Ajizi nyumba ya umaskini na siio njaa!

Ajizi nyumba ya umaskini na siio njaa!

Mkuu Mkandara , nilikaa kimya kwasababu bandiko #19 ulikuja kwa hamaki kidogo.

Nikueleza jambo moja, hiyo Canada miye naifahamu vema hasa kuanzia kwa Pierr Trudeau babaye yake Justin ambaye alikuwa rafiki wa Nyerere. Trudeau ndiye alimpa Nyerere zile engine kubwa za treni kutoka Bombardier.
Katika watu waliokuwa karibu na suala hilo ni mheshimiwa Samwel Sitta.

Vugu vugu la Quebec na referendum ya Trudeau nimeyaona enzi hizo, watu wakivuka hapo Gateneu ili nchi kijitenga warudi upande wa Canada a.k.a Kanata. Hao akina Maroi wa PQ ni wa leo tena wiki iliyopita Liberal wamehukua Quebec kwasababu ya siasa za PQ.

Akina marehemu Chief Lukumbuzya ni sehemu ya mabalozi wetu. Kuanzia enzi hizo kuja kwa Mulroney, Jean Chretiene, Paul Martin nimekuwa na mwanga mzuri kwasababu mengine nimeyaona yakifanyika.
Hapo Ontario mbona padogo tu! tuongee ya Nunavut na Yellow knife au North territory ya Hudson bay.

Ugomvi wa North and south Carolina nimeona makovu yake ndipo nilipokwenda kudurusu kuhusu Antebellum


Siandiki madudu, mengi nimeyaona.

Hebu nikuulize kidogo, kwani Canada imeanzaje hadi kufikia hapo?
I mean confederation to federation.
Nauliza hivyo ili tujue tofauti ya znz na Ontario, mfumo wa Warioba na Canada.
 
Mkuu Mkandara , nilikaa kimya kwasababu bandiko #19 ulikuja kwa hamaki kidogo.

Nikueleza jambo moja, hiyo Canada miye naifahamu vema hasa kuanzia kwa Pierr Trudeau babaye yake Justin ambaye alikuwa rafiki wa Nyerere. Trudeau ndiye alimpa Nyerere zile engine kubwa za treni kutoka Bombardier.
Katika watu waliokuwa karibu na suala hilo ni mheshimiwa Samwel Sitta.

Vugu vugu la Quebec na referendum ya Trudeau nimeyaona enzi hizo, watu wakivuka hapo Gateneu ili nchi kijitenga warudi upande wa Canada a.k.a Kanata. Hao akina Maroi wa PQ ni wa leo tena wiki iliyopita Liberal wamehukua Quebec kwasababu ya siasa za PQ.

Akina marehemu Chief Lukumbuzya ni sehemu ya mabalozi wetu. Kuanzia enzi hizo kuja kwa Mulroney, Jean Chretiene, Paul Martin nimekuwa na mwanga mzuri kwasababu mengine nimeyaona yakifanyika.
Hapo Ontario mbona padogo tu! tuongee ya Nunavut na Yellow knife au North territory ya Hudson bay.

Ugomvi wa North and south Carolina nimeona makovu yake ndipo nilipokwenda kudurusu kuhusu Antebellum


Siandiki madudu, mengi nimeyaona.

Hebu nikuulize kidogo, kwani Canada imeanzaje hadi kufikia hapo?
I mean confederation to federation.
Nauliza hivyo ili tujue tofauti ya znz na Ontario, mfumo wa Warioba na Canada.
Mkuu wangu hata siku moja siandiki kwa hamaki ila pengine lugha nayotumia ndio imekuwa kali kidogo.
Swala la mungano wa Canada unaweza ku google ukaipata sintopenda kuandika vitu wakati vinapatikana ktk website hata mbumbumbu anaweza kuvipoata.

Hapa tunafahamishana jinsi wenzetu wanavyoziongoza nchi zao na sii kubishana. Uwe unaifahamu historia ya Canada ama umeisoma hili sii tatizo ila tatizo ni pale unapokosa ufahamu maana wapo walosoma saana lakini ufahamu hawana kwa maana ya kwamba waloyasoma hawawezi kuyasimamia.

Kama nilivyosema naishi Canada na naujua muundo wa serikali yao na majirani zetu, hivyo maadam hapa tunazungumzia muundo wa seikali ndio haswa tunapotakiwa kujikita. Na sintokwenda nje ktk Urafiki wa Nyerere na Trudeau maana wakati wake Canada ilikuwa na marafiki wengi duniani ama niseme haikuwa na maadui hivyo ni sisi tuloacha mahusiano ya karibu na Canada na kuwaleta Wachina tena wakiishi maghorofani pale Chang'ombe.

Nilikwisha kuambia ya kwamba Muungano baina yetu na Zanzibar sio federation ila ni Political Union hivyo ndio maana watu wengi wanashazwa sana na muungano wetu wakitumia vigezo vya federation wanazozijua (kuiga). Kwetu sisi kila nchi ilikuwa na limited authority kama ilivyokuwa USSR baada ya Mapinduzi ya Lenin. Na hatuwezi kuuvunja ama kuusahihisha muungano ule pasipo kupitia vigezo na sababu zilizotufikisha hapa tulipo leo kwa miaka 50. Sababu zinazotolewa zote ni ushabiki wa vyama dhidi ya CCM.

Ndio nikasema hivi, sababu na chanzo cha mapungufu ktk muundo wa serikali zetu umetokana na mabadiliko ya mfumo wa kiuchumi mwaka 1984 na 1993 ambapo tuliacha siasa ya Ujamaa ikafuatiwa na mfumo wa vyama vingi. Mageuzi yote haya hayakufanyiwa utafiti wa kutosha kiasi kwamba hadi leo bado serikali kuu inaendesha shughuli zote za maendeleo kwa nchi 2, huui ndio mzizi wa fitna zote na changamoto kwa wabune ni kuondosha shughuli za maendeleo mikononi mwao na kuwakabidhi majimbo ili kesho vyama vya upinzani vikishinda uchaguzi wa majimbo viwe na mamlaka kamili ya kuendesha shughuli zote za maendeleo.

Hivyo basi kama nilivyosema tuwe na serikali 1, 2 au 3 kama hatukubali kuunda mfumo utakawawezesha wananchi kuchagua chama wanachoamini kitawaletea maendeleo iwe kwa madaraka mikoani, kuunda kukubali na kuwapa Zanzibar mamlaka kamili ya uendeshaji wa shughuli za serikali huku wakicangia mfuko wa Jamhuri kwa asilimia sawa na Bara.

Pia sisi wenyewe wananchi muhimu tufahamu tofauti kubwa iliyopo baina ya 1. mamlaka kamili ktk Uendeshaji wa shughuli za serikali na nyingine ni 2. Mamlaka kamili ya kuwa na kiti UN, sijui kuwa na uwezo wa kuweka mikataba nchi za nje, na ati kila nchi iwe na wizara zake zisizokuwa na mamlaka nchi nyingine shiriki Mkiziita - Mambo yasiyokuwa na Muungano na mwisho Mkipendekeza Federation ambayo serikali kuu ( ya 3) kuwa na wizara chache tu ambazo ni muhimu kuwa ktk muungano.

