipindishe.

Waziri wa kilimo wa JMT ya sasa hapaswi kufanya kazi znz kwasababu hana kiballi cha ukaazi wala kufanya kazi.

Unapokuwa na serikali 3 wiizara husika hazina mawaziri katika serikali shirikishi. Kwa maana kuwa waziri wa ulinzi ni mmoja tu na anakuwa na uwezo wa kufanya kazi kama waziri wa ulinzi wa JMT.
Waziri wa kilimo wa Tanganyika hapaswi kwenda znz au kinyume chake.

Ndivyo ilivyo huko Canada, kwamba kuna mbunge wa Jimbo, bunge la jimbo, serikali ya jimbo na mhakama za jimbo.
Hakuna waziri wa ulinzi wa jimbo isiokuwa yule wa federal goverment.

Kuna mambo ya federal na mengine ni ya province.
Kwa mfano sera ya afya ni federal matter, lakini namna gani kila jimbo linahudumia watu wake kwa sera ile ile ni suala la jimbo.

Kwa mfano, kuna wanaotoza familia kiasi fulani cha fedha kwa mwezi. Lipo jimbo linalotoza kupitia kodi za bidhaa kwamba kwa kila bidhaa kuna senti kadhaa za afya. Kuna majimbo ambayo hutoza kwa pay cheque.


Lakini, narudia tena sera za afya ni jukumu la federal government na waziri ni mmoja tu.

Kuna ulinzi wa ndani, wanakitu kinaitwa Royal Police, halafu kila jimbo lina Polisi wake na kila jiji ndani ya jimbo lina polisi wake. Kuna mambo yanahusu Police wa federal na mengine ya majimbo na majiji.

Hoja yangu kuhusu waziri a kilimo ilijikita kwa mazingira ya sasa na si ya serikali 3.
Tafadhali soma vema hoja kwasababu upotoshaji si jambo jema.

Kama unataka nikueleza kuhusu Marekani, Australia au India naweza pia, tena kuanzia katika federal level hadi ward. Nina ushahidi wa kujitosheleza na kile ninachozungumza.

Nitakueleza jinsi Scotland Yard na London Police wanavyofanya kazi.
Jinsi FBI, NYPD au LAPD na Sheriff wanavyofanya kazi kule Marekani
Nitakuleza jinsi RCMP, OPP na local police wanavyofanya kazi
Nitakueleza jinsi Melbourne, Brisbane, Perth n.k. zinavyofanya kazi kama washirika.

Mimi sidanganywi na JK kuwa uwepo wa federal government utasababisha jeshi liasi.
Namcheka sana JK kwa kudhani sote ni ndondocha.


Hakika mkuu wangu kwa majibu yako unaendelea kuonyesha jinsi msivyofahamu muundo wa serikali 3 hasa hapo ulipotumia serikali ya Canada. Waziri wa kilimo nchini humo ni Jerry Ritz huyu ni waziri wa serikali kuu na ana mamlaka Canada nzima bila kujali anatoka jimbo gani. Huyu ni waziri ktk serikali ya Waziri mkuu ambaye ni sawa na rais wa Tanzania.

Ila basi kila jimbo lina serikali yake na waziri wa kilimo wa jimbo hana mamlaka ktk jimbo jingine maana mamlaka alokuwa nayo ni ya ki reppublic yaani eneo la mipaka ya nchi alogombea, lakini waziri yeyote wa serikali kuu ya Harper au Obama ana mamlaka Canada/USA nzima inapokuwa maswala ya kimataifa yanayohusiana na kilimo.

Kwa maana ya kwamba ikiwa serikali ya Canada wanataka kufanya mkataba na China say kuuza mbao zao, ni waziri huyu wa Kilimo anahusika zaidi ya waziri wa Ontario ama British Columbia maana mikataba ya aina hii hupitia jina la Taifa kufuatia uwezo wa Taifa kudai ama kulipa deni. Canada ndiyo yenye credit score na sio Ontario ama British Columbia kimataifa. Unakumbuka Harper alipokuja na mawaziri wake Tz tulizungumzia maswala ya Barricks wakati shirika hilo lipo jimbo la Ontario na hatoki Ontario.

