Albert Chalamila atishia kumuweka ndani mkandarasi wa Mwendokasi

Albert Chalamila atishia kumuweka ndani mkandarasi wa Mwendokasi

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema haridhishwi na kasi ya ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka ya Gongo la Mboto na kama hali itaendelea hivyo atamuweka ndani mkandarasi au mhandisi mshauri.

Ametoa kauli hiyo leo Aprili 18, 2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya awamu ya tatu ya mradi wa mabasi yaendayo haraka yenye urefu wa kilomita 23.6 inayojengwa kati ya Gongo la Mboto hadi Katikati ya mji chini ya mkandarasi Syno Hydro.

Chalamila amefanya ziara baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wakazi wa eneo hilo juu ya tabu wanayoipata kufuatia ubovu wa barabara uliosababishwa na ujenzi unaoendelea.

Chalamila amesema mara zote mkandarasi amekuwa akijinasibu kufanya kazi usiku na mchana lakini hakuwahi kumshuhudia.
 
Ile ya kwenda Mbagala mbona haianzi kufanya kazi wakati kila kitu kiko tayari mpaka majengo yameanza kuchakaa? Tatizo nini? Ni hujuma kwa Mwendazake au ni nini?

Chalamila si angalau ahakikishe kwanza hii ya Mbagala imeanza kufanya kazi badala ya kuanza kukoroma kwingineko 😬🚮
 
..kama kazi inachelewa maana yake contractor hana uwezo.

..RC Chalamila anapaswa kuwakamata watumishi wa serikali ya Ccm waliompa kazi mkandarasi asiye na uwezo.
Umegonga penye mshono

Hivi wanaotoa hizo kandarasi, ni vyama vya upinzani?

Inakuwaje ikiwa ni hiyo hiyo serikali inayoongozwa na CCM, ndiyo iliyompa mkandarasi huyo, halafu CCM hiyo hiyo itishie kumfukuza mkandarasi huyo??🙆
 
Mkandarasi akiwa locked up itasaidia kuharakisha ujenzi!?
 
Ametoa kauli hiyo leo Aprili 18, 2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya awamu ya tatu ya mradi wa mabasi yaendayo haraka yenye urefu wa kilomita 23.6 inayojengwa kati ya Gongo la Mboto hadi Katikati ya mji chini ya mkandarasi Syno Hydro.
Huwa wanapanga
Anawaambia in advance nikifika pale nitawatishia kuwaweka ndani, halafu ninyi tetemekeni kidogo, wananchi wataridhika tu
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema haridhishwi na kasi ya ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka ya Gongo la Mboto na kama hali itaendelea hivyo atamuweka ndani mkandarasi au mhandisi mshauri.

Ametoa kauli hiyo leo Aprili 18, 2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya awamu ya tatu ya mradi wa mabasi yaendayo haraka yenye urefu wa kilomita 23.6 inayojengwa kati ya Gongo la Mboto hadi Katikati ya mji chini ya mkandarasi Syno Hydro.

Chalamila amefanya ziara baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wakazi wa eneo hilo juu ya tabu wanayoipata kufuatia ubovu wa barabara uliosababishwa na ujenzi unaoendelea.

Chalamila amesema mara zote mkandarasi amekuwa akijinasibu kufanya kazi usiku na mchana lakini hakuwahi kumshuhudia.
Je, kwenye Mkataba kuhusu Kandarasi hiyo kuna kifungu cha makubaliano kinachosema kwamba Mkandarasi akichelewesha utekelezaji wa Mradi adhabu yake ni kuwekwa ndani na Mkuu wa Mkoa??
 
Ile ya kwenda Mbagala mbona haianzi kufanya kazi wakati kila kitu kiko tayari mpaka majengo yameanza kuchakaa? Tatizo nini? Ni hujuma kwa Mwendazake au ni nini?

Chalamila si angalau ahakikishe kwanza hii ya Mbagala imeanza kufanya kazi badala ya kuanza kukoroma kwingineko 😬🚮
Hawanianmagari wanatafuta mwekezaji
 
Ile ya kwenda Mbagala mbona haianzi kufanya kazi wakati kila kitu kiko tayari mpaka majengo yameanza kuchakaa? Tatizo nini? Ni hujuma kwa Mwendazake au ni nini?

Chalamila si angalau ahakikishe kwanza hii ya Mbagala imeanza kufanya kazi badala ya kuanza kukoroma kwingineko 😬🚮
Mkuu magari ya kuanza kwenye hiyo barabara hakuna... Ndiyo maana amepewa mwekezaji alete mabus.
Mbagala pekee yanahitajika mabus 770 hii ni Kwa mujibu wa DARTS wenyewe
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema haridhishwi na kasi ya ujenzi wa barabara ya mabasi yaendayo haraka ya Gongo la Mboto na kama hali itaendelea hivyo atamuweka ndani mkandarasi au mhandisi mshauri.

Ametoa kauli hiyo leo Aprili 18, 2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa barabara ya awamu ya tatu ya mradi wa mabasi yaendayo haraka yenye urefu wa kilomita 23.6 inayojengwa kati ya Gongo la Mboto hadi Katikati ya mji chini ya mkandarasi Syno Hydro.

Chalamila amefanya ziara baada ya kuwapo kwa malalamiko kutoka kwa wakazi wa eneo hilo juu ya tabu wanayoipata kufuatia ubovu wa barabara uliosababishwa na ujenzi unaoendelea.

Chalamila amesema mara zote mkandarasi amekuwa akijinasibu kufanya kazi usiku na mchana lakini hakuwahi kumshuhudia.
Kwakweli hawa wakandarasi wa mchongo wanatuchelewesha sana.

Huyu Wa GMboto na yule wa Ilala Boma kwenda Buguruni ni wavivu kupita kiasi au hawana hela.
 
Speed lazima ipungue, mvua hizi na ujenzi hauwezi kwenda kwa kasi
 
Waanze kufanya ukaguzi alipataje tenda hiyo kupitia zabuni ilivyotangazwa.

Maana watu wanawapa ndugu zao tenda ambao ni "least qualified" kwa minajili mbalimbali.
 
Ile ya kwenda Mbagala mbona haianzi kufanya kazi wakati kila kitu kiko tayari mpaka majengo yameanza kuchakaa? Tatizo nini? Ni hujuma kwa Mwendazake au ni nini?

Chalamila si angalau ahakikishe kwanza hii ya Mbagala imeanza kufanya kazi badala ya kuanza kukoroma kwingineko 😬🚮
Itakuwa wanasubiria kumkabidhi mzabuni kuiendesha maana hii ya Kimara si imeangukia pua.
 
Back
Top Bottom