Hii ya pili hii ni makosa makubwa kabisa na wala haifanani na muundo wa serikali kwa nchi yeyote yenye mfumo wa federation kwa sababu hakuna wizara isokuwa muhimu kwa serikali kuu hakuna. Sasa kama mnashangaa serikali 2 kuwa ya kipekee mbona nanyi mnatuletea mapendekezo ya kipekee?


Tofauti baina ya Zanzibar na Ontario ni kubwa katika mamlaka maana Ontario wana mamlaka kamili. Quebec wana mamlaka kamili kiasi kwamba PQ wakishinda uchaguzi Ontario wataendesha wao shghuli zote za serikali na Maadam Liberal wameshinda uchaguzi Quebec ndio wao wanao ongoza shughuli zote za maendeleo ya Quebec.

Zanzibar hawana mamlaka kamili na kwa wao wanachodai sii mamlaka kama ya Ontario ama Quebec. Na pia Pinda na wapenda serikali 3 wanataka serikali kuu iwe na wizara chache tu kuepuka matumizi makubwa ilihali nchi haiwezi kuwa na serikali kuu dhaifu, hakuna nchi yenye serikali kuu dhaifu kwa sababu ndiyo yenye credit score na mamlaka ya kimataifa. Hata utawala wa Sultan au Ufalme huhakikisha kuna serikali kuu inayowakilisa utawala huo pamoja na kwamba wanatawala nchi na majimbo nje ya mipaka yao..
 
Mkuu wangu hata siku moja siandiki kwa hamaki ila pengine lugha nayotumia ndio imekuwa kali kidogo.
Swala la mungano wa Canada unaweza ku google ukaipata sintopenda kuandika vitu wakati vinapatikana ktk website hata mbumbumbu anaweza kuvipoata.

Hapa tunafahamishana jinsi wenzetu wanavyoziongoza nchi zao na sii kubishana. Uwe unaifahamu historia ya Canada ama umeisoma hili sii tatizo ila tatizo ni pale unapokosa ufahamumaana wapo walosoma saana lakini ufahamu hawana kwa maaa ya kwamba waloyasoma hawawezi kuyasimamia.

Kama nilivyosema naishi Canada na nnaujua muundo wa serikali zao, hivyo maadam hapa tunazungumzia muundo wa seikali ndio haswa tunapotakiwa kujikita. Na isintokwenda ktk Urafiki wa Nyerere na Trudeau maana wakati wake Canada ilikuwa na marafiki wengi duniani ama niseme haikuwa na maadui hivyo ni sisi tuloacha mahusiano ya karibu na Canada na kuwaleta Wachina tena wakiishi maghorofani pale Chang'ombe.

Nilikwisha kuambia ya kwamba Muungano baina yetu na Zanzibar sio federation ila ni Political Union hivyo ndio maana watu wengi wanashangaa sana kuungano wetu kwa kutumia vigezo vya federation. Kwetu sisi kila nchi ilikkuwa na limited authority kama ilivyokuwa USSR baada ya Mapinduzi ya Lenin. Na hatuwezi kuuvunga ama kuusahihisha muungano ule pasipo kupitia vigezo na sababu zilizotufikisha hapa tulipo leo kwa miaka 50.

Ndio kusema hivi sababu na chanzo cha mapungufu ktk muundo wa serikali zetu umetokana na mabadiliko ya mfumo wa kiuchumi mwaka 1984 na 1993 ambapo tuliacha siasa ya Ujamaa ikafuatiwa na mfumo wa vyama vingi. Mageuzi yote haya hayakufanyiwa utafiti wa kutosha kiasi kwamba hadi leo bado serikali kuu inaendesha shughuli zote za maendeleo kwa nchi 2.

Hivyo basi kama nilivyosema tuwe na serikali 1, 2 au 3 kama hatukubali kutoa madaraka mikoani, kuwapa Zanzibar mamlaka kamili ya uendeshaji wa shughuli za serikali. Na muhimu tufahamu tofauti kubwa iliyopo baina ya mamlaka kamili ktk Uendeshaji wa shughuli za serikali na nyingine ni mamlaka kamili ya kuwa na kiti UN kuwa na uwezo wa kuweka mikataba nchi za nje, na ati kila nchi iwe na wizara zake zisizokuwa na mamlaka nchi nyingine Mkiziita - Mambo yasiyokuwa na Muungano na mwisho Mkipendekeza Federation ambayo serikali kuu (3) kuwa na wizara chache tu ambazo ni za muungano. Hii ya pili hii ni makosa makubwa kabisa na wala haifanani na muundo wa serikali kwa nchi yeyote yenye mfumo wa federation. sasa kama mnashangaa serikali 2 kuwa ya kipekee mbona nanyi mnatuletea mapendekezo ya kipekee?


Tofauti baina ya Zanzibar na Ontario ni kubwa katika mamlaka maana Ontario wana mamlaka kamili< Quebec wana mamlaka kamili kiasi kwamba PQ wakishinda Ontarioa wataendesha wao shghuli zote za serikali na Maadam Liberal wameshinda uchaguzi Quebec ndio wao wanao ongoza shughuli zote za maendeleo ya Quebec.

Zanzibar hawana mamlaka kamili na kwa wao wanachodai sii mamlaka kama ya Ontario ama Quebec. Na pia Pinda na wapenda serikali 3 wanataka serikali kuu iwe na wizara chache tu kuepuka matumizi makubwa ilihali nchi haiwezi kuwa na serikali kuu dhaifu, hakuna nchi yenye serikali kuu dhaifu kwa sababu ndiyo yenye credit score na mamlaka ya kimataifa. Hata utawala wa Sultan au Ufalme huhakikisha kuna serikali kuu inayowakilisa utawala huo pamoja na kwamba wanatawala nchi na majimbo nje ya mipaka yao..

Mkandara:

Wewe na Nguruv3 mnataja kitu kimoja muhimu sana: MAMLAKA. Walichofanikiwa Canada, USA na nyingine ni mgawanyo na mipaka ya mamlaka. Kwa sasa hivi, mfumo wa utawala wa Tanzania hauna mipaka inayoeleweka na nguvu nyingi imechukuliwa na ofisi ya Rais. Na walio wengi bungeni ni waumini wa utawala wa rais asiye na madaraka yenye mipaka.

