Al Merrekh 0-0 Simba | Al Hilal Stadium | CAF

6 March 2021
Cairo, Egypt

AL AHLY WAKIELEKEA UWANJANI
Basi la Ahly likielekea Cairo stadium kukumbana na AS V.Club
Source : Al Ahly TV
 
Cairo Stadium

Dakika ya 10'
Toka uwanja huu wa kimataifa Al Ahly ndiyo inaonekana kukamia kutafuta matokeo chanya kujaribu kukusanya pointi zote 3

Al Ahly SC 0 - 0 AS Vita Club
 
Cairo Stadium

Dakika ya 10'
Toka uwanja huu wa kimataifa Al Ahly ndiyo inaonekana kukamia kutafuta matokeo chanya kujaribu kukusanya pointi zote 3
Al Ahly SC 0 - 0 AS Vita Club

As Vita hawezi chomoka hii game hata km wameroga
 
Dakika 25'

Al Ahly SC 0 - 0 AS Vita Club


Mayamba wa AS Vita ! Anakosa nafasi nzuri kabisa
 
Dakika 26'

Al Ahly SC 0 - 0 AS Vita Club
Walter Bwalya katika nafasi nzuri ndani ya box, anapiga mpira wa kichwa ! Mpira unapaa juu ya mwamba, nafasu nzuri Al Ahly kupata bao la kuongoza lakini inapotea.
 
Dakika 32'
fursa 2 nyingine ndani ya box lakini mipira yote ya Al Ahly inaokolewa na AS Vita Club toka mstari wa goli, kweli kuna mkono wa bwana unaisaidia hii timu ya Kinshasa DR Congo, Yaaani leo ni khatari ikiwa AS Vita watatoka salama hapa Cairo bila kubebeshwa zigo la magoli na Al Ahly
Al Ahly SC 0 - 0 AS Vita Club
 
Dakika 32'
fursa 2 nyingine ndani lakini mipira yote ya Al Ahly inaokolewa na AS Vita Club toka mstari wa goli, kweli kuna mkono wa bwana unaisaidia hii timu ya Kinshasa DR Congo
Al Ahly SC 0 - 0 AS Vita Club
Kama ilivyokuwa kwa Simba leo.
 
GOOOAAL !
Dakika 40'

Al Ahly SC 0 - 1 AS Vita Club

Timu nyingine ya Congo siyo Congo Brazaville, TP Mazembe Englebert timu maarufu ya DR Congo leo walipoteza 2-1 kwa Mamelodi Sundowns ya South Afrika.

Hapa Muyamba kwa shuki kali kabisa anawaduwaza Al Ahly kwa goal safi kabisa toka upande wa kulia nje kidogo ya box
 
Dakika 45'

Al Ahly SC 0 - 1 AS Vita Club

Helwaa kurupushani za juhudi za Al Ahly mpaka sasa zimeshindwa kufumania nyavu za AS Vita

Timu zinakwenda mapumbizo na super kocha Florent Ibenge wa AS Vita na wachezaji wake wanakwenda vyumbani wakiwa kifua mbele.

Wachezaji wa Ahly nao wanaenda mapumziko huku baadhi yao wakibusu pitch ya wanja hili la Cairo International stadium kutoa shukrani kwa Munyazi Mungu, baada ya kukoswa kufungwa bao lingine dakika hii ya 45' wakati Lolepo wa AS Vita akiwa uso kwa uso na kapteni wa Al Alhy golikipa Mohamed El-Shenawy mchezaji bora wa Al Ahly wa wiki hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…