Ndege aliye mtini, hawezi kamwe kulia,
Labda aliye shimoni, hewa imempelea.
Hivi ni sababu gani, machozi hawezi toa?
Ndege aliye mtini, kamwe hawezi kulia.
Wakiiji zangu salamu,nikushukuru kwa hili
Nami nishike yangu kalamu, niseme moja mawili
Umesema yalo adimu, yenye mwanga kandili
Milio mingine feki, usivutike sauti
Kuna videge vizushi,kama kunguru mwangapwani
Vyashika wako utashi, Kwa milio vikighani
Sauti zao chekeshi,weza hisi umewini
Mioyo yao beleshi,utachotwa masikini.
Kuna vingine vidogo, vyafanana na shomoro
Vyapatikana ugogo, sauti zao si kero
Ila vipe tu kisogo, vyatunguliwa kwa jero
Hivi angalau kidogo, Anajua kaka Melo
Na kuna makorobindo, ya zamani sio leo
Sauti zao kishindo, yamekwepa makombeo
Manati kwao msondo, labda uje na komeo
Niliyaona Kibondo, kwa kaka Batolomeo
Duh! Kuna vichokoriko,Hivi kula kwangu mwiko
Vinalia dikodiko, Lakini,mmh! mevipiga kiwiko
Tatizo lao chereko,shebedua na vicheko
Hawa kwangu mwiko!
Kuna ndege sisubiri, alie wala acheke
Mhozo-habeshi nikiri, huyu hana makeke
Kazidi makhirikhiri,machejo na pozi zake.
Huyu mtini simtungui, Nampandia namchukua!!
Asante Mzee kwa vitu adimu hivi!Wazushi waniwangia, ndege kunifukuzia,
Hakika nawaambia, wangu namng'ang'ania,
Kamwe hawatopatia, watabaki angalia,
Ndege amekwishalia, mwajua kitofatia!
Kutunguliwa.
MMM
Watani habari gani, nawasalimu jamani,
Kumi na moja i ndani, nakuja na hizi ghani,
Limenijia kichwani, wazo hili si utani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijelengesha tungua!
Nimemuona mtini, ndege kweli chakarani,
Ana mbwembwe kama nini, na rangirangi mbawani,
Sijui ni wa Kingoni, Anaimba kama nini,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, chukua
Kafumba macho tawini, na kawimbo mdomoni,
Ndege wenzake mtini, wamenyamaza kwa soni,
Anabadilisha tyuni, kama kasomea fani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha pasua
Mwindaji akaja chini, na manati mkononi,
Kaangalia mtini, achague ndege gani,
Mwenye kelele mtini, akamlenga jamani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, kamua
Mara Puh! Ndege chini, wenzake wako angani!
Kisu kikambusu shingoni, kisiwe kibudu jamani,
Kanyonyolewa majini, akatundikwa motoni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha nyanyua!
Ndipo nikaja amini, chunguza kwanza mtini,
Yule anojiamini, huimba sana tawini,
Ni kitoweo mtani, cha maakuli jioni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha tumbua!
Na. M. M. Mwanakijiji (BGM) – Sauti ya Kijiji
Ujumbe umefika mheshimiwa saana
mi nitakamua tu akijirengesha
Wazushi waniwangia, ndege kunifukuzia,
Hakika nawaambia, wangu namng'ang'ania,
Kamwe hawatopatia, watabaki angalia,
Ndege amekwishalia, mwajua kitofatia!
Kutunguliwa.
MMM
huku kwetu uswahilini, hata ndege hakuna
tumezungukwa na nyani, na ngedere wengi sana
tena tupo hatarini , kifo lini? tunaulizana
ndege alie mtini , ni ndoto kwetu kuona.
udenda umenitoka, kusoma hili shairi
ndege wa kusadikika, moyoni ameshamiri
mengi nimelazimika, akilini kufikiri
lini mimi nitamshika, nipate nijivinjari.
mnasema analia, natamani lake chozi
wengine wamebishia, kulia katu hawezi
vyovyote itavyokuaa, kuvumilia siwezi
kuhama nimeamua, naenda hamia mbezi
ndege nipate tungua, kwa manjonjo na mapozi.
ni mimi malenga wenu klorokwini a.k.a mshamba mstaarabu
Ewe kidonge mwenzangu, kumbe nawe uko ndani,
Napata kizunguzungu, umenigusa moyoni,
Ndege wa kwenu kimbungu, leo wamkataani?
Ndege huyu ndege wetu, kila shemu huishi
Labda kama baharini, kusipokuwa na miti,
Huko hakuwezekani, asijepata mititi,
Hamia kwetu nyumbani, nitakupatia hati,
Nitakupatia hati, ndege umuweke ndani.
Watani habari gani, nawasalimu jamani,
Kumi na moja i ndani, nakuja na hizi ghani,
Limenijia kichwani, wazo hili si utani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijelengesha tungua!
Nimemuona mtini, ndege kweli chakarani,
Ana mbwembwe kama nini, na rangirangi mbawani,
Sijui ni wa Kingoni, Anaimba kama nini,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, chukua
Kafumba macho tawini, na kawimbo mdomoni,
Ndege wenzake mtini, wamenyamaza kwa soni,
Anabadilisha tyuni, kama kasomea fani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha pasua
Mwindaji akaja chini, na manati mkononi,
Kaangalia mtini, achague ndege gani,
Mwenye kelele mtini, akamlenga jamani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, kamua
Mara Puh! Ndege chini, wenzake wako angani!
Kisu kikambusu shingoni, kisiwe kibudu jamani,
Kanyonyolewa majini, akatundikwa motoni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha nyanyua!
Ndipo nikaja amini, chunguza kwanza mtini,
Yule anojiamini, huimba sana tawini,
Ni kitoweo mtani, cha maakuli jioni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha tumbua!
Na. M. M. Mwanakijiji (BGM) Sauti ya Kijiji
duh! Imetulia mbayaaa
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Ndio hapa mnambie, kwa nini wampakata?
Tena nidadavulie, ni raha gani wapata?
Ili nami nikimbie, nimsake huyo bata,
Nawauliza malenga, bata anapakatwaje?
Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
'Mesikia nimeona, bata yake kuharisha,
Wala sio kunong'ona, hilo usije kubisha
Kumpakata mi naona, hilo jambo la kutisha,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Domo lake lachokoa, vinyesi na konokono,
Alacho ndio atoa, kwani nimpe mkono?
Usije kunizodoa, haya yangu ni maono,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)
Pope at his best,,kumbe ndo maana ulikuwa huji mlimani!