Kuwa na federation sio lazima entities zinazounda federation zijiunge. Kwa mfano USA ilianza na majimbo 13. Haya ndio yaliounda USA. Majimbo mengine ni maeneo yalionunuliwa, yaliotekwa au kuongezwa. Na ukiangalia ramani ya majimbo ya Marekani, utaona kuwa mipaka mingi ya majimbo ya mwanzo yaliyounda USA ilikuwa mipaka asilia (kama vile mito). Mipaka ya Majimbo yaliyoongezwa, ambayo yapo maeneo ya kati na magharibi, ni ya kupima (mipaka iliyonyooka)

Swali la kujiuliza kwanini majimbo yaliyojiunga baadaye tena mengine kwa kununuliwa au kutekwa yalipewa mamlaka kamili kama majimbo 13 yalioanzisha USA? Hawaii iliyojiunga mwaka 1959 miaka miwili kabla Tanganyika haijapa uhuru ina mamlaka sawa New York.

Jibu ya swali hili, toka mwanzo wenzetu waliona umuhimu wa watu katika maeneo yao kujiamulia matatizo yao. Kwa upande wetu hatuamini kuwa watu katika maeneo yao ndio chanzo cha maendeleo yao.

Tukiwa na watu wenye fikra kuwa maeneo mbalimbali nchini yanaweza kuwa na mamlaka ya kutatua matatizo, hili suala la katiba na mgawanyo wa mamlaka litaondoka.
 
Mkandara:

Wewe na Nguruv3 mnataja kitu kimoja muhimu sana: MAMLAKA. Walichofanikiwa Canada, USA na nyingine ni mgawanyo na mipaka ya mamlaka. Kwa sasa hivi, mfumo wa utawala wa Tanzania hauna mipaka inayoeleweka na nguvu nyingi imechukuliwa na ofisi ya Rais. Na walio wengi bungeni ni waumini wa utawala wa rais asiye na madaraka yenye mipaka.

Kuwa na federation sio lazima entities zinazounda federation zijiunge. Kwa mfano USA ilianza na majimbo 13. Haya ndio yaliounda USA. Majimbo mengine ni maeneo yalionunuliwa, yaliotekwa au kuongezwa. Na ukiangalia ramani ya majimbo ya Marekani, utaona kuwa mipaka mingi ya majimbo ya mwanzo yaliyounda USA ilikuwa mipaka asilia (kama vile mito). Mipaka ya Majimbo yaliyoongezwa, ambayo yapo maeneo ya kati na magharibi, ni ya kupima (mipaka iliyonyooka)

Swali la kujiuliza kwanini majimbo yaliyojiunga baadaye tena mengine kwa kununuliwa au kutekwa yalipewa mamlaka kamili kama majimbo 13 yalioanzisha USA? Hawaii iliyojiunga mwaka 1959 miaka miwili kabla Tanganyika haijapa uhuru ina mamlaka sawa New York.

Jibu ya swali hili, toka mwanzo wenzetu waliona umuhimu wa watu katika maeneo yao kujiamulia matatizo yao. Kwa upande wetu hatuamini kuwa watu katika maeneo yao ndio chanzo cha maendeleo yao.

Tukiwa na watu wenye fikra kuwa maeneo mbalimbali nchini yanaweza kuwa na mamlaka ya kutatua matatizo, hili suala la katiba na mgawanyo wa mamlaka litaondoka.

Mkuu

Ni muhimu sana tunapoangalia haya maswala ya muungano tuangalie na logic iliyofikisha hapo, atuwezi sema sababu awa wanafanya hivi na sisi tu-copy au namna wanavyo endesha serikari yao ndio bench mark ya good governance. Maana sio nchi zote zina mfumo wa majimbo but other forms of decentralization to serve their societal needs.

Kwa hivyo ni muhimu sana kuangalia sababu za muungano kama tunataka kuutolea mfano, for instance katiba ya America inaoana na muundo wa serikari zake ulivyo kwa sababu za awali zilizofanya hizo nchi ziungane in the first place. Lengo lao kubwa ilikuwa ni kukataa sera za mkoloni, kupinga ongezeko za kodi (itategemea unataka kurudi nyuma vipi) lakini ata swala la "Somerset v Stewart" alikupokewa vizuri especially down south, from there on a feeling of distrust, ukiongeza na kodi za ovyo jamaa wakaona ni enough.

Hivyo hata state za mwanzo lengo ilikuwa ni kuungana kwa sababu ya kupambana na colonial master lakini kila mtu abaki na serikari yake ambayo itakuwa na wajibu kwa watu wake na ndivyo hivyo ilivyo mpaka leo. Isitoshe hata wao hawakuanza na mambo yote ambayo leo federal government inasimamia vitu vingi viliongezwa baadae,mfano mara tu baada ya vita ya independence kuna majimbo yalikuwa bankrupt na kuanza kuchapisha ela ovyo kulipa madeni, hilo alikuwapendeza wengine ndio kuanza sababu ya central control ya finances ili kulinda sarafu na mambo mengi sana yamefuatia baadae kutokana na kutafuta muafaka wa kuendesha namna bora za muungano wao. Hivyo hata kesho state nyingine ikiungana itakutana na fate au na previlege zilizopo sasa kwa sababu misingi mikuu ya kuunda muungano bado hipo palepale.

Sisi atuwezi tumia sababu hizo kama mfano wa muungano wetu, kama tulilenga kwa kuona undugu wetu kingine na hapo bora muungano ufe, ndio maana kuna wengine wetu tunaona kuvunjika kwa muungano ni kiashiria ya kuwa bado kunachangamoto ZnZ, sio bara.

Maana kama kuna ukweli wa wao kwa 2/3 kuwa inaishi bara permanently, kwa siasa za sasa za ZnZ na madai yao ya serikari tatu ina maana hisia zilizofanya tuungane in the first place bado atujaweza zizima. Amna mtu anaependezewa na sera za kibaguzi bunge lao linavyofanya lakini hivi vitu vina ashiria hawa wakitoka na wabara watarudiana wenyewe kwa wenyewe. Hivi Jussa anaweza kudirika kusema mbele ya bunge la jamhuri ya watanzania eti nikapendekeza ajira za utalii kule Znz wa ZnZbari wapewe kipaumbele na nilipo kataliwa nikasusa na kutoka nje. Hawa kweli wanazingatia hata bara ikiamua kurudhisha mashambulizi hii ngoma inakuwaje.

To me it is evident kwamba kwa sasa serikali ya CCM zanzibari wanaburuzwa na Jamsheed pengine kwa kutojifahamu hivyo sio wakati sahihi kuachana nao kabisa.

Mkuu Mkandara swala la kusafisha mji limecheleweshwa sana kwa maoni yangu mie; lazima tuje na utaratibu madhubuti wa health promotion policies, maana kwa sasa serikari inatumia pesa nyingi sana kutibia magonjwa ambayo vyanzo vyake vinatokana na mazingira machafu ya kibiashara na sidhani kama hizi biashara zinarudisha hela directly hata kwa nusu kwenye gharama za afya. Its time measure are taken some ill-health are preventable or could be reduced largely, kwa mfano mi naona ni wakati sasa na makabati ya mbao kuwekea chips yawe marufuku kwa kweli i mean how do you disinfect such an equipment safely.

