Akilia sana, karibu kutunguliwa...!

Akilia sana, karibu kutunguliwa...!

BABU NAOMBA CHANGIA,kwenye hili umenigusa
KWENYE HII TASINIA,hakika umebobea
KWAKO SIFA NAZIMWAGA,hakika umebobea

ANGALIZO WAZI NAWEKA,wiselady uniachie
KAMA LOVE NI KUSAFA,walau sasa nitulie
BABU HUYO MTU ACHA,tena usichakachue
ANGALIZO NAWEKA WAZI,wiselady uniachie

huyo ndo TEAMO sasa....
 
Kwani ana rangi gani, hebu nijuzeni
Yupo yule wa kijani, anaringa mtini
kwa madaha anaghani, tena kama hayawani
Pretta nitoe gizani, kama umeme wa dowani
 
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Ndio hapa mnambie, kwa nini wampakata?
Tena nidadavulie, ni raha gani wapata?
Ili nami nikimbie, nimsake huyo bata,
Nawauliza malenga, bata anapakatwaje?

Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

'Mesikia nimeona, bata yake kuharisha,
Wala sio kunong'ona, hilo usije kubisha
Kumpakata mi naona, hilo jambo la kutisha,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Domo lake lachokoa, vinyesi na konokono,
Alacho ndio atoa, kwani nimpe mkono?
Usije kunizodoa, haya yangu ni maono,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?

Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)

umenena kaizeri , nadhani hukukosea
hata namimi nakiri, bata hana mazoea
ni mchafu sio siri, tena sio maridhia
kunataka ujasiri , kumpakata sawia

tokea tangu na tangu, bata hulazwa bandani
iweje magulumangu, amuweke mapajani?
naona kizunguzungu, jibu sipati jamani
naapa haki ya mungu, sitojaribu maishani

bata akiwa sokoni , kwa nje anavutia
kama hukuwa makini, waweza kumrukia
mpeleke kwako uwani, hapo utajionea
atakushusha thamani, nyumba ataichafua

chakula alacho bata, pia ni cha kuzingatia
humeza anachopata, usaha hata mafua
iweje kumpakata , hamuogopi churua?
wengi walompakata, hivi sasa waugua.


kalamu naiangusha, nafasi ninaitoa
kama unaweza bisha, shairi nilolitoa
wamalenga mnatisha, kijasho mnanitoa
bata mwampakatisha, kinyume na mazowea


na klorokwini a.k.a malenga bubu.
 
umenena kaizeri , nadhani hukukosea
hata namimi nakiri, bata hana mazoea
ni mchafu sio siri, tena sio maridhia
kunataka ujasiri , kumpakata sawia

tokea tangu na tangu, bata hulazwa bandani
iweje magulumangu, amuweke mapajani?
naona kizunguzungu, jibu sipati jamani
naapa haki ya mungu, sitojaribu maishani

bata akiwa sokoni , kwa nje anavutia
kama hukuwa makini, waweza kumrukia
mpeleke kwako uwani, hapo utajionea
atakushusha thamani, nyumba ataichafua

chakula alacho bata, pia ni cha kuzingatia
humeza anachopata, usaha hata mafua
iweje kumpakata , hamuogopi churua?
wengi walompakata, hivi sasa waugua.


kalamu naiangusha, nafasi ninaitoa
kama unaweza bisha, shairi nilolitoa
wamalenga mnatisha, kijasho mnanitoa
bata mwampakatisha, kinyume na mazowea


na klorokwini a.k.a malenga bubu.


huyo ndo klorokwini sasa....,malenga bubu lakini hapo naona umesema! hahaha so entertaining!
 
mwanakijiji hivi ni wewe hua unaandika makala katika gazeti fulani hapa nchini?
 
pia mimi sikudhani, uwanja huu ni wako
na sasa nimeamini, hii pia fani yako
aspirini, klorokwini, hii dozi ni kiboko
mwanakijiji haamini, tunavyotoa milipuko.

huyo ndege unaesema, tayari nimemuona,
mwili umenitetema , leo nimeita jana
kumpata ni lazima , iwe usiku au mchana
nitamla mzima mzima, tena kwa kumtafuna.