Pamoja na hivo kila ya transactionpato lolote la nchi mojawapo ktk kilimo, serikali kuu ya Harper kuchukua direct asilimia 8 acha mbali ushuru wa forodha na kadhalika hivyo serikali kuu ina vyanzo vingi vya ndani na nje ktk kukusanya fedha za mfuko wake wa maendeleo kwa Canada nzima. Na zipo project kubwa ambazo Jimbo moja haliwezi kuzimudu, serikali kuu huchukua nafasi ya kuwwezesha majimbo hayo ktk miradi mikubwa. Mimi naishi Canada kwa miaka 28 mkuu wangu najua mengi ya utawla wa nchi hiyo kuliko msomi yeyote wa Tanzania ambaye hana exposure. Kutembea dunia ni elimu ya chuo kikuu mkuu wangu maana wanasema uko kama mwanajeshi uko uwanja wa vita.

Kwenda kusoma Uingereza ama Canada huwezi kuyajua mengi ya Ubepari na athari zake, unahitaji kuishi nao, ufanye kazi nao na uwasikilize mazungumzo na mawazo yao na kuyaona wanayofanya ukiwa sehemu ya nguvu ya kazi. Ni watu kama sisi tunaoweza kuwapa picha halisi ya muundowa serikali 3. Na ndio nikasema toka nawasikiliza wajume wote wa upande wa kushoto na kulia wote wameonyesha hawajui kazi walopewa zaidi ya kupiagana vishoka. Zitto peke yake kanionyesha anajua muundo wa serikali 3 unatakiwa kuwa vipi na sii kama trasimu ama wajume wa baraza hilo wanavyopendekeza iwe wa CUF au Chadema.

Kikubwa zaidi mnachokosea ama niseme wajumbe wanachokosea ni pale wanapodai changu changu na chako chako! ndio nasema hakuna kitu kama hcho! ila ni kugawana umaskini. Hivyo sii kwamba napinga muundo wa serikali 3 laa ila mapendekezo ya muundo wake ni mbovu sana na kwa mwenye kuelewa atagundua kuwa mnajaribu kuondosha KERO badala ya kuchanganua sabau zilizosababuisha kero hizo.

Watanganyika mnachokifanya ni reaction tu baada ya Zanzibar kutangaza kuwa nchi na wakatunga katiba yao lakini tunasahau kwamba kwa miaka 30 ilopita Tanganyika tumechukua mambo mengi sana na kuyafanya ya Kitaifa bila ridhaa yao ama kinyume cha makubaliano ya awali. Kwa mfano rais akitoka bara basi makamu wake lazima atoke Zanzibar na pia alikuwa rais wa Zanzibar.

Pili, ikiwa nchi zote duniani mfuko wa Taifa ni mfuko wa nchi zote husika inakuwaje sisi mfuko huo unatenganisha fedha za Zanzibar na za Tanganyika ilihali zimekusanywa ktk account moja na Tanganyika? Tofauti na mataifa mengine tukiomba mkopo kwa kitamaifa kujenga barabara ni swala la Jamhuri lakini fedha jhizo zinaijenga Bara. Kuvaa kloti la Muungano)..kinyume chake mnapendekleza Tanganyika ijitenge wakati mnajua fioka Tanganyika haiwezi kupewa mikopo ya nje kama nchi ya shirikisho la Muungano. isiyokuwa na kiti UN wala Credit score kama nchi.

Nisome kwa makini, kiwa jimbo la Ontaria, Canada yenye mfuiko na reserves kubwa mara 100 ya Tanganyika hawawezi kuingia mikataba mikubwa ya kimataifa pasipo kupitia serikali kuu ya Harper ni kipi kinachowapeni tumaini nyie kuwa Tanganyika itaweza kusimama wakati haina credit score kama Taifa?.