Bwana afya, sijui vikundi vya kupambana na epidemics, health officer ni kama hawapo wakati vyombo vyote vipo na amna measures to remove hazards or risk to health, Aiwezekani mteja auziwe chips mbele kuna dimbwi la maji machafu, magari yanarusha vumbi maana yake kipindupindu nje nje , minyoo, diarrhea, malaria kuna watu wanapatia magonjwa kwa muuza chips kwa sababu ya mazingira ya biashara yake. All this would be reduced largely especially among children with simple measures like enforcing cleanness and in return save billions of shilling in treating children.
 
Mkandara:

Wewe na Nguruv3 mnataja kitu kimoja muhimu sana: MAMLAKA. Walichofanikiwa Canada, USA na nyingine ni mgawanyo na mipaka ya mamlaka. Kwa sasa hivi, mfumo wa utawala wa Tanzania hauna mipaka inayoeleweka na nguvu nyingi imechukuliwa na ofisi ya Rais. Na walio wengi bungeni ni waumini wa utawala wa rais asiye na madaraka yenye mipaka.

Kuwa na federation sio lazima entities zinazounda federation zijiunge. Kwa mfano USA ilianza na majimbo 13. Haya ndio yaliounda USA. Majimbo mengine ni maeneo yalionunuliwa, yaliotekwa au kuongezwa. Na ukiangalia ramani ya majimbo ya Marekani, utaona kuwa mipaka mingi ya majimbo ya mwanzo yaliyounda USA ilikuwa mipaka asilia (kama vile mito). Mipaka ya Majimbo yaliyoongezwa, ambayo yapo maeneo ya kati na magharibi, ni ya kupima (mipaka iliyonyooka)

Swali la kujiuliza kwanini majimbo yaliyojiunga baadaye tena mengine kwa kununuliwa au kutekwa yalipewa mamlaka kamili kama majimbo 13 yalioanzisha USA? Hawaii iliyojiunga mwaka 1959 miaka miwili kabla Tanganyika haijapa uhuru ina mamlaka sawa New York.

Jibu ya swali hili, toka mwanzo wenzetu waliona umuhimu wa watu katika maeneo yao kujiamulia matatizo yao. Kwa upande wetu hatuamini kuwa watu katika maeneo yao ndio chanzo cha maendeleo yao.

Tukiwa na watu wenye fikra kuwa maeneo mbalimbali nchini yanaweza kuwa na mamlaka ya kutatua matatizo, hili suala la katiba na mgawanyo wa mamlaka litaondoka.
Shukran mkuu wangu na ndio maana haswa ya ajizi ya Mwafrika kuwa nyumba ya umaskini.

Sasa kama hawa jamaa wamenisoma vizuri wataelewa ya kwamba sipingi lolote juu ya serikali 2 ama 3 kwa sababu siamini kuwa matatizo yetu yapo ktk muundo wa serikali SIASAKi isipokuwa ni mfumo wa KIUCHUMI ulotuweka sote nyuma na hata ukiyatazama kwa makini madai ya Zanzibar yanahusiana zaidi na UCHUMI hivyo suluhisho walofikia jamaa zetu ni kugawana umaskini.

Watabisha sana juu ya hili na kwamba Muungano hautavunjika lakini ukiwasoma maelezo yao utaziona Jazba, hamaki na uchu ndio umetanugulia maamuzi yao. Utasikia Zanzibar wanatunyonya sisi tena basi Bara haina faida yoyote ambayo Zanzibar wakidai wao ndio wanaumia zaidi ktk muungano huu kwa sababu tu ati zamani makamu wa rais alikuwa ndiye rais wa Zanzibar sasa hapo nani alokataa Bilal asiwe rais wa Zanzibar pia au ndivyo walivyotaka wao?. Yote kwa ujumla wao ni vurugu ya kutaka kufaidika na Muungano na sii Udugu tulokuwa nao baina yetu.

Kuna Mapungufu mawili tu ktk mahitaji yetu ya Mfumo wa Utawala na ambao ndio chanzo cha KERO zote. Hizi wakizipatia dawa basi hakuna upande wala nchi utakuja lalamikia mwenza hata ikiwa ktk mfumo wowote wa serikali.

1. Bado tunaendelea na Mfumo wa Kijamaa ambapo serikali kuu imeshika mamlaka ya kuendesha shughuli zote za serikali kama tulivyokuwa enzi za mwalimu. Mamlaka ya chini kabisa wamepewa Zanzibar na hata Mikoa, Halmashauri na serikali za mitaa kiasi kwamba nchi nzima inategemea serikali kuu kupanga na kuendesha shughukli za maendeleo na hivyo kukusanya asilimia 100 wao na kuzigawa kama ilivyokuwa toka wakati wa Nyerere.

2. Kugawa wizara zetu kuwa za Muungano na nyingine zisizokuwa za muungano jambo ambalo linaidhoofisha serikali kuu kwa kuachiwa wizara ambazo haina mapato. Wakati hakuna wizara hata moja ambayo haiwezi kuwa na maswala ya Kimataifa International hivyo ni mamlaka tu ya kuendesha shughuli za serikali ndio yanakuwa sii ya Muungano lakini sii wizara zake. Mfano wizara ya Kilimo inakuwa Bara na Visiwani ila kila upande wanashughulikia Kilimo kwa msaada mkubwa toka serikali kuu aidha kutafuta soko ama kutafuta mikopo ya mbolea na pembejeo kutoka nje. Zanzibar haina Credit wala Bara haina credit!


Katika mfumo huu kila serikali iwe ya nchi ama majimbo itachangia asilimi 60 ktk mfuko wa Taifa na ile 40 itabakia ktk nchi ama jimbo kisha serikali kuu itatumia hizo asilimia 60 ktk ujenzi wa miundo mbinu kulingana na mahitaji ya Nchi, ama jimbo. ivyo nashangaa Chadema kutoka ktk hoja yao ya msingi wameingia ktk mkenge huu wa kugawana Umasikini wakati CCM itaendelea kuwa na nguvu kubwa kama tutaendelea na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ambayo ni itikadi ya chama hicho
 
Mkuu

Ni muhimu sana tunapoangalia haya maswala ya muungano tuangalie na logic iliyofikisha hapo, atuwezi sema sababu awa wanafanya hivi na sisi tu-copy au namna wanavyo endesha serikari yao ndio bench mark ya good governance. Maana sio nchi zote zina mfumo wa majimbo but other forms of decentralization to serve their societal needs.

Kwa hivyo ni muhimu sana kuangalia sababu za muungano kama tunataka kuutolea mfano, for instance katiba ya America inaoana na muundo wa serikari zake ulivyo kwa sababu za awali zilizofanya hizo nchi ziungane in the first place. Lengo lao kubwa ilikuwa ni kukataa sera za mkoloni, kupinga ongezeko za kodi (itategemea unataka kurudi nyuma vipi) lakini ata swala la "Somerset v Stewart" alikupokewa vizuri especially down south, from there on a feeling of distrust, ukiongeza na kodi za ovyo jamaa wakaona ni enough.

