Albert Msando atoa maoni juu ya majibu ya miss Tanzania na Lundenga

Albert Msando atoa maoni juu ya majibu ya miss Tanzania na Lundenga

lundenga amemonopolize shindano
kwa kweli mimi binafsi toka 98 Basila mwanukuzi alikua miss nlianza kuangalia mpaka mwaka huu ila kwa upuuzi wa lundenga na bibi bomba wake nimejivua rasmi kuangalia shindano hilo

Richa adhia ilikua mwisho wangu nilishaona dalili kama hizi nikajitoa..na wala siwez angalia tena haya mambo
 
daaah eti ludenga anasema kuongea kifaransa kwa sitti ilikuwa ni moja ya njia ya kuwa approach majaji ...sasa ningependa miss tanzania ijayo mmoja wapo aongee kikabila kama ni muhehe au mchaga au msukuma aongee kisukuma..........
 
Watu ni noma kwa kufananisha matukio hebu soma hiyo picha chini then sikiliza maneno ya dj Khalid kwenye nyimbo yake ya hold you down ImageUploadedByJamiiForums1413926186.204471.jpg
 
Hakusafisha tuhuma. .zaidi kaleta maswali tu
 
Hahaaa raha sana, say may name nyaluhusa87 "mwamfupeeeeeee"
 
daaah eti ludenga anasema kuongea kifaransa kwa sitti ilikuwa ni moja ya njia ya kuwa approach majaji ...sasa ningependa miss tanzania ijayo mmoja wapo aongee kikabila kama ni muhehe au mchaga au msukuma aongee kisukuma..........

Hivi kuna jaji alikuwa anajua hiko kifaransa kweli? Au ndio mbele kwa mbele hata kama aliongea utumbo
 
Mzee Lundenga ndipo ulipogotea uwezo wake wa kufikiri. Anadhani watanzania wote wana akili sawa na wale mashabiki wa chama chao wenye akili za maiti.

Nae ndio mwisho wake....
 
Hii ameandika kupitia ukuta wake wa Instagram.

Ni Tanzania pekee Miss Tanzania anaulizwa kuhusu taarifa tofauti kwenye Passport, Leseni ya Udereva na Cheti cha Kuzaliwa anajibu kwamba hilo ni suala binafsi!!

Sasa mtu unaenda kuwakilisha NCHI na kudai utailetea sifa huku ukiwa na tuhuma kwamba umedanganya kuhusu umri ili ushiriki lakini unatoa majibu ya kitoto ili uonekane mtoto?

Labda tuiweke hivi. Ni kweli Sitti amezaliwa 1991 kama cheti chake KIPYA kinavyoonyesha. Pia ni kweli aliweza kupata cheti KIPYA cha kuzaliwa bila kutoa taarifa polisi kwamba cha zamani kimepotea. Tanzania inawezekana!!!

Je si kweli amedanganya kwa kutoa taarifa tofauti kwenye Passport na Leseni yake huko nje? Au ukiwa Marekani unaruhusiwa kudanganya na ukirudi hapa inakuwa poa tu?

Je kuna watu wanataka tuamini kwamba kilichotakiwa na Kamati ni Cheti cha kuzaliwa BASI kama kuna ushahidi mwingine unaopingana na Cheti hicho sio kazi ya Kamati!!

Ili kufanya mashindano haya yaheshimiwe na kuondoa maneno ambayo Kamati inasema ni shutuma za kipuuzi basi wangesema ukweli.

Wangetoa maelezo ya kina kuhusu taarifa tofauti za tarehe ya kuzaliwa kwenye Cheti, Passport na Leseni.

Hata kama alighushi ili apate kazi na aruhusiwe kuendesha gari Marekani basi waseme hivyo. Huwezi kuhalalisha uongo kwa kusema uongo zaidi!!

Huwezi kuita hizo shutuma ni umbea, chuki au upuuzi.
Hiyo ni dharau kwa waliolipa kiingilio na sisi ambao tunatamani kuona nchi yetu iking'aa kwenye anga za kimataifa!!

Its only light that can chase away darkness.... Kwa majibu ya leo kuhusu shutuma dhidi ya Ms Tanzania basi tunaenda kubaya!

Tulianza kudanganya na kutoa majibu mepesi kwenye kughushi vyeti, mikataba, matokeo ya mitihani, matokeo ya uchaguzi sasa kwenye michezo!!! #Basata #ShambaLaBibi #MajibuMepesi #Tanzania

Karibuni wadau Cc: Matola, King Kong III warumi?
Lundenga kashaanza kufikiri kama hao warembo
 
Last edited by a moderator:
siku aliposhnda babake alisema ana masters Lundenga anasema ana degree,ila wanajitahd kuongopa aiseee!
 
Bibi Bomba Huyu kafanya sana ufuska huko Marekani Leo eti mnatuletea abebe taji la heshima Kwa watanzania wote
Huu kweli ni upuuzi uliotukuka
Hapa Nina hasira sana na Ludenga na kuwaonea huruma wale majaji wote walio na akili fupi
#bongobound
 
kwani hakuna mshindi wa pili? kwanini asipewe huyo?, au aende kwanza mahakamani hii issue ndo ataisolve!
 
Mimi nimejitolea kwenda kwa mguu ubalozi wa Uingereza Counsular section kuwakabidhi vielelezo vya fojari hii with dispatch book halafu tuone kama Uingereza huwa inatowa Viza kwa mijitu inayofojifoji.

Cc: Pasco

Yeah....Tupambane na huu ufisadi.
 
Hivi si kuna wakati walimpitisha mhindi wakasema ni msukuma? au napoteza kumbukumbu, nisaidie kunikumbusha
 
mjadala huu hauna tija kwa taifa...

Karibu jukwaani mh. Mtemvu.
Hivi kweli mheshimiwa unamnadi mwanao kwa wakware kisa pesa, tutaaminije watoto wetu unaowapeleka mashariki ya kati huwapigi bei pia? Hivi na ile "Noah Nyeusi" ni yako? Mbona iko jimboni kwetu tu?
 
Back
Top Bottom