hahaha babe kuna watu wanataka kumpakata bata!
hahaha,,nimeona love nikawa puzzled lkn asante kwa kuniwakilishia maswali yangu wacha nisubiri majibu,,lol
BABU NAOMBA CHANGIA,kwenye hili umenigusa
KWENYE HII TASINIA,hakika umebobea
KWAKO SIFA NAZIMWAGA,hakika umebobea
ANGALIZO WAZI NAWEKA,wiselady uniachie
KAMA LOVE NI KUSAFA,walau sasa nitulie
BABU HUYO MTU ACHA,tena usichakachue
ANGALIZO NAWEKA WAZI,wiselady uniachie
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Ndio hapa mnambie, kwa nini wampakata?
Tena nidadavulie, ni raha gani wapata?
Ili nami nikimbie, nimsake huyo bata,
Nawauliza malenga, bata anapakatwaje?
Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
'Mesikia nimeona, bata yake kuharisha,
Wala sio kunong'ona, hilo usije kubisha
Kumpakata mi naona, hilo jambo la kutisha,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Domo lake lachokoa, vinyesi na konokono,
Alacho ndio atoa, kwani nimpe mkono?
Usije kunizodoa, haya yangu ni maono,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)
umenena kaizeri , nadhani hukukosea
hata namimi nakiri, bata hana mazoea
ni mchafu sio siri, tena sio maridhia
kunataka ujasiri , kumpakata sawia
tokea tangu na tangu, bata hulazwa bandani
iweje magulumangu, amuweke mapajani?
naona kizunguzungu, jibu sipati jamani
naapa haki ya mungu, sitojaribu maishani
bata akiwa sokoni , kwa nje anavutia
kama hukuwa makini, waweza kumrukia
mpeleke kwako uwani, hapo utajionea
atakushusha thamani, nyumba ataichafua
chakula alacho bata, pia ni cha kuzingatia
humeza anachopata, usaha hata mafua
iweje kumpakata , hamuogopi churua?
wengi walompakata, hivi sasa waugua.
kalamu naiangusha, nafasi ninaitoa
kama unaweza bisha, shairi nilolitoa
wamalenga mnatisha, kijasho mnanitoa
bata mwampakatisha, kinyume na mazowea
na klorokwini a.k.a malenga bubu.
pia mimi sikudhani, uwanja huu ni wako
na sasa nimeamini, hii pia fani yako
aspirini, klorokwini, hii dozi ni kiboko
mwanakijiji haamini, tunavyotoa milipuko.
huyo ndege unaesema, tayari nimemuona,
mwili umenitetema , leo nimeita jana
kumpata ni lazima , iwe usiku au mchana
nitamla mzima mzima, tena kwa kumtafuna.
naipanga mikakati, na mitego ya kileo
naitengeza manati, gobole pia koleo
nitamtungulia kati, apapatike na kilio
nikamle kwa chapati, nimfanye kitoweo
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?
Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)
Mhhhhhhhhhh imekaaa njema sanaWatani habari gani, nawasalimu jamani,
Kumi na moja i ndani, nakuja na hizi ghani,
Limenijia kichwani, wazo hili si utani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijelengesha tungua!
Nimemuona mtini, ndege kweli chakarani,
Ana mbwembwe kama nini, na rangirangi mbawani,
Sijui ni wa Kingoni, Anaimba kama nini,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, chukua
Kafumba macho tawini, na kawimbo mdomoni,
Ndege wenzake mtini, wamenyamaza kwa soni,
Anabadilisha tyuni, kama kasomea fani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha pasua
Mwindaji akaja chini, na manati mkononi,
Kaangalia mtini, achague ndege gani,
Mwenye kelele mtini, akamlenga jamani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, kamua
Mara Puh! Ndege chini, wenzake wako angani!
Kisu kikambusu shingoni, kisiwe kibudu jamani,
Kanyonyolewa majini, akatundikwa motoni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha nyanyua!
Ndipo nikaja amini, chunguza kwanza mtini,
Yule anojiamini, huimba sana tawini,
Ni kitoweo mtani, cha maakuli jioni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha tumbua!