Hivyo hata state za mwanzo lengo ilikuwa ni kuungana kwa sababu ya kupambana na colonial master lakini kila mtu abaki na serikari yake ambayo itakuwa na wajibu kwa watu wake na ndivyo hivyo ilivyo mpaka leo. Isitoshe hata wao hawakuanza na mambo yote ambayo leo federal government inasimamia vitu vingi viliongezwa baadae,mfano mara tu baada ya vita ya independence kuna majimbo yalikuwa bankrupt na kuanza kuchapisha ela ovyo kulipa madeni, hilo alikuwapendeza wengine ndio kuanza sababu ya central control ya finances ili kulinda sarafu na mambo mengi sana yamefuatia baadae kutokana na kutafuta muafaka wa kuendesha namna bora za muungano wao. Hivyo hata kesho state nyingine ikiungana itakutana na fate au na previlege zilizopo sasa kwa sababu misingi mikuu ya kuunda muungano bado hipo palepale.

Sisi atuwezi tumia sababu hizo kama mfano wa muungano wetu, kama tulilenga kwa kuona undugu wetu kingine na hapo bora muungano ufe, ndio maana kuna wengine wetu tunaona kuvunjika kwa muungano ni kiashiria ya kuwa bado kunachangamoto ZnZ, sio bara.

Maana kama kuna ukweli wa wao kwa 2/3 kuwa inaishi bara permanently, kwa siasa za sasa za ZnZ na madai yao ya serikari tatu ina maana hisia zilizofanya tuungane in the first place bado atujaweza zizima. Amna mtu anaependezewa na sera za kibaguzi bunge lao linavyofanya lakini hivi vitu vina ashiria hawa wakitoka na wabara watarudiana wenyewe kwa wenyewe. Hivi Jussa anaweza kudirika kusema mbele ya bunge la jamhuri ya watanzania eti nikapendekeza ajira za utalii kule Znz wa ZnZbari wapewe kipaumbele na nilipo kataliwa nikasusa na kutoka nje. Hawa kweli wanazingatia hata bara ikiamua kurudhisha mashambulizi hii ngoma inakuwaje.

To me it is evident kwamba kwa sasa serikali ya CCM zanzibari wanaburuzwa na Jamsheed pengine kwa kutojifahamu hivyo sio wakati sahihi kuachana nao kabisa.

Mkuu Mkandara swala la kusafisha mji limecheleweshwa sana kwa maoni yangu mie; lazima tuje na utaratibu madhubuti wa health promotion policies, maana kwa sasa serikari inatumia pesa nyingi sana kutibia magonjwa ambayo vyanzo vyake vinatokana na mazingira machafu ya kibiashara na sidhani kama hizi biashara zinarudisha hela directly hata kwa nusu kwenye gharama za afya. Its time measure are taken some ill-health are preventable or could be reduced largely, kwa mfano mi naona ni wakati sasa na makabati ya mbao kuwekea chips yawe marufuku kwa kweli i mean how do you disinfect such an equipment safely.

Bwana afya, sijui vikundi vya kupambana na epidemics, health officer ni kama hawapo wakati vyombo vyote vipo na amna measures to remove hazards or risk to health, Aiwezekani mteja auziwe chips mbele kuna dimbwi la maji machafu, magari yanarusha vumbi maana yake kipindupindu nje nje , minyoo, diarrhea, malaria kuna watu wanapatia magonjwa kwa muuza chips kwa sababu ya mazingira ya biashara yake. All this would be reduced largely especially among children with simple measures like enforcing cleanness and in return save billions of shilling in treating children.
Mkuu neno hili AJIZI nyumba ya Njaa nimelibadilisha makusudi kwa sababu na sababu zenyewe ni kama hizo ulizoziweka hapo juu maana sisi tuna wasomi walosoma sana lakini hawakujaliwa UFAHAMU na kibaya zaidi tunashindwa hata kumuomba Mola atujalie Ufahamu. Hivyo usomi wetu wooote ni wa majukwaani tu hauwezi kuweka elimu hiyo ktk vitendo kama Masheikh/Wachungaji wanaosema usifuate nayofanya fuata nayoyasema!..

Inanishangaza sana kuona maamuzi yetu siku zote, mara zote hutokana na kero na sii Mapungufu ambayo yanahitaji muundo bora wa kutuwezesha kukabiliana na matatizo yaliyopo kabla hayajawa kero. Mji wa Dar hauwezi kuwa msafi pasipo utaratibu mzuri wa kisheria unaosisitiza Usafi wa mazingira kiasi kwamba iwe utamaduni wa wakazi wa Jiji.

Miundombinu pia ijengwe kulingana na makuzi ya jiji lenyewe lakini tazama kama soko la Kariakoo ambalo lilijengwa na Mwalimu toka miaka ya 70 Population ya jii ikiwa chini ya Mil.2 lakini hadi leo ndilo soko kubwa kuliko yote. Kisha kwa ujinga ule ule soko hilo halikuffganyiwa mapanuzi ila wamehamisha makao makuu ya soko kuwa Ilala ili magari ya mazao yaishie soko la Ilala ambalo pia halitoshelezi.

Sasa tazama maamuzi yalotolewa kuusafisha mji. Kima Mama ntilie ndio wanafukuzwa, mabanda ya wachuuzi wadogo wadogo ndio wanapigwa vita wakati hawa watu wana serve asilimi 80 ya wakazi wa Dar ambao uwezo wao ni mdogo sana kwenda ktk masoko ya kisasa (supermarket). Na ukijiuliza hivi kweli uchafu wa mama Ntilie na mchuuzi wa sokoni ni zile bidhaa wanazouza ama uchafu wa mazingira yenyewe. Kukosekana kwa vifaa vya usafi na hata uwezo wa kukusanya usafi maana hata ukienda Muhimbili leo utashikwa na kichefuchefu, huko ndani hakuna Mama Ntilie wala wachuuzi. Nenda ofisi za serikali, ndani ya masoko, barabara ndogo (mitaa) madukani kote uogopa hata kuingia maana mazingira yanatisha. yananuka!.

Kifupi mji mzima wa Dar ni hatarishi kwa uhai wa binadamu. Na nvua hii ilonyesha kwa muda wa wiki nzima imetuonyesha jinsi gani mji wetu ni mchafu mbali kabisa na hao kina mama Ntilie na wachuuzi. Barabara za lami zimegeuka kuwa za tope taka kila kona halafu kama alivyosema Mwalimu Nyerere kuhusu Corruption.