Nitarudia kusema hivi, ktk nchi za magharibi hakuna wizara zisizokuwa na muungano - HAKUNA isipokuwa kwa maana hii. Ya kwamba kila nchi inakuwa na mamlaka ya kirepublic kuendesha shughuli zake za maendeleo, ukusanyaji kodi na ushuru tena wao hata jeshi la Polisi kila nchi ina lake na mamlaka kamili ya kuunda jeshi hilo kuna Jeshi la Polisi la Kitaifa ambalo linaingia mahala popote ktk Jamhuri husika. hapa Canada wanaitwa RCMP. hawa hawana cha bara wala zisiwani sasa nyie mnataka serikali 3 kisha mnagawana umaskini. Kila mtu na chake mnafikiri sisi wajinga kiasi gani haswaa!!

Hivyo basi ili mtu kama mimi nikubaliane na kundi lenu ni lazima muwe na ufafamuzi mzuiri wa serikali 3 na sii madai ya kuondokana na KERO. Serikali 3 huwa na serikali za nchi zenye mamlaka ktk majimbo yao kuendesha shughuli zote za maendeleo lakini haina maana kila nchi inabeba mzigo wake.

Wizara zote zipo chini ya serikali kuu isipokuwa kuna nchi zinaweza kutokuwa na zwizara fulani ktk mamlaka yake maana sii rahisi Dodoma ikawa na wizara ya Uvuvi. Pamoja na hayo nchi hizi ktk muungano wao hugawana kazi tu badala ya kuwa kila kitu kiko centraled ktk serikali kuu. Kwa kugawan hivyo hurahisisha kazi za uendeshaji kama vile wewe uwe na watoto wawili mmoja analima shamba na mwingine ni mfugaji, mkeo akipika na kuwalea walokuwa wadogo wewe ofisini machimbo ya TRA..

Kila mmoja wanu amejikitita katika kuendesha biashara hizo pasipo kuingiliana ila wote hawa wako chini yako na wakitumia jina lako na mashamba yako.Tanznaia ni kielelezo tu cha mipaka na maeneo yalokuwa chini ya dola husika lakini vitu vyote vinafanywa na majimbo. Ni ujinga mkubwa sana kuwagawanisha watoto ukawapa urithi kabla hujafa kisha ukadai wewe hutakufa njaa wakati huna vyanzo! Mapendekezo ya serikali 3 ni uhuni mtupu kama mnashindwa kujenga hoja ila kutaka kuandika historia upya ya Tanzania ka kupitia wanasheria udwanzi kama TL na Jussa.

Na pia mapendekezo ya serikali 2 ni kukataa ukweli kwamba Tanganyika imelivaa koti la Muungano maanake nao hawana hoja ya kutuonyesha kwamba wanajua wanayoyafanya ni kinyume na wako tayari kurekebisha. Wameshindwa kwa miaka 30 leo hii sii rahisi mimi nikubali kwamba CCM wako tayari kurekebisa mahitaji ya Wazanzibarkwa manufaa ya Muungano.
 
Mkuu wangu
Serikali 3 za Tanzania si za Canada kwasababu znz tayari ni nchi. Ontario ni jimbo. Hili lieleweke.
Wewe mwenyewe unasema kuna mambo yameingizwa kinyemela, Canada hakuna anayesema hivyo kwasababu wote wanaamini katika shirikisho.

Unapokuwa na znz kama nchi, halafu ukawa na Tanzania ambayo znz ipo bila kuwa na mshirika, huwezi kuweka hali hiyo katika mizani na Canada. Hivyo kuna tofauti ndio maana tume ikasema ili kuondoa mambo ya kinyemela basi yasiyo ya muungano ambayo JK kasema pia yaondolewe. Swali ambalo hujibu ni moja, yapelekwe wapi?

Waziri wa Kilimo wa Canada anashughulikia mambo ya sera za taifa hasa katika kiwango cha kimataifa. \
Waziri wa kilimo wa jimbo anashughulikia sera za jimbo kuhusu kilimo. Hapa kwetu hilo haliwezekani kwasababu znz wanasema hawataki kuwa na sera moja na utekelezaji katika level ya 'majimbo'.

Wao wanataka waziri wao wa kilimo Hivyo lazima uangalie mazingira yaliyopo. Znz hawataki kuwa jimbo kama Ontario au BC sasa unawezaje kuwa na model kama ya Canada?

