Akili Bandia ya 'Bard AI' sasa inakubali lugha ya Kiswahili

Akili Bandia ya 'Bard AI' sasa inakubali lugha ya Kiswahili

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1689262310183.png

Akili Bandia ya Bard ambayo inamilikiwa na Google ili kushindana na Akili Bandia ya ChatGPT imefanya mabadiliko.

Google Bard imeongeza upatikanaji wake kwa lugha zaidi ya 40 ikiwemo lugha ya Kiswahili. Sasa hivi unaweza kuuliza akili bandia ya Google maswali yoyote kwa lugha ya kiswahili na inajibu kwa lugha ya kiswahili.

𝗣𝗶𝗮 𝗸𝘂𝗮𝗻𝘇𝗶𝗮 𝗹𝗲𝗼 𝗔𝗸𝗶𝗹𝗶 𝗕𝗮𝗻𝗱𝗶𝗮 𝘆𝗮 𝗕𝗮𝗿𝗱 𝗶𝘁𝗮𝗸𝘂𝘄𝗮 𝗻𝗮 𝗺𝗮𝗯𝗼𝗿𝗲𝘀𝗵𝗼 𝘆𝗮𝗳𝘂𝗮𝘁𝗮𝘆𝗼:

🔘 Uwezo wa ku-pin majibu. Hivyo itasaidia kama kuna majibu ambayo ungependelea kuyahifadhi.

🔘 Ina uwezo wa kuzungumza na kuyasoma majibu kwa sauti - Read Aloud

🔘 Ina uwezo wa kuchagua urefu wa majibu; unaweza kuchagua ikupatie maelezo mengi au maelezo machache.

🔘 Sasa unaweza ku-upload picha na ikaitazama na kukupatia majibu kwa kukagua picha. Imeunganishwa na Google Lens.

🔘 Imeongeza uwezo wa ku-export kwenye Google Colab na Python Replit

SWAHILITEK
 
Google wako vizuri ijapokuwa Microsoft walitangulia wameshapigwa gap
Kwenye masuala kama haya mbona wachina hawapo? Nilikuwa nategemea wachina watakuja na AI yao.
Nilitegemea pia wachina watakuja na OS yao ambayo itakuwa shindani kwenye Windows computer, Android na IOS?
Kipindi kile upo na Symbian, Blackberry OS na windows phone. Unaona kuna utofauti mkubwa sana.
 
Kwenye masuala kama haya mbona wachina hawapo? Nilikuwa nategemea wachina watakuja na AI yao.
Nilitegemea pia wachina watakuja na OS yao ambayo itakuwa shindani kwenye Windows computer, Android na IOS?
Kipindi kile upo na Symbian, Blackberry OS na windows phone. Unaona kuna utofauti mkubwa sana.
OS ya kwenye computer Wachina wanayo Kylin Linux

Kwenye AI wapo China ni ya pili duniani baada ya US
 
OS ya kwenye computer Wachina wanayo Kylin Linux

Kwenye AI wapo China ni ya pili duniani baada ya US
Linux, computer operating system created in the early 1990s by Finnish software engineer Linus Torvalds and the Free Software Foundation (FSF). While still a student at the University of Helsinki, Torvalds started developing Linux to create a system similar to MINIX, a UNIX operating system.
Kylin Linux ni copy ya linux, ni sawa na uchukue Windows ya Microsoft, uongeze feature yako halafu useme ni OS yako.
*Nataka aliyotengeneza mchina mwenyewe bila ya kucopy kwa mtu. Kama umeshawahi kutumia Symbian, Blackberry OS, Windows phone, Android na IOS.
 
Linux, computer operating system created in the early 1990s by Finnish software engineer Linus Torvalds and the Free Software Foundation (FSF). While still a student at the University of Helsinki, Torvalds started developing Linux to create a system similar to MINIX, a UNIX operating system.
Kylin Linux ni copy ya linux, ni sawa na uchukue Windows ya Microsoft, uongeze feature yako halafu useme ni OS yako.
*Nataka aliyotengeneza mchina mwenyewe bila ya kucopy kwa mtu. Kama umeshawahi kutumia Symbian, Blackberry OS, Windows phone, Android na IOS.
Tuko dunia ya innovation mkuu

Unewahi kutumia computer yenye OS ya Kylin?

Kylin wana int'l intellectual property rights nothing copied from Linux

Kylin ilitengenezwa na China National University of Defense Technology
 
Back
Top Bottom