Mwalimu alionya sana ya kwamba ktk utawala wenye rushwa kubwa kubwa tutawatumikia matajiri na itafika wakati askari wetu watawanyanyasa watu wadogo wadogo. Hotuba hii nimeisikia jana tu baada ya taarifa ya Habari ya TBC jion na kila alosema mwalimu ktk hotuba hiyo yanaonekana leo wazi kabisa lakini haiwanyimi usingizi viongozi wetu kwa sababu wao ni watumishi wa Matajiri. Mjio hautaweza kuwa msafi na hatutaweza kukidhi mapungufu kwa kutazama kero. safari yetu kufikia maendeleo inazidi kuwa nguvu na ndefu zaidi. AJIZI hizi ndio nyumba ya Umaskini...
 
Mkuu

Ni muhimu sana tunapoangalia haya maswala ya muungano tuangalie na logic iliyofikisha hapo, atuwezi sema sababu awa wanafanya hivi na sisi tu-copy au namna wanavyo endesha serikari yao ndio bench mark ya good governance. Maana sio nchi zote zina mfumo wa majimbo but other forms of decentralization to serve their societal needs.

Kwa hivyo ni muhimu sana kuangalia sababu za muungano kama tunataka kuutolea mfano, for instance katiba ya America inaoana na muundo wa serikari zake ulivyo kwa sababu za awali zilizofanya hizo nchi ziungane in the first place. Lengo lao kubwa ilikuwa ni kukataa sera za mkoloni, kupinga ongezeko za kodi (itategemea unataka kurudi nyuma vipi) lakini ata swala la "Somerset v Stewart" alikupokewa vizuri especially down south, from there on a feeling of distrust, ukiongeza na kodi za ovyo jamaa wakaona ni enough.

Hivyo hata state za mwanzo lengo ilikuwa ni kuungana kwa sababu ya kupambana na colonial master lakini kila mtu abaki na serikari yake ambayo itakuwa na wajibu kwa watu wake na ndivyo hivyo ilivyo mpaka leo. Isitoshe hata wao hawakuanza na mambo yote ambayo leo federal government inasimamia vitu vingi viliongezwa baadae,mfano mara tu baada ya vita ya independence kuna majimbo yalikuwa bankrupt na kuanza kuchapisha ela ovyo kulipa madeni, hilo alikuwapendeza wengine ndio kuanza sababu ya central control ya finances ili kulinda sarafu na mambo mengi sana yamefuatia baadae kutokana na kutafuta muafaka wa kuendesha namna bora za muungano wao. Hivyo hata kesho state nyingine ikiungana itakutana na fate au na previlege zilizopo sasa kwa sababu misingi mikuu ya kuunda muungano bado hipo palepale.

Sisi atuwezi tumia sababu hizo kama mfano wa muungano wetu, kama tulilenga kwa kuona undugu wetu kingine na hapo bora muungano ufe, ndio maana kuna wengine wetu tunaona kuvunjika kwa muungano ni kiashiria ya kuwa bado kunachangamoto ZnZ, sio bara.

Maana kama kuna ukweli wa wao kwa 2/3 kuwa inaishi bara permanently, kwa siasa za sasa za ZnZ na madai yao ya serikari tatu ina maana hisia zilizofanya tuungane in the first place bado atujaweza zizima. Amna mtu anaependezewa na sera za kibaguzi bunge lao linavyofanya lakini hivi vitu vina ashiria hawa wakitoka na wabara watarudiana wenyewe kwa wenyewe. Hivi Jussa anaweza kudirika kusema mbele ya bunge la jamhuri ya watanzania eti nikapendekeza ajira za utalii kule Znz wa ZnZbari wapewe kipaumbele na nilipo kataliwa nikasusa na kutoka nje. Hawa kweli wanazingatia hata bara ikiamua kurudhisha mashambulizi hii ngoma inakuwaje.

To me it is evident kwamba kwa sasa serikali ya CCM zanzibari wanaburuzwa na Jamsheed pengine kwa kutojifahamu hivyo sio wakati sahihi kuachana nao kabisa.

Mkuu Mkandara swala la kusafisha mji limecheleweshwa sana kwa maoni yangu mie; lazima tuje na utaratibu madhubuti wa health promotion policies, maana kwa sasa serikari inatumia pesa nyingi sana kutibia magonjwa ambayo vyanzo vyake vinatokana na mazingira machafu ya kibiashara na sidhani kama hizi biashara zinarudisha hela directly hata kwa nusu kwenye gharama za afya. Its time measure are taken some ill-health are preventable or could be reduced largely, kwa mfano mi naona ni wakati sasa na makabati ya mbao kuwekea chips yawe marufuku kwa kweli i mean how do you disinfect such an equipment safely.

Bwana afya, sijui vikundi vya kupambana na epidemics, health officer ni kama hawapo wakati vyombo vyote vipo na amna measures to remove hazards or risk to health, Aiwezekani mteja auziwe chips mbele kuna dimbwi la maji machafu, magari yanarusha vumbi maana yake kipindupindu nje nje , minyoo, diarrhea, malaria kuna watu wanapatia magonjwa kwa muuza chips kwa sababu ya mazingira ya biashara yake. All this would be reduced largely especially among children with simple measures like enforcing cleanness and in return save billions of shilling in treating children.

Zinjas:

Mambo uliyozungumza ni sawa kabisa lakini hoja yangu haikulenga kwenye ku-copy serikali ya majimbo. Nimetoa mfano wa majimbo ya USA na jinsi mipaka ya mamlaka inavyoheshimiwa. Huwezi kuwa na decentrazation yenye ufanisi wakati hakuna mipaka ya mamlaka inayojulikana.

Kwa mfano mwaka 1972 Nyerere alifanya decentrazation aliyoita madaraka mikoani. Lakini mikoa haikuwa na mamlaka ya kujiamulia mambo yao. Kila mipango ya maendeleo ilitoka Ikulu na viongozi wa mikoa walikuwa kama viranja au wanyampala.

Katiba ni nzuri kwa kuangalia watu wanayoitumia. Liberia wali-copy mambo mengi kutoka USA: Katiba, Bendera. Lakini hawakuheshimu waliyokopi na matokeo yake walikuwa mabaya. Vilevile sio mambo yote mazuri yanayofanyika USA, Canada, yameandikwa kwenye katiba zao. Mambo mengi yanatokana na utamaduni wa wananchi na viongozi. Viongozi wa Tanzania hawana utamaduni wa kuheshimu katiba. Wanaitumia katiba hili kuhalalisha mamlaka yao lakini sio kuitumia kama mwongozo wa nchi.
 
Shukran mkuu wangu na ndio maana haswa ya ajizi ya Mwafrika kuwa nyumba ya umaskini.

Sasa kama hawa jamaa wamenisoma vizuri wataelewa ya kwamba sipingi lolote juu ya serikali 2 ama 3 kwa sababu siamini kuwa matatizo yetu yapo ktk muundo wa serikali SIASAKi isipokuwa ni mfumo wa KIUCHUMI ulotuweka sote nyuma na hata ukiyatazama kwa makini madai ya Zanzibar yanahusiana zaidi na UCHUMI hivyo suluhisho walofikia jamaa zetu ni kugawana umaskini.