Kuhusu credit score, tume imesema suala hilo liwe la serikali kuu. Znz wanasema wanataka wawe wenyewe, kama ambavyo Ontario ingeomba kuwa yenyewe. Hivi mkuu hapo huoni unalinganisha chungwa na Nanasi?

Lakini kwa taarifa yako Tanganyika ina credit score. Tanganyika ina assets na inaweza kupata mkopo yenyewe.
Hata sasa hivi tunapata hiyo mikopo kwa credit za Tanganyika siyo znz.
Uwezekano wa Tanganyika kukopesheka ni mkubwa mara 100 kuliko znz.

Suala la kugawana umasikini. Sisi sote ni masikini na hakuna hoja ya kugawana umasikini.
Tutagawana umasikini gani na znz Mkandara?

Znz ni sawa na Ilemela mwanza, tugawane nini. Unachotaka ni kunyanyua hadhi ya Znz wakati namba hazikubali.
Labda useme hivi 'tunachotaka ni kuwasaidia wznz kwa umasikini' hatugawani kwasababu miaka 20 hawana lolote walilosaidia Tanganyika, tugawane hewa. Miaka 20 wanatia pilipili katika umasikini wetu kwa kuomba, kudai hata wasicho na haki nacho. Ni sawa na kupe ambaye licha ya fadhila za kubebwa na ngombe bado anatia mwiba anyonye damu hata kumuua ng'ombe. Hizo serikali 2 ni kuendeleza ukupe, kwamba tubebe zigo katika kauli mbiu ya kuchangia umasikini.

Kuhusu kuingizwa mambo Kinyemeal JK kaonyesha jinsi mambo hayo yalivyoingizwa.
Sijui kama unakubalina au hukubaliani naye. Karume kasaini kwa niaba ya znz unyemela upo wapi hapo mkuu?
Mbona unazusha mambo, la sivyo kataa alichosema JK kama si kweli.

Kuhusu RCMP, huko Canada wana mandate ya federal lakini hawaingii kila mahali hovyo. Kuna mambo yanayohusu RCMP yapo ya majimbo na yapo ya majiji.
 
Naomba nichangie nikidokoa dokoa ili kukidhi haja ya mjadala.
Mkuu Mkandara, Quebec siyo nchi ni jimbo nchini Canada.
Lina waziri wa jimbo(Premier) lakini si waziri mkuu Prime minister. Kuna sheria zinazotambulika kila jimbo, hata leseni zinatofautiana kwa viwango na usajili wake.

Znz ni nchi ina wimbo wake, bendera, Bunge na kila kitu kwa mujibu wa katiba ya 2010.
Quebec hawana mamlaka ya kuhoji uhalali wa katiba ya Canada au hawana uhalali wa kuondoa jambo au kuongeza bila federal government kujua. Zanzibar wanaweza kuzuaia hoja za JMT

Kuhusu Uchangiaji, Quebec kama jimbo wanachangia federal government kama majimbo mengine.Znz kama nchi haichangii chochote katika muungano.

Kama unafuatilia habari Quebec waliataka kujitenga wakati wa Pierr Trudeau.
Referendum ikapendelea kuwepo kwa shirikisho.

Nao kama znz kelele haziishi ingawa ni jimbo masikini. Wanapata ruzuku kutoka majimbo mengine kama Zanzibar na mchango wao ni almost nil kama Zanzibar.

Tofauti na Zanzibar Quebec wanachangia kile walicho nacho kidogo kama ishara ya kuwajibika, Zanzibar ikiwa ni nchi zaidi ya jimbo la Quebec inachukua hata isichostahili wala haijishughulishi kujua gharama za muungano zaidi ya kudai mapesa na vyeo kila uchao

Uchaguzi wa premier wa Quebec majuzi ulileta kizaazaa, kama ulifuatilia habari za media.
Hoja ya kujitenga ikajirudia tena.

Majimbo mengine ya Canada yakasema sasa inatosha, Quebec ni wategemezi lakini hawaishi gubu kama Zaznibar. Kama wanataka kuondoka to hell waende zao.
Majimbo yamechoka kama ilivyochoka Tanganyika.

