Albert Msando atoa maoni juu ya majibu ya miss Tanzania na Lundenga

Albert Msando atoa maoni juu ya majibu ya miss Tanzania na Lundenga

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Hii ameandika kupitia ukuta wake wa Instagram.

Ni Tanzania pekee Miss Tanzania anaulizwa kuhusu taarifa tofauti kwenye Passport, Leseni ya Udereva na Cheti cha Kuzaliwa anajibu kwamba hilo ni suala binafsi!!

Sasa mtu unaenda kuwakilisha NCHI na kudai utailetea sifa huku ukiwa na tuhuma kwamba umedanganya kuhusu umri ili ushiriki lakini unatoa majibu ya kitoto ili uonekane mtoto?

Labda tuiweke hivi. Ni kweli Sitti amezaliwa 1991 kama cheti chake KIPYA kinavyoonyesha. Pia ni kweli aliweza kupata cheti KIPYA cha kuzaliwa bila kutoa taarifa polisi kwamba cha zamani kimepotea. Tanzania inawezekana!!!

Je si kweli amedanganya kwa kutoa taarifa tofauti kwenye Passport na Leseni yake huko nje? Au ukiwa Marekani unaruhusiwa kudanganya na ukirudi hapa inakuwa poa tu?

Je kuna watu wanataka tuamini kwamba kilichotakiwa na Kamati ni Cheti cha kuzaliwa BASI kama kuna ushahidi mwingine unaopingana na Cheti hicho sio kazi ya Kamati!!

Ili kufanya mashindano haya yaheshimiwe na kuondoa maneno ambayo Kamati inasema ni shutuma za kipuuzi basi wangesema ukweli.

Wangetoa maelezo ya kina kuhusu taarifa tofauti za tarehe ya kuzaliwa kwenye Cheti, Passport na Leseni.

Hata kama alighushi ili apate kazi na aruhusiwe kuendesha gari Marekani basi waseme hivyo. Huwezi kuhalalisha uongo kwa kusema uongo zaidi!!

Huwezi kuita hizo shutuma ni umbea, chuki au upuuzi.
Hiyo ni dharau kwa waliolipa kiingilio na sisi ambao tunatamani kuona nchi yetu iking'aa kwenye anga za kimataifa!!

Its only light that can chase away darkness.... Kwa majibu ya leo kuhusu shutuma dhidi ya Ms Tanzania basi tunaenda kubaya!

Tulianza kudanganya na kutoa majibu mepesi kwenye kughushi vyeti, mikataba, matokeo ya mitihani, matokeo ya uchaguzi sasa kwenye michezo!!! #Basata #ShambaLaBibi #MajibuMepesi #Tanzania

Karibuni wadau Cc: Matola, King Kong III warumi?
 
Last edited by a moderator:
Mzee Lundenga ndipo ulipogotea uwezo wake wa kufikiri. Anadhani watanzania wote wana akili sawa na wale mashabiki wa chama chao wenye akili za maiti.
 
Nafikiri anadhani haya mashindano ni yaje mwenyewe ufike wakati baraza la sanaa litoe tamko na kusimamia haya mashindano sasa.
 
lundenga amemonopolize shindano
kwa kweli mimi binafsi toka 98 Basila mwanukuzi alikua miss nlianza kuangalia mpaka mwaka huu ila kwa upuuzi wa lundenga na bibi bomba wake nimejivua rasmi kuangalia shindano hilo
 
lundenga amemonopolize shindano
kwa kweli mimi binafsi toka 98 Basila mwanukuzi alikua miss nlianza kuangalia mpaka mwaka huu ila kwa upuuzi wa lundenga na bibi bomba wake nimejivua rasmi kuangalia shindano hilo

BASATA kazi yake ni ipi? TBL kupitia kinywaji chao cha Redds watoe tamko .Watu wana hisa zao mule hawatapenda upumbavu kama huu.
 
BASATA kazi yake ni ipi? TBL kupitia kinywaji chao cha Redds watoe tamko .Watu wana hisa zao mule hawatapenda upumbavu kama huu.

Haswa hao Tbl basata sidhani maana akikosa wadhamini ndio atatia akili.
 
Lundenga ameonyesha uwezo mdogo wa kufikiria. Nafikiri ana zeeka na ni wakati muafaka wa kuachie wengine kuendesha mashindano hayo. Kwani rhino agency ndo pekee wenye mamlaka na uwezo wa kuendesha mashindano ya miss Tanzania
 
Mzee Lundenga ndipo ulipogotea uwezo wake wa kufikiri. Anadhani watanzania wote wana akili sawa na wale mashabiki wa chama chao wenye akili za maiti.

hivi lundenga aliishia form gani?
 
Miss anaulizwa je una mtoto anadai eti kama muheshimiwa alivoeleza ndo hivo wanaotaka habari zaidi kuhusu miaka yake waende mamlaka ya kutoa cheti huyu miss bibi bomba ni zero brain na.mkorogo uliozidi

Mie kaniacha hoi kwa majibu yake jamani halafu leo sijui hajapaka make up aisee ndio nimeona uzee wake aiseee nadhani atakuwa na miaka 30 hivi na mtoto juu
 
Wameshauriana weeee na Abbas, wakaona liwalo na liwe, kwani nini..

Hivi Miss world si wanafanya utafiti au nao watafunika kombe ?
 
Back
Top Bottom