Watabisha sana juu ya hili na kwamba Muungano hautavunjika lakini ukiwasoma maelezo yao utaziona Jazba, hamaki na uchu ndio umetanugulia maamuzi yao. Utasikia Zanzibar wanatunyonya sisi tena basi Bara haina faida yoyote ambayo Zanzibar wakidai wao ndio wanaumia zaidi ktk muungano huu kwa sababu tu ati zamani makamu wa rais alikuwa ndiye rais wa Zanzibar sasa hapo nani alokataa Bilal asiwe rais wa Zanzibar pia au ndivyo walivyotaka wao?. Yote kwa ujumla wao ni vurugu ya kutaka kufaidika na Muungano na sii Udugu tulokuwa nao baina yetu.

Kuna Mapungufu mawili tu ktk mahitaji yetu ya Mfumo wa Utawala na ambao ndio chanzo cha KERO zote. Hizi wakizipatia dawa basi hakuna upande wala nchi utakuja lalamikia mwenza hata ikiwa ktk mfumo wowote wa serikali.

1. Bado tunaendelea na Mfumo wa Kijamaa ambapo serikali kuu imeshika mamlaka ya kuendesha shughuli zote za serikali kama tulivyokuwa enzi za mwalimu. Mamlaka ya chini kabisa wamepewa Zanzibar na hata Mikoa, Halmashauri na serikali za mitaa kiasi kwamba nchi nzima inategemea serikali kuu kupanga na kuendesha shughukli za maendeleo na hivyo kukusanya asilimia 100 wao na kuzigawa kama ilivyokuwa toka wakati wa Nyerere.

2. Kugawa wizara zetu kuwa za Muungano na nyingine zisizokuwa za muungano jambo ambalo linaidhoofisha serikali kuu kwa kuachiwa wizara ambazo haina mapato. Wakati hakuna wizara hata moja ambayo haiwezi kuwa na maswala ya Kimataifa International hivyo ni mamlaka tu ya kuendesha shughuli za serikali ndio yanakuwa sii ya Muungano lakini sii wizara zake. Mfano wizara ya Kilimo inakuwa Bara na Visiwani ila kila upande wanashughulikia Kilimo kwa msaada mkubwa toka serikali kuu aidha kutafuta soko ama kutafuta mikopo ya mbolea na pembejeo kutoka nje. Zanzibar haina Credit wala Bara haina credit!


Katika mfumo huu kila serikali iwe ya nchi ama majimbo itachangia asilimi 60 ktk mfuko wa Taifa na ile 40 itabakia ktk nchi ama jimbo kisha serikali kuu itatumia hizo asilimia 60 ktk ujenzi wa miundo mbinu kulingana na mahitaji ya Nchi, ama jimbo. ivyo nashangaa Chadema kutoka ktk hoja yao ya msingi wameingia ktk mkenge huu wa kugawana Umasikini wakati CCM itaendelea kuwa na nguvu kubwa kama tutaendelea na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ambayo ni itikadi ya chama hicho

Mkandara:

Tanganyika yenyewe ina eneo kubwa na watu zaidi ya milioni 40. Kuirudisha serikali ya Tanganyika kwa mfumo uliopo sasa bado hakutasaidia watanganyika. Umefika wakati watanganyika wawe wabunifu. Wanapodai serikali yao basi waonyesha wanadai muundo wa serikali yenye ufanisi vilevile.
 
Wakuu Mkandara na Zakumi

Jiji la Dar-Es-Salaam ni picha kamili what is wrong with our national politics, priorities, weledi wa viongozi na madhara ya kukosa dira si la taifa tu, ata kwenye local governments target policies.

Sielewi kabisa shughuli ya mameya na kazi ya serikari za mitaa it is as if wao kazi yao kuuza viwanja tu. Kama unaangalia hata thread zingine jukwaa la siasa kuna baadhi ya wabunge wanachukua lawama sana kwa shughuli za viongozi wa serikari za mitaa.

Ukiangalia siasa hizi hizi za serikari ya mitaa nyanda za juu kama Mwanza na Musoma jamaa kule wameanza kuwajabika kwa sababu ya siasa za ushindani majuzi walimfungia meya matata asishiriki kwenye budget ya mwanza mjini kwa sababu aaminiki tena kwa mujibu. Kuna thread kazaa za uchakachuaji wa majengo ambazo manispaa ya Mwanza inasimamia na watu wana amshana kule kutafuta accountability.

Hayo mambo yamesaidia serikari za mitaa kuanza kuangalia miundombinu na namna bora za kutumia mapato yao nyanda za juu. Mfano mwanza mjini kuna anza kuwa kusafi kwa sababu wametenga budget ya kusafisha katikati ya mji kama nakumbuka vizuri. Bado wanachangamoto lakini siasa za serikari za ngazi hizi kule zimeanza kuzaa matunda kutokana na vuguvugu la siasa za ushindani.

Dar-Es-Salaam ni kichefu chefu kuna thread kazaa alizo anzisha critical thinker or some name bearing those hallmarks, ameweka hoja kadhaa kenye jukwaa la siasa akiponda uongozi wa jiji la Dar-Es-Salaam, kikubwa akihoji wahusika bado hawana concept ya kazi kubwa na changamoto walizo nazo kama viongozi wa jiji kubwa hili kuuweka katika ramani kama mji wa kisasa.

Pili serikari aina malengo ya afya, ingekuwa lengo la usafi ni afya wange encourage kwanza wafanya biashara ku-adapt better practices kama ulivyosema kwakuwa wana serve a large proportion of those marginalized among us na wangetenga sehemu maalum za kibiashara hili watu wasitapake hovyo mabarabarani.

Since their services have higher demands to be ignored. Ni bora kungekuwa na course za kuwafundisha jinsi ya kufanya biashara katika mazingira ya usafi (maana wengine practices zao ni kwa sababu ya ignorance na kwa tanzania sidhani kama kabla ujafunguwa kibanda chako cha chakula unahitaji hata kuwa na certificate ya 'food hygiene' or 'health and safety'), lakini lazima tuwe wakweli most of these businesses are just about hand to mouth hivyo lazima waangaliwe kwa jicho la huruma na kuboreshewa mazingira ya kazi.

Kingine hapa kuna uhaba wa supportive sector kwenye service za chakula amna wajasiriamali watu wanaenda kwa mama ntilie inabidi wale palepale watu wanashindwa kutengeneza hata mabox ya plastic au 'polystyrene containers' hili wafanyakazi wabebe hata take away uchafu wakatupie kwenye ma-bin ya kazini. Yaani hata chips unafungiwa kwenye magazeti au foil paper urojo wote unakumwagikia come on watu wamekaa ulaya miaka yote hata kusema jamani embu tuwatengezee maboksi ya chips au expansive can that be, sasa kweli wataweza hata kutengeneza yale makabati ya chips ya mabati na mashine za kuweka chakula kibaki cha moto. Hivyo ni vifaa ambavyo nadhani sasa vinahitajika sio dar-es-salaam bali tanzania nzima and are commercial sound kwenye kuboresha mazingira na afya. Sisi bado na kuna vast opportunity ila watu wamelala nimejiuliza sana hawa watu walionza kurudi kabla yetu miaka yote hawakuona opportunities zilizojaa zaidi ya kwenda kushindana na wenye malori sijui mabasi no wonder wengi wanafail wakirudi kwa sababu ni zero creativity.