Hivyo kuna similarity za Quebec na Znz kitabia, gubu, kuchukua na kutokutoa.
Kuna tofauti kati ya Quebec na Znz kwasababu moja ni jimbo na nyingine ni nchi.
Mfano wako haujakidhi na haujitoshelezi.


Nguruvi3:

Hili suala la kuhoji katiba ni lazima uliangalie kimakini. Unapokuwa kwenye muungano na bunge la muungano kupitisha sheria au mabadiliko ya katiba, mabunge ya entities zilizopo kwenye muungano yanaweza kuhoji au kufanya ratification ya mabadiliko hayo.

Wewe unayeomba serikali tatu ni lazima uwe na vyombo vya kuhakiki kuwa serikali ya muungano haivuki mipaka yake.
 
Nguruvi3:

Hili suala la kuhoji katiba ni lazima uliangalie kimakini. Unapokuwa kwenye muungano na bunge la muungano kupitisha sheria au mabadiliko ya katiba, mabunge ya entities zilizopo kwenye muungano yanaweza kuhoji au kufanya ratification ya mabadiliko hayo.

Wewe unayeomba serikali tatu ni lazima uwe na vyombo vya kuhakiki kuwa serikali ya muungano haivuki mipaka yake.
Nitajie mambo ambayo serikali ya muungano imevuka mpaka.
Kuhoji katiba si tatizo, shida ni pale hatua za kuidhalilisha katiba ya muungano zinapofanyika.

Sikuona sababu za znz kuondoa jambo kama reli na bandari ambayo yapo katika muungano kisheria na kwa sheria ya bunge. Wanaweza kufanya hivyo ikiwa tu wanapitia mkondo uliounda sheria hiyo yaani bungeni.
Sheria za bunge hufutwa na bunge, sasa znz inapofuta yenyewe ni uhuni

Leo katiba ya JMT inamtambua waziri kiongozi, katiba ya znz inatambua makamu wa rais.
Hivi huoni kuna ubabe wa utoto hapo?

Znz inapotunga katiba iliyo juu ya katiba ya muungano, kuna muungano hapo!
Kumbuka ni znz hiyo hiyo inadai heshima na usawa, upande mwingine haina heshima wala usawa.
 
Nitajie mambo ambayo serikali ya muungano imevuka mpaka.
Kuhoji katiba si tatizo, shida ni pale hatua za kuidhalilisha katiba ya muungano zinapofanyika.

Sikuona sababu za znz kuondoa jambo kama reli na bandari ambayo yapo katika muungano kisheria na kwa sheria ya bunge. Wanaweza kufanya hivyo ikiwa tu wanapitia mkondo uliounda sheria hiyo yaani bungeni.
Sheria za bunge hufutwa na bunge, sasa znz inapofuta yenyewe ni uhuni

Leo katiba ya JMT inamtambua waziri kiongozi, katiba ya znz inatambua makamu wa rais.
Hivi huoni kuna ubabe wa utoto hapo?

Znz inapotunga katiba iliyo juu ya katiba ya muungano, kuna muungano hapo!
Kumbuka ni znz hiyo hiyo inadai heshima na usawa, upande mwingine haina heshima wala usawa.

Nguruvi3

Hivi reli zenyewe zipo wapi? Itafika wakati watajitoa kwenye shirika la posta na utawaona wanadhalilisha wakati biashara ya posta is outdated.
 
Mkuu wangu
Serikali 3 za Tanzania si za Canada kwasababu znz tayari ni nchi. Ontario ni jimbo. Hili lieleweke.
Wewe mwenyewe unasema kuna mambo yameingizwa kinyemela, Canada hakuna anayesema hivyo kwasababu wote wanaamini katika shirikisho.

Unapokuwa na znz kama nchi, halafu ukawa na Tanzania ambayo znz ipo bila kuwa na mshirika, huwezi kuweka hali hiyo katika mizani na Canada. Hivyo kuna tofauti ndio maana tume ikasema ili kuondoa mambo ya kinyemela basi yasiyo ya muungano ambayo JK kasema pia yaondolewe. Swali ambalo hujibu ni moja, yapelekwe wapi?