naipanga mikakati, na mitego ya kileo
naitengeza manati, gobole pia koleo
nitamtungulia kati, apapatike na kilio
nikamle kwa chapati, nimfanye kitoweo

Klorokwini ndugu yangu, nakupa zangu hongera,
Kumpata ndege wangu, hukuwa nazo papara,
Usimle wanguwangu, usijepata kuhara,
Ndege huyu ndege wangu, ni ndege aso hiyana

Ndege huyu aimbaye, siyo siyo kama anolia,
Kwa upole amwindaye, mtini atatulia,
Kwa papara afanyaye, ndege wangu takimbia,
Ndege huyu ndege wangu, ni ndege aso hiyana.
 
Nilikuwa ninawaza, kalamu nisiishike,
Nikae kwenye baraza, moja mbili nisishike,
Maguluma kanikwaza, ngoja mic niishike
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?


Hommie wangu 'Sipirini, hata nawe Klorokwini,
Mwanakijiji Amani, Magulumangu mwiteni,
Aje hapa barazani, aujibu mtihani,
Bata anapakatwaje, nawauliza malenga?


Na Kaizer K. Kaizer (Sauti ya watu)

Homi wangu homu boi, Ndege gani wasemea?
Ndege mtini hakai, bata huyo wasemea,
Bata hakika hafai, mtini hawezi kaa,
Ndege mkaa mtini, ndio hoja simamia.

Bata zake ni bandani, nchi kavu mwakemwake,
Jifarakua majini, uchafu ni ndugu yake,
Akienda msalani, uharo ni fani yake,
Kumkumbatia bata, Ni fani ya wachafuzi.
 
Akijelengesha tungua

Ndege ajilengeshe, nasema usimtungue,
Raha ya ndege abishe, umsake akimbie,
Kimtego utegeshe, ndaniye aingie,
Heri ndege asumbue, nami nijibidishe.

Akijilengesha, chukua

Ndege ajilengeshe, kibudu usichukue,
Kwa nini ajileweshe, ni wa mdondo ujue,
Ndege raha kasheshe, kwata akuchezee,
Heri ndege asumbue, nami nijibidishe,

Akijilengesha pasua

Ndege ajilengeshe, si vema umpasue,
Ndege raha msemeshe, nyimboze zikuingie,
Hata chambo umlishe, ulimbo umnasie,
Heri ndege asumbue, nami nijibidishe,

Akijilengesha, kamua

Ndege ajilengeshe, kataa usikamue,
Ni usaha umuoshe, angani umuachie,
Nakuonya usibishe, ni kwani ndege asinzie?
Heri ndege asumbue, nami nijibidishe,

Akijilengesha nyanyua!

Ndege ajilengeshe, uvundo usinyanyue,
Mbali msafirishe, na huko akaozee,
Mke usimjulishe, itabidi azomee,
Heri ndege asumbue, nami nijibidishe,

Akijilengesha tumbua!

Ndege ajilengeshe, rafiki usitumbue,
Kaditama na yaishe, ndege raha asumbue,
Mpinzani na abishe, vya mdondo atumbue,
Heri ndege asumbue, nami nijibidishe,
 
Watani habari gani, nawasalimu jamani,
Kumi na moja i ndani, nakuja na hizi ghani,
Limenijia kichwani, wazo hili si utani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijelengesha tungua!

Nimemuona mtini, ndege kweli chakarani,
Ana mbwembwe kama nini, na rangirangi mbawani,
Sijui ni wa Kingoni, Anaimba kama nini,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, chukua

Kafumba macho tawini, na kawimbo mdomoni,
Ndege wenzake mtini, wamenyamaza kwa soni,
Anabadilisha tyuni, kama kasomea fani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha pasua

Mwindaji akaja chini, na manati mkononi,
Kaangalia mtini, achague ndege gani,
Mwenye kelele mtini, akamlenga jamani,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha, kamua

Mara Puh! Ndege chini, wenzake wako angani!
Kisu kikambusu shingoni, kisiwe kibudu jamani,
Kanyonyolewa majini, akatundikwa motoni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha nyanyua!