Kwa hivyo magoi goi wa serikari za mitaa na wao wanatakiwa kuinvest on infrastructure ambazo zinalenga kuboresha usafi wa mazingira na wafanya biashara wadogo watozwe a small licence fee towards that contribution na sio kodi ya mapato hilo siliafiki kutokana na faida zenyewe kuwa ndogo.

Tatu kutanua mji wa Dar-Es-Salaam traffic is centered towards on direction, all the outer zones head towards one direction at the moment, hivyo kupanua soko la kariakoo would just increase the capacity but it wont reduce the congestion of both the motors and people heading there, in addition to the already large population that is sheltered in those high rises (hapana aisee kariakoo if you ask me kwa sasa soko inabidi liondoke kabisa, jamaa wamearibu sana na migorofa, sijui ni ushamba). With those facts there would be even larger piles of rubbish to clear.

Inabidi watu wakae chini na waangalie sababu za kwanini watu wanaenda kariakoo na kupunguza safari za huko, serikari za mitaa zetu zimezubaa. Mfano kama UK ambapo kuna mfumo kama wa Tanzania local governments zinashindana kutafuta wawekezaji. Unakuta serikari inaona ikijenga soko ikalimiki ni good investment maana unapokea kodi za mapango na licence fees za kufanyia kazi, serikari kuu inachukua kodi where necessary na wao wanapata licence fees na kodi na kuna magari ya kukusanya uchafu kwa wenye biashara za chakula kama mafuta na food products huku wakichajiwa.

Lakini sio sisi tunashangaa na hayo mapato ndio yanasaidia ku-improve sehemu nyingine kama ku-invest kwenye properties, miundombinu kama mitaro etc lakini wao wanategemea mapato ya matangazo na mgao wa central government lakini creativity ni zero.

Na kodi zinazokusanya Dar unakuta serikari kuu kila kodi inarudisha kwenye mji kwa namna moja ama nyingine kuboresha jiji zima kama miundo mbinu za barabara kuu, vituo vya mabasi au hata kujenga Airport (sisi tunaona kama vile uwanja wa ndege ni public good, wakati wenzetu wanaona kama vile cash cow).

Mfano safari za ndege sasa hivi zinavyozidi kuwa cheap watu wanasafiri sana kibiashara a long stay car park ya wiki inaleta hela, ukifungua uwanja mkubwa na sehemu za maduka tayari yale yale ya uchumi wa sokoni yana amia airpot with a different marketing strategy in mind to entice big names only kama vile mabaa ya kisasa kuwepo hapo, supermarket ya size ndogo etc na vitu vingi tu. Lakini wapi?

Nne, umegusia kitu muhimu sana (Sheria) ambacho bila ya kigezo hicho kupewa national attention maendeleo yetu yatachukua muda mrefu sana. Sheria kwa Tanzania si kitu cha muhimu au ambacho kina fahamika na wengi hili kiweze eshimiwa. Tatizo hili linaanzia na mfumo wa elimu nahisi, likiendelezwa na poor regulators.

Kwa sasa watu pekee ambao naona wanafanya kazi yao ni wakaguzi wa bidhaa those people are taking their role serious atleat ukiwafananisha na regulators wengine na sasa naona wafanya biashara makanjanja wanaanza kufikiria mara mbili kuleta bidhaa feki jamaa wanazuia production, wanafunga biashara au wanataifisha bidhaa mchana kweupe. With that commitment in the long run itazaa matunda tu ya kuheshimu quality demanded by the government.

Ukirudi kwenye ufahamu wa sheria na wafanyakazi wa umma ni tatizo, sheria nyingi za serikari azifikii malengo yange kwakuwa implementers wenyewe ndio wasio ziheshimu huko makazini kwao au kuzi-enforce. Kwa wenzetu inakuwa ngumu sana kupachikana kwenye ajira kwa sababu mfanyakazi yeyote anatakiwa azielewe sheria za mazingira ya kazi yake maana hizo ukizivunja, kampuni inapelekwa mahakamani na kupigwa faini za nguvu. Sasa wewe usishangae kwa mfano Tanzania labda kungekuwa na sheria ya usimamizi wa usafi (mtu ambae anatakiwa akague mazingira ya usafi ndio atakuwa mpokeaji mkubwa wa rushwa na kuacha watu watupe uchafu sehemu zisizo takiwa) na hivyo ndio mambo yanavyofanyika sehemu zote za serikari.

Hapo ndio nadhani ndio tatizo lilipo wafanyakazi wengi hawaelewi hata sheria za kazi zao vinginevyo huwezi kwenda hospitali dokta akuchunie akijua hilo ni kosa lakufungwa with the right watch-dogs au hata hospitali yenyewe inayotibu wagonjwa ndio chanzo cha magonjwa wako wapi wasimamizi wa afya, without laws and enforcement officers tutasogea polepole sana, mi nadhani imefikia wakati hili swala hilo lipewe kipaumbele sehemu za umma na private. Maloya wetu embu nao wawe wajasiriamali kidogo kusaka opportunities za uzembe, serikarini kwa sasa kuna mpunga wa nguvu watu kuzidi kuwa matajiri kwenye fani hiyo kutokana watendaji wahuni waliojaa Tanzania.
 
Zakumi na Zinjathropus,

I wish na nitasema tena Iwish hawa jamaa wote wa ukumbi huu, baraza la Katiba na viongozi wengine wa vyama na serikali, asasi za kijamii wamepata muda wa kuwasoma ili kidogo iwasaidie kuelewa haswa nini chimbuko la kero zetu na sii kukimbilia Muungano. Kuna mambo mengi sana ambayo tunayafanya kinyume kabisa ca ustaarabu ama weredi wa maswala yote ya kiutawala na pengine hata niseme umuhimu wa KATIBA yenyewe.

Nawaomba great thinker woote wapitie mabandiko yenu japo mmeandika kwa ufupi sana pengine tunaweza kubadilisha fikra na mitazamo ya kizazi hiki maana binafsi yangu naona kama tunarudi nyuma vile. Ustaraabu umekwisha, watu hawana aibu, hekima na busara zimekuwa kama elimu ya kununua. Sijui bana pengine labda walosema waswahili kuwa akili nyingi huondoa maarifa ndio hii.

Shukran sana nimewasoma na hakika tusipobadilika, AJIZI hii itakuwa kama mdudu asotibika..
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom