Alaaniwe aliebomoa nyumba za watu na kuiba vitu vyao huko Mapinga Bagamoyo

wanasema.asiyesikia la mkuu uvunjika guu.walishaambiwa hayo maeneo ni uvamizi pale mingoi nyuma ya kiwanda cha rami lakn hawakusikia.haya ndo malipo yake.
 
wanasema.asiyesikia la mkuu uvunjika guu.walishaambiwa hayo maeneo ni uvamizi pale mingoi nyuma ya kiwanda cha rami lakn hawakusikia.haya ndo malipo yake.
Ndio hadi kuiba Mali zao Sasa?busara huepusha madhara,wangepewa muda wakuondoa Mali zao,wangeambulia bati na tofali kadhaa ,madirisha, materials za pesa mingi Sana Apo zimepotea
 
Hivi sheria inasemaje ikiwa mtu alipewa eneo na serikali ya kijiji/mji na hakufanya chochote kwa muda mrefu baadae serikali ya kijiji ikarudisha eneo kwa wananchi ndipo yule mwekezaji akajitokeza na kudai eneo baada ya kesi kwenda mahakamani yule mwekezaji akashindwa kesi lakini akawa bado anaenda kwenye maeneo yale kukagua mipaka hii imekaaje kisheria?
 
Watanganyika wanatesaka kati ardhi ya nchi yao....kuna mwisho, ipo siku.
Mambo mengine lazima tufuate haki za watu. Hapa hawa waliovunjiwa walivamia shamba la mtu wakaambiwa waondoke wakafanya jeuri hata hawakutaka majadiliano na mwenye shamba!! Sasa mahakama imeamua hawa wavamizi waondolewe shambani kwa mwenyewe maadam hawakutaka maelewano!!
Uvamizi Kama huu uko kwenye mashamba ya Watu mengi huko kuelekea seheme za Mapinga , hivyo nyumba nyingi zitavunjwa iwapo wavamizi hawatapata suluhu na wenye mashamba! Kumbuka haya mashamba yana TITLE DEEDS!
 
Hakikisha unanunua eneo ambalo, muuzaji anakuonyesha nyaraka zote muhimu hasa Hati miliki kutoka wizarani

Hayo mengine hayana maana yoyote coz serikali ya kijiji haina mamlaka ya kuweza kuthibitisha uhalali wa umiliki ,
 
Unakuja nyarakaz za serikali ya Kijiji,mwenzako anakuja na title deed.na risiti zote kila mwaka analipia ardhi yake,Nani atakua na nguvu?
 
No wonder Msemaji rasmi wa SMZ alionya kuhusu RAZABA!
 
Ungesema Mapinga ipi? Mwakibosha au sehemu gani mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…