Ndipo nikaja amini, chunguza kwanza mtini,
Yule anojiamini, huimba sana tawini,
Ni kitoweo mtani, cha maakuli jioni,
Ndege akilia sana, karibu kutunguliwa!
Akijilengesha tumbua!

Na. M. M. Mwanakijiji (BGM) – Sauti ya Kijiji
Mhhhhhhhhhh imekaaa njema sana
 
Daah.. nyie jamaa wabaya sana! Hongereni sana kwa kuonesha wenu weledi kwenye tasnia ya ushairi.Ntarudi nimjibu Kaizer na maswali yake kwa Al-Batat.
 
Aspirini aksante, kutuliza yangu hofu
Bado kidogo nidate, nikupe wangu mnofu
Kiuno litaka nikate, vina vilonitia upofu
Mh kweli u malenga mzuri Asprini

Mwanakijiji kumbuka, ndege makazi yake mtini
mwindaji yake hulka, kumtibua usingizi
Ukicheza ataruka, kutafuta jema zizi
Kwanini kumtioungua, ngemuacha singelia
 
Shukurani za dhati ziwaendee MMM, Teamo, AmaniGK, Klorokwini na Asprin, haki ya nani nimedownload thread nzima kwa kumbukumbu zangu binafsi!

Once again wapwaz na mabinamz mmeprove kuwa JF ni KISIMA KIREFU kilichojaa Hekima!

Asanteni sana na endeleeni kutufunza!
 
huyu ndege atakuwa kunguru wa zenji.
akijilengesha chakachuwa pwaaaa!!!!!!:A S kiss:
 
hahahahahaa unampandia unamchukua eee???
du humu leo kuna mambo nimependa sana
Wakiiji zangu salamu,nikushukuru kwa hili
Nami nishike yangu kalamu, niseme moja mawili
Umesema yalo adimu, yenye mwanga kandili
Milio mingine feki, usivutike sauti

Kuna videge vizushi,kama kunguru mwangapwani
Vyashika wako utashi, Kwa milio vikighani
Sauti zao chekeshi,weza hisi umewini
Mioyo yao beleshi,utachotwa masikini.

Kuna vingine vidogo, vyafanana na shomoro
Vyapatikana ugogo, sauti zao si kero
Ila vipe tu kisogo, vyatunguliwa kwa jero
Hivi angalau kidogo, Anajua kaka Melo


Na kuna makorobindo, ya zamani sio leo
Sauti zao kishindo, yamekwepa makombeo
Manati kwao msondo, labda uje na komeo
Niliyaona Kibondo, kwa kaka Batolomeo


Duh! Kuna vichokoriko,Hivi kula kwangu mwiko
Vinalia dikodiko, Lakini,mmh! mevipiga kiwiko
Tatizo lao chereko,shebedua na vicheko
Hawa kwangu mwiko!

Kuna ndege sisubiri, alie wala acheke
Mhozo-habeshi nikiri, huyu hana makeke
Kazidi makhirikhiri,machejo na pozi zake.
Huyu mtini simtungui, Nampandia namchukua!!
 
huku kwetu beach labda mapapa na manyangumi
huku kwetu uswahilini, hata ndege hakuna
tumezungukwa na nyani, na ngedere wengi sana
tena tupo hatarini , kifo lini? tunaulizana
ndege alie mtini , ni ndoto kwetu kuona.

udenda umenitoka, kusoma hili shairi
ndege wa kusadikika, moyoni ameshamiri
mengi nimelazimika, akilini kufikiri
lini mimi nitamshika, nipate nijivinjari.

mnasema analia, natamani lake chozi
wengine wamebishia, kulia katu hawezi
vyovyote itavyokuaa, kuvumilia siwezi
kuhama nimeamua, naenda hamia mbezi
ndege nipate tungua, kwa manjonjo na mapozi.




ni mimi malenga wenu klorokwini a.k.a mshamba mstaarabu
 
Klorokwini ndugu yangu, nakupa zangu hongera,
Kumpata ndege wangu, hukuwa nazo papara,
Usimle wanguwangu, usijepata kuhara,
Ndege huyu ndege wangu, ni ndege aso hiyana

