Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,319
Wapinzani wa Taifa Stars kwenye mechi ya mchujo wa kuwania kufuzu kombe la Dunia, timu ya Algeria imepata pigo la kuwakosa nyota wake watatu wanaocheza vilabu vya Porto, Valencia na Dynamo Zaghreb.
Kwa mujibu wa tovuti ya shirikisho la Algeria, wachezaji tegemeo, Yaccini Brahimi ( Porto), Sofiane Felghouli (Valencia) na El Soudani hawataweza kucheza pambano la Jumamosi dhidi ya Taifa Stars.
Wote watatu ni majeruhi hivyo kukosa pambano hilo la mtoano litakalochezeshwa na mwamuzi kutoka Mali.
Msafara wa Algeria unatarajiwa kuwasili nchini siku ya Alhamis kwa ndege binafsi ya kukodi, ukiwa na jumla ya watu 65 wakiwamo wachezaji 24.
Chanzo: Soka360
Kwa mujibu wa tovuti ya shirikisho la Algeria, wachezaji tegemeo, Yaccini Brahimi ( Porto), Sofiane Felghouli (Valencia) na El Soudani hawataweza kucheza pambano la Jumamosi dhidi ya Taifa Stars.
Wote watatu ni majeruhi hivyo kukosa pambano hilo la mtoano litakalochezeshwa na mwamuzi kutoka Mali.
Msafara wa Algeria unatarajiwa kuwasili nchini siku ya Alhamis kwa ndege binafsi ya kukodi, ukiwa na jumla ya watu 65 wakiwamo wachezaji 24.
Chanzo: Soka360
