ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 21,643
- 51,642
Albatrosi ni ndege wakubwa wa bahari katika familia Diomedeidae. spishi hizi za ndege wana mabawa marefu kabisa kuliko ndege wote duniani. Albatrosi ana mabawa ambayo mawili pamoja yana urefu wa sm 310 kwa wastani na urefu mkubwa kabisa uliopimwa ulikuwa sm 370. Rangi zao zinatofautiana kutoka nyeupe na mabawa kijivu hafifu hadi mwili wote kijivucheusi. Wana domo mkubwa sana wenye ncha. Mirija miwili ya pua inapitia pande zote mbili za domo.
Ndege hawa huenda mbali sana wakiruka angani na wanaweza kuzunguka dunia. Hawapigi mabawa sana baada ya kuruka, lakini wananyiririka kwa mabawa yaliyonyooshwa. Huwakamata ngisi, samaki na hula mizoga pia. Kwa kawaida albatrosi huyatengeneza makazi yao kwenye visiwa vya mbali visipokaa watu wala mamalia wengine. Jike hulitaga yai moja tu.huyu ndege hutumia maisha yake ya mwanzo ya miaka Sita kuruka bila kutua chini
Ndege hawa huenda mbali sana wakiruka angani na wanaweza kuzunguka dunia. Hawapigi mabawa sana baada ya kuruka, lakini wananyiririka kwa mabawa yaliyonyooshwa. Huwakamata ngisi, samaki na hula mizoga pia. Kwa kawaida albatrosi huyatengeneza makazi yao kwenye visiwa vya mbali visipokaa watu wala mamalia wengine. Jike hulitaga yai moja tu.huyu ndege hutumia maisha yake ya mwanzo ya miaka Sita kuruka bila kutua chini