Ndege huyu aimbaye, siyo siyo kama anolia,
Kwa upole amwindaye, mtini atatulia,
Kwa papara afanyaye, ndege wangu takimbia,
Ndege huyu ndege wangu, ni ndege aso hiyana.

moja mbili nimerudi , hapa tena uwanjani
ewe jibaba la wodi , ya wazazi, aspirini
nimeanza kumfaidi, ndege alie mtini
kurejea sina budi , kuwapeni shukurani.

ndege niliempata, hakuwa tawi la chini
tamaa sikuikata , moyoni nilijiamini
mitego nikatafuta,nikaiweka begani
polepole sikusita , nikaingia kazini.

sikutumia manati, nilihofia madhara
nilikitega kijiti , akaja bila papara
alishuka kwenye mti, akaishiwa na sera
sasa nimemdhibiti , hakuna wa kunikera

rangi yake ni smati, weusi wa kahawia
ana doa kati kati , jekundu linavutia
na tena kila wakati, huwa ananiimbia
nimeshaandika hati,hakuna wa kuniibia.

nilimshika mkia , sauti akalegeza
pumzi zikanishia, ghafula nikateleza
macho ya kusinzia, hakika kanimaliza
ndege huyu maridhia, amejaa miujiza

simalizi sifa zake , musije mukaniloga
nyembamba sauti yake, akiimba hana woga
ni kijani kope zake , anang'ara bila kukoga
ni njema tabia zake, hapendi kula mizoga.

kwasasa natua hapa, nimefika kituoni
inanibidi kusepa , nirejee nyumbani
ni wakati wa kumpa, chakula ndege tunduni
kazi kwenu vidampa, mlofeli mawindoni.
 
Aspirini aksante, kutuliza yangu hofu
Bado kidogo nidate, nikupe wangu mnofu
Kiuno litaka nikate, vina vilonitia upofu
Mh kweli u malenga mzuri Asprini

Mwanakijiji kumbuka, ndege makazi yake mtini
mwindaji yake hulka, kumtibua usingizi
Ukicheza ataruka, kutafuta jema zizi
Kwanini kumtioungua, ngemuacha singelia

Mjukuu orijino, Sante kunifagilia,
Nitanenepa unono, kwa sifa ulonigea,
babu kwa hayo maneno, bichwa limejivimbia,
Ahsante kwa ufagio, Babu raha nasikia.
 
moja mbili nimerudi , hapa tena uwanjani
ewe jibaba la wodi , ya wazazi, aspirini
nimeanza kumfaidi, ndege alie mtini
kurejea sina budi , kuwapeni shukurani.

ndege niliempata, hakuwa tawi la chini
tamaa sikuikata , moyoni nilijiamini
mitego nikatafuta,nikaiweka begani
polepole sikusita , nikaingia kazini.


simalizi sifa zake , musije mukaniloga
nyembamba sauti yake, akiimba hana woga
ni kijani kope zake , anang'ara bila kukoga
ni njema tabia zake, hapendi kula mizoga.

kwasasa natua hapa, nimefika kituoni
inanibidi kusepa , nirejee nyumbani
ni wakati wa kumpa, chakula ndege tunduni
kazi kwenu vidampa, mlofeli mawindoni.

Ndugu yangu klorokwini, ndege ulojipatia,
Usimtupe shimoni, ndege asije kulia,
Ahsante kwa shukurani, sisi ni ndugu sawia,
Ila usije sahau, zuri kula na nduguyo.

Ndege huyo maridadi, kama ulivomsifu,
Asipigwe na baridi, wala kung'atwa siafu,
Kumtuna huna budi, Asije kupata ufu,
Msiba wake mkubwa, kufiwa na ndege wako.

Kaa naye kwa makini, haja kumtimizia,
Asijeshinda bandani, njaa kumuumizia,
Chakula alie ndani, siyo chini kumwekea,
Ndege akinona nona, ndo utamu utapata.
 
Back
Top Bottom