Na. M. M. Mwanakijiji (BGM) Sauti ya Kijiji
Wakiiji zangu salamu,nikushukuru kwa hili
Nami nishike yangu kalamu, niseme moja mawili
Umesema yalo adimu, yenye mwanga kandili
Milio mingine feki, usivutike sauti
Kuna videge vizushi,kama kunguru mwangapwani
Vyashika wako utashi, Kwa milio vikighani
Sauti zao chekeshi,weza hisi umewini
Mioyo yao beleshi,utachotwa masikini.
Kuna vingine vidogo, vyafanana na shomoro
Vyapatikana ugogo, sauti zao si kero
Ila vipe tu kisogo, vyatunguliwa kwa jero
Hivi angalau kidogo, Anajua kaka Melo
Na kuna makorobindo, ya zamani sio leo
Sauti zao kishindo, yamekwepa makombeo
Manati kwao msondo, labda uje na komeo
Niliyaona Kibondo, kwa kaka Batolomeo
Duh! Kuna vichokoriko,Hivi kula kwangu mwiko
Vinalia dikodiko, Lakini,mmh! mevipiga kiwiko
Tatizo lao chereko,shebedua na vicheko
Hawa kwangu mwiko!
Kuna ndege sisubiri, alie wala acheke
Mhozo-habeshi nikiri, huyu hana makeke
Kazidi makhirikhiri,machejo na pozi zake.
Huyu mtini simtungui, Nampandia namchukua!!
huku kwetu uswahilini, hata ndege hakuna
tumezungukwa na nyani, na ngedere wengi sana
tena tupo hatarini , kifo lini? tunaulizana
ndege alie mtini , ni ndoto kwetu kuona.
udenda umenitoka, kusoma hili shairi
ndege wa kusadikika, moyoni ameshamiri
mengi nimelazimika, akilini kufikiri
lini mimi nitamshika, nipate nijivinjari.
mnasema analia, natamani lake chozi
wengine wamebishia, kulia katu hawezi
vyovyote itavyokuaa, kuvumilia siwezi
kuhama nimeamua, naenda hamia mbezi
ndege nipate tungua, kwa manjonjo na mapozi.
ni mimi malenga wenu klorokwini a.k.a mshamba mstaarabu
Klorokwini ndugu yangu, nakupa zangu hongera,
Kumpata ndege wangu, hukuwa nazo papara,
Usimle wanguwangu, usijepata kuhara,
Ndege huyu ndege wangu, ni ndege aso hiyana
Ndege huyu aimbaye, siyo siyo kama anolia,
Kwa upole amwindaye, mtini atatulia,
Kwa papara afanyaye, ndege wangu takimbia,
Ndege huyu ndege wangu, ni ndege aso hiyana.
Aspirini aksante, kutuliza yangu hofu
Bado kidogo nidate, nikupe wangu mnofu
Kiuno litaka nikate, vina vilonitia upofu
Mh kweli u malenga mzuri Asprini
Mwanakijiji kumbuka, ndege makazi yake mtini
mwindaji yake hulka, kumtibua usingizi
Ukicheza ataruka, kutafuta jema zizi
Kwanini kumtioungua, ngemuacha singelia
moja mbili nimerudi , hapa tena uwanjani
ewe jibaba la wodi , ya wazazi, aspirini
nimeanza kumfaidi, ndege alie mtini
kurejea sina budi , kuwapeni shukurani.
ndege niliempata, hakuwa tawi la chini
tamaa sikuikata , moyoni nilijiamini
mitego nikatafuta,nikaiweka begani
polepole sikusita , nikaingia kazini.
simalizi sifa zake , musije mukaniloga
nyembamba sauti yake, akiimba hana woga
ni kijani kope zake , anang'ara bila kukoga
ni njema tabia zake, hapendi kula mizoga.
kwasasa natua hapa, nimefika kituoni
inanibidi kusepa , nirejee nyumbani
ni wakati wa kumpa, chakula ndege tunduni
kazi kwenu vidampa, mlofeli mawindoni.