Akiba ya pesa kwenye akaunti kwa dola za Marekani ni bora kuliko Shilingi za kitanzania?

Akiba ya pesa kwenye akaunti kwa dola za Marekani ni bora kuliko Shilingi za kitanzania?

Nendeni DTB dollar account ni $1 per month Na unafanya withdraw mpaka $10000 bure hivo hii ni salama zaidi

Lakini hoja ya mtoa mada itakuwa sahihi tu pale ambapo dollar imepanda zaidi ya ile bei uliyonunulia

Hivi DTB ni benki ya kuaminika? maana mkuu ukianza mchakato kama huo wa kuweka vidola vyako halafu ukaambiwa benki imefirisika, unaweza kupelekwa milembe huku unajiona.
 
Hivi DTB ni benki ya kuaminika? maana mkuu ukianza mchakato kama huo wa kuweka vidola vyako halafu ukaambiwa benki imefirisika, unaweza kupelekwa milembe huku unajiona.
Mkuu Agha Khan yule Wala huwezi fananisha credibility ya DTB Na bank nyingi tu hapa nyumbani jamaa wako smart sana kwenye masuala ya pesa mimi ndio bank yangu miaka nenda rudi Na nipo salama kabisaaa
 
Inategemea na chanzo chako cha hizo dollar, kama unazipata moja kwa moja kama dollar, ni vizuri ukaziweka katika akaunt ya usd, zipo benki hazitozi makato ya kila mwezi, utakatwa pale unapotaka kutoa pesa tu. Kwa maana hiyo, lengo lako kama ni kuweka akiba, hautakua unatoa mara kwa mara.

Lakini endapo unapokea Tshs kisha ununue usd uweke akiba, hakikisha ni mpango wa muda mrefu.
 
Mkuu Agha Khan yule Wala huwezi fananisha credibility ya DTB Na bank nyingi tu hapa nyumbani jamaa wako smart sana kwenye masuala ya pesa mimi ndio bank yangu miaka nenda rudi Na nipo salama kabisaaa
Ata mm hii ndo bank yangu wako vizuri sana sana
 
Inategemea na chanzo chako cha hizo dollar, kama unazipata moja kwa moja kama dollar, ni vizuri ukaziweka katika akaunt ya usd, zipo benki hazitozi makato ya kila mwezi, utakatwa pale unapotaka kutoa pesa tu. Kwa maana hiyo, lengo lako kama ni kuweka akiba, hautakua unatoa mara kwa mara.

Lakini endapo unapokea Tshs kisha ununue usd uweke akiba, hakikisha ni mpango wa muda mrefu.
Huu ndo Ushauri wa kutuata niliwahi kufanya hivi nilikuwa napata dollar moja Kwa moja Kwa bei ya chini kabisa niliweza kusave hela nyingi na nilikuwa nadhiifadhi ndani
 
Huu ndo Ushauri wa kutuata niliwahi kufanya hivi nilikuwa napata dollar moja Kwa moja Kwa bei ya chini kabisa niliweza kusave hela nyingi na nilikuwa nadhiifadhi ndani
Naona mnafukua makaburi!!!ushauri mzuri huo ila sasa mdau SPINE inabidi aje atupe mrejesho kama alifungua a/c au la maana ni miaka 4 sasa tangu alete huu uzi.

Ila bado kwa wale wanaoingiza ela kwa posho nyingi za vikao na safari nyingi nyingi za kikazi au anakuwa na deal nyingi nje ya kipato chake sio mbaya wakiwekeza huku hata kama watafanya exchange bado itakuja kuwasaidia baadae
 
Back
Top Bottom