Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
AKILI INAPOKATAA KUAMINI NA KUUKUBALI UKWELI
Kaniandikia:
"MMS kila mara unapoandika UISLAM ndipo unapochefua watu.
Ubongo wako umekataa kulikubali hilo, nami nakuacha kama ulivyo.
Lakini ujue unakera sana. Mimi ni mmoja wa wengi tunaopenda kusoma maandiko yako lakini hata para ya 1 nikiona tu mambo ya uislam naacha. Siendelei kusoma.
Tupo wengi wa aina yangu."
Nami nikampa jibu langu:
"Sishangai hilo kwani lipo siku zote wala wewe si wa kwanza.
Soma kitabu cha Historia ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni (1977)kitakufurahisha.
Historia yote ya mchango wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika ilifutwa.
Lakini mimi waasisi wa harakati za uhuru ni wazee wangu na nikiijua historia hii na nilitambua kwa nini imefutwa.
Nimeiandika historia hii na sasa ni sehemu muhimu sana ya historia ya Tanganyika na Afrika kwa ujumla.
(Historia hii sasa ipo katika Dictionary of African Biography (DAB) toka mwaka wa 2011).
Halikadhalika ni sehemu ya historia ya Julius Nyerere awe amependa au hakupenda kwani hiyo ndiyo historia yake.
Vipi ubongo wangu ukatae historia yangu kwani huko ni mimi kujichukia.
Unadhani mimi natishika kwa wewe kusema ati mko wengi hamnisomi?
Kama wewe unavyoudhika na kusoma historia ya Waislam katika kupambana na dhulma ya ukoloni ndivyo mimi ninavyo tafakhar yaani kujifaharisha na historia ya jamii ninayotoka.
Babu yangu Salum Abdallah ni mmoja wa hawa wazalendo walipigania uhuru wa nchi hii.
Wala siwadharau wale ambao wazee wao hawakuwapo katika harakati hizi.
Isingewezekana wote wawepo.
Kama wapo wanaochefuka kama wewe basi jua pia wapo wanaopendezwa na historia hii.
Wewe unaacha kusoma kisa huipendi historia hii.
Historia ya Waislam inakuchefua.
Wako wanaoipenda historia hii na ndiyo kisa kitabu kimechapwa mara nne toka kitoke mara ya kwanza kwa Kiingereza mwaka wa 1998.
Kitabu kimependwa kwa kuwa nimeandika historia ya kweli si ile iliyowanyanyapaa wazalendo wakubwa waliounda AA na TANU wakapigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana 1961 kisa ni Waislam.
Huna sababu ya kuitesa nafsi yako uko huru kuni block."
Akanijibu:
"Mimi vitu vilivyojaa UISLAM usisumbuke kunitumia, huwa sivisomagi.
Uwe na siku njema, KK."
Kaniandikia:
"MMS kila mara unapoandika UISLAM ndipo unapochefua watu.
Ubongo wako umekataa kulikubali hilo, nami nakuacha kama ulivyo.
Lakini ujue unakera sana. Mimi ni mmoja wa wengi tunaopenda kusoma maandiko yako lakini hata para ya 1 nikiona tu mambo ya uislam naacha. Siendelei kusoma.
Tupo wengi wa aina yangu."
Nami nikampa jibu langu:
"Sishangai hilo kwani lipo siku zote wala wewe si wa kwanza.
Soma kitabu cha Historia ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni (1977)kitakufurahisha.
Historia yote ya mchango wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika ilifutwa.
Lakini mimi waasisi wa harakati za uhuru ni wazee wangu na nikiijua historia hii na nilitambua kwa nini imefutwa.
Nimeiandika historia hii na sasa ni sehemu muhimu sana ya historia ya Tanganyika na Afrika kwa ujumla.
(Historia hii sasa ipo katika Dictionary of African Biography (DAB) toka mwaka wa 2011).
Halikadhalika ni sehemu ya historia ya Julius Nyerere awe amependa au hakupenda kwani hiyo ndiyo historia yake.
Vipi ubongo wangu ukatae historia yangu kwani huko ni mimi kujichukia.
Unadhani mimi natishika kwa wewe kusema ati mko wengi hamnisomi?
Kama wewe unavyoudhika na kusoma historia ya Waislam katika kupambana na dhulma ya ukoloni ndivyo mimi ninavyo tafakhar yaani kujifaharisha na historia ya jamii ninayotoka.
Babu yangu Salum Abdallah ni mmoja wa hawa wazalendo walipigania uhuru wa nchi hii.
Wala siwadharau wale ambao wazee wao hawakuwapo katika harakati hizi.
Isingewezekana wote wawepo.
Kama wapo wanaochefuka kama wewe basi jua pia wapo wanaopendezwa na historia hii.
Wewe unaacha kusoma kisa huipendi historia hii.
Historia ya Waislam inakuchefua.
Wako wanaoipenda historia hii na ndiyo kisa kitabu kimechapwa mara nne toka kitoke mara ya kwanza kwa Kiingereza mwaka wa 1998.
Kitabu kimependwa kwa kuwa nimeandika historia ya kweli si ile iliyowanyanyapaa wazalendo wakubwa waliounda AA na TANU wakapigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana 1961 kisa ni Waislam.
Huna sababu ya kuitesa nafsi yako uko huru kuni block."
Akanijibu:
"Mimi vitu vilivyojaa UISLAM usisumbuke kunitumia, huwa sivisomagi.
Uwe na siku njema, KK."