Waziri wa Kilimo wa Canada anashughulikia mambo ya sera za taifa hasa katika kiwango cha kimataifa. \
Waziri wa kilimo wa jimbo anashughulikia sera za jimbo kuhusu kilimo. Hapa kwetu hilo haliwezekani kwasababu znz wanasema hawataki kuwa na sera moja na utekelezaji katika level ya 'majimbo'.

Wao wanataka waziri wao wa kilimo Hivyo lazima uangalie mazingira yaliyopo. Znz hawataki kuwa jimbo kama Ontario au BC sasa unawezaje kuwa na model kama ya Canada?

Kuhusu credit score, tume imesema suala hilo liwe la serikali kuu. Znz wanasema wanataka wawe wenyewe, kama ambavyo Ontario ingeomba kuwa yenyewe. Hivi mkuu hapo huoni unalinganisha chungwa na Nanasi?

Lakini kwa taarifa yako Tanganyika ina credit score. Tanganyika ina assets na inaweza kupata mkopo yenyewe.
Hata sasa hivi tunapata hiyo mikopo kwa credit za Tanganyika siyo znz.
Uwezekano wa Tanganyika kukopesheka ni mkubwa mara 100 kuliko znz.

Suala la kugawana umasikini. Sisi sote ni masikini na hakuna hoja ya kugawana umasikini.
Tutagawana umasikini gani na znz Mkandara?

Znz ni sawa na Ilemela mwanza, tugawane nini. Unachotaka ni kunyanyua hadhi ya Znz wakati namba hazikubali.
Labda useme hivi 'tunachotaka ni kuwasaidia wznz kwa umasikini' hatugawani kwasababu miaka 20 hawana lolote walilosaidia Tanganyika, tugawane hewa. Miaka 20 wanatia pilipili katika umasikini wetu kwa kuomba, kudai hata wasicho na haki nacho. Ni sawa na kupe ambaye licha ya fadhila za kubebwa na ngombe bado anatia mwiba anyonye damu hata kumuua ng'ombe. Hizo serikali 2 ni kuendeleza ukupe, kwamba tubebe zigo katika kauli mbiu ya kuchangia umasikini.

Kuhusu kuingizwa mambo Kinyemeal JK kaonyesha jinsi mambo hayo yalivyoingizwa.
Sijui kama unakubalina au hukubaliani naye. Karume kasaini kwa niaba ya znz unyemela upo wapi hapo mkuu?
Mbona unazusha mambo, la sivyo kataa alichosema JK kama si kweli.

Kuhusu RCMP, huko Canada wana mandate ya federal lakini hawaingii kila mahali hovyo. Kuna mambo yanayohusu RCMP yapo ya majimbo na yapo ya majiji.
Nguruvi3, mkuu wangu kama hujui kitu uliza kwanza kabla hujaandika madudu. Ontario ni nchi sio jimbo kama Kilimanjaro au Arusha. Hata rais wake ambaye anaitwa Waziri mkuu haina maana ana mamlaka kama Pinda wetu. Huyu ana mamlaka kamili kama rais wa Marekani, JK au rais mwingine yeyote. Labda nikwambie tu ya kwamba Harper ana mamalka sawa ni Waziri mkuu wa Uingereza ama Obama kwa Marekani.

Hivyo matumizi ya maneno kama Province isikufanye ufikri Kitanzania ya kwamba maadam Arusha ni Province basi hata Ontario ni Province kama Arusha. Ontario ina bendera yake, serikali yake, mahakama zake na bunge lake na pia wana wajumbe ktk serikali kuu ktk nafasi hizo hizo. Marekani vile vile ndio kusema State ni sawa na Province ya Canada lakini sio sawa na Province ya Tanzania.

Hii kutoelewa muundo wa serikali mnaypopendekeza ndio inawasukuma kufanya makosa makubwa ktk rasimu ya Wariobba. Ningewaomba tu nyote mnaopendekeza serikali 3 mjifunze kutokana na muundo wa serikali ya Marekani au Canada mnazozitumia ktk mifano yetu kwa sababu hakuna state yoyote yenye mamlaka ya kuwa na wizara ambazo hazipo ktk muungano.

