Tetesi: Ali Hapi kwenda kumng'oa Mwigulu jimboni Iramba 2025

Tetesi: Ali Hapi kwenda kumng'oa Mwigulu jimboni Iramba 2025

Lyambalyetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2021
Posts
278
Reaction score
255
Ali Hapi ambaye anatoka familia ya Mzee Ugula katika kijiji cha Tutu, Kata ya Kiomboi, Wilayani Iramba amekuwa na safari nyingi za kumtembelea bibi yake Mzaa Mama kijijini hapo na safari ya mwisho aliyoifanya na kupiga picha na bibi huyo inasemekana imezalisha jicho la kuonwa na mama na kupewa Nafasi ya Ukatibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi. Hii yote ni kutokana na Ali Hapi kuonwa anawajali sana wazazi na anaweza kