Al Masry vs Simba Sc kuonyeshwa na Tv hizi

Al Masry vs Simba Sc kuonyeshwa na Tv hizi

[emoji16] [emoji16] mbona amna kitu aisee
Dakika ya 6 ya mchezo Al-Masry 0 - Simba 0 :
Vitu live kabisa YouTube(streaming) naona, Simba anacheza kama vile wanalinda ushindi huku Al-Masry wanashambulia kama mwaka mwenye kichaa kutafuta goli la ushindi mapema.

Source : ON sports
 
Yaani mpira anaoucheza Simba hauna tofauti alioucheza mwenzake Yanga,wachezaji hawajiamini ,wanapoteza mipira yaani hovyo kabisa waoga.
 
Dakika 7:
Juko Marshid anamfanyia foul Islam Issa wa Al-Masry katika pembe ya kushoto ya penalt box ya lango la Simba .

Adhabu inapigwa kwenda kwa Simba na inambabatiza mtu Shagari Kapombe na kutoka nje. Kapombe shuti kali linampata kichwani yupo chini akipata huduma ya kwanza. Simba kapona Sasa ni goli kiki .

Dakika ya 11:
Mchezaji wa Al-Masry an akaendelea chini na kugaaga, Dakika zinapita na benchi la Al- Masry wakaamua kufanya mabadiliko ya mchezaji.

Dakika 13:
Aristide Bancé anachukua nafasi ya mchezajI wa Al- Masry aliyeumia, uwanja unazizima kumshangilia nyota wao raia wa Burkina Faso.

Dakika 45:
Half time mapumziko Al-Masry 0 - Simba 0. Naona wachezaji wa Simba wakikumbatiana, kupongezana na kushukuru kumaliza ngwe ya kwanza ya mechi ya leo bila kuruhusu goli. Tutarudi tena JF kuendelea kuwapatia maendeleo ya mechi hii ya kufa au kupona Al-Masry vs Simba
. Tukirudi uwanjani tutajiunga moja kwa moja na mwana-JF aliyepo uwanjani Port Said, Misri Kunguru Mjanja aendelee na matangazo mubashara.
 
wabongo bana,huwa hamukubali kuzidiwa!!!!mkuu hapo mupo uarabuni mkuu au unafikir ni Mbeya mkicheza na Mbeya city?
Kuzidiwa tumezidiwa lkn ile mitaa ya kijani wanayommulika Manula inazingua ,kwani ww hauoni.
 
wabongo bana,huwa hamukubali kuzidiwa!!!!mkuu hapo mupo uarabuni mkuu au unafikir ni Mbeya mkicheza na Mbeya city?
Ni kweli Awa Watu Wanacheza Mpira wa Kasi Sana Yaani Simba Siwaoni Bocco ndo Simuoniii Kabisaaa.

Waarabu Awafai na Mola Anawaona Yaani

Wanacheza Mpira Kwa Njaaa ya Hatari Saana

Simba Mola Awasimamie InshaAllah.
 
Simba dakika izi za mwisho Mngezitumia Mngekuwa Wapi
 
Back
Top Bottom