Wizara zote ni za Muungano isipokuwa sheria na Policy za uendeshaji wa shughuli hizo ndio upo ktk mikono ya nchi ama majimbo hayo kwa sababu ikiwa Chadema wameshinda uchaguzi Kilimanjaro, Chadema ndio wanakuwa na mamlaka kamili ya kuendesha shughuli zote za maendeleo ya Kilimanjaro japo rais anaweza kutoka CCM au CUF. Haya ndio mamalka kamili na sii kugawana umaskini. Hakuna hii kitu ya shughuli zisizokuwa za muungano kuwa milki ya nchi hiyo serikali kuu haina mkono ndani, nakuomba ufahamu hilo kwanza kuwa serikali kuu inaingia kila mahala na kila transaction ya mauzo wanakata kisu chao kwa kila state, province au nchi shiriki.Na kama ingekuwa mnavyopendekeza I swear Obama asingeweza kuitawala Marekani hata kwa usiku mmoja.

Mnaogopa Znz kuwa na bunge lake, katiba yake halafu nyie nyie mnataka serikali 3 ambazo kila nchi huwa na na vitu vyote hivyo. Na ndio maana mnachekesha kutoa sababu za bendera na kadhalika hali muungano wetu ni wa nchi ambazo zilikuwa huru. Tena basi kila mwaka tunasherehe kubwa za Uhuru wa Tanganyika.. Tofauti baina ya serikali 2 na 3 ni kutengenisha tu majina lakini mtajikuta mnarudia yale yale maana hakuna kati yenu anajua muundo wa serikali 3 unatanguliwa na vitu vipi kwanza isipokuwa jina la Tanganyika lirudishwe.
 
Hapana Quebec ilikuwa ni nchi kama ilivyokuwa Ontario, New Bruzwinsk, zikajiunga Alberta, Nova Socatia na kutengeneza ferderation. Tofauti ni kuwa Quebec ilikuwa na Mfaransa zingine zikiwa ni Dominion chini ya Malikia.

Kwasasa kila jimbo lina kila kitu chake lenyewe. Premier wa Quebec hana uwakilishi UN na wala katika mambo mazitio kama ulinzi hana jeshi. Znz Rais wake ana jeshi, na katiba yake inayomtambua kwa ukuu mbele ya JMT.

Quebec hawana nafasi ya kuchezea katiba ya Canada, Zazibar wakiamua watu 50 wanaoitwa baraza la wawakilishi wanakaa na kunywa chai wakifikira nini wachomoe nini waongeze katika katiba ya JMT
nguruvi, baada ya kukusoma nimegundua ya kwamba hata wewe umeingia ktk mkenge wa Pinda ya kwamba Zanzibar sio nchi kwa maana ya Muungano kama zilivyo Quebec na Ontario bila kufahamu kwanza maana na matumizi ya neno hili NCHI. Quebec ilikua nchi na bado hadi leo ni nchi kama zilivyo province nyinginezo zote za Canada. Na nchi za Marekani zilikuwa nchi na bado ni nchi hadi leo ktk muungano wa nchi hizo kuunda TAIFA moja la Marekani na ndio maana inaitwa United STATES of America.

Maajabu ni kwamba unakubali nchi 12 au 50 za Marekani ziliungana kuunda federation na nchi zote hizo zilikuwa na bendera zao, serikali za0, mabunge yao na mahakama, hata kabla hawajaungana ila hufahamu ya kwamba ncjhi hizo bado zina mamlaka yaleyale na vyombo hivyo hadi leo ktk muungano wa nchi hizo. hakikubadilika kitu zaidi ya kuongezeka Uwakilishi ktk serikali Kuu ambayo mimi naiita ya TAIFA.

Quebec haiwezi kuwa na kiti UN kwa sababu ni NCHI sio TAIFA lakini wana mamlaka kamili ya kuendesha shughuli za serikali wao wenyewe na ndio maana chama cha PQ kikishinda uchaguzi ndicho husimamia shughuli zote za serikali pasipo kuingiliwa na chama tawala cha Kitaifa. Na kila province au States ya Marekani shughuli zote za serikali huwa ni mamlaka kamili ya nchi hiyo hivyo wakichagua chama fulani ndicho chenye mamlaka ya kuendesha shughuli za serikali haina maana kwamba wanagawana umaskini bali wanagawana kazi kutokana na uchaguzi wa wananchi.

Lakini nikija kwetu sisi utagundua hatutazami swala hili la Muungano kwa kuwawezesha wananchi kuchagua chama na sera zake ili chama hicho kiwe na mamlaka kamili ya kuendesha shughuli za serikali. Na Wazanzibar kwa kutosoma ama kuelewa wanalalamika pasipo kujua ya kwamba maadam chama kinachoongoza ni CCM wataendelea kuwa na mfumo, sera na ilani za CCM hata kama tukijenga serikali 3 ila tu inawezekana kama CUFau Chadema itashinda na sio ktk mfumo uliopo iwe kwa serikali 2 au 3. Kinachotakiwa ni kifungu cha ACT kinachotoka mamlaka kamili kwa uendeshaji wa shughuli za nchi kwa maana na malengo haya. Wadhungu wanasema - States and Provinces are jurisdictions that receive their power and authority directly from the Constitution act., Hii ndio tunaihitaji ktk KATIBA MPYA na sii kwa Zanzibar tu bali Tanzania yote na ktk amjimbo yote.

Ndio kusema hata huku Bara tunahitaji mamlaka kamili ya majimbo yetu ili kesho kama Chadema watachukua Mikoa ya Mwanza, Mara, Arusha,Kigoma na Kilimanjaro basi wao ndio wawe viongozi wa shughuli zote za serikali ya majimbo hayo. na sii kila chama kurudi kwa CCM kutenga bakuli kwa sababu bado tunaendelea na mfumo wa central Government ku control shughuli, mapato, na utekelezaji wa sera za kiuchumi kwa TAIFA zima. Hi ina maana bado sisi tunaendelea na siasa za Ujamaa chini ya mwavuli wa hili neno demokrasia.

Hivyo basi kinachotakiwa kubadilishwa sio serikali 2 au 3 au 1 maana pande zote zinakosa mamlaka kamili zaidi ya CCM kuendelea ku control shughuli zote za serikali iwe kwa nchi, majimbo na TAIFA japo vyama vingine vinashinda uchaguzi ktk majimbo kadhaa. Hata Halmashauri ya jiji hawana mamlaka kamili kama Hamashauri, kuna shughuli za Halmashauri hadi leo zimeshikiliwa na serikali kuu sasa unategemea vipi Halmashauri hizo zinaweza kujiendesha.

Pili, Ubinafsishaji umevuka mipaka kiasi kwamba Hata usafi wa mji unashikiliwa na watu binafsi wakati nchi za wenzetu mamlaka ya usafi wa mji yako chini ya City. Hivyo ndani ya nchi kuna ugawanaji wa shugjhuli za maendeleo serikali ikibakia tu kupanga sera na ilani ili kutimiza ahadi walizotoa kwa wananchi wakati huo huo wakikusanya kodi na ushuru. Sisi tumebinafsisha toka Usafiri, usalama (fire) hadi usafi na majitaka badala ya City kuwajibika na shughuli hizo moja kwa moja toka mipango hadi mapato ili wajiendeshe!

Kina sisi toka serikali kuu hadi serikali za mitaa - Cheo sii dhamana ila ni Unyapala. Kila kiongozi amekabidhi mjeredi na wananchi lazima tuwasujudie ili kupata - maadam huduma! maana huduma zenyewe hazina nafuu japo ni haki yetu. Jeshi a Polisi linaitwa Police FORCE wakati wenzetu hujiita Police services - To serve and Protect. Hii ndio Ajizi nyumba ya Umaskini.
Usipoona athari hizi za mfumo uliopo ukarukia serikali 3 utakuwa unapotosha wengine ambao hawafahamu KERO zetu haswa zimetokana na nini!
 
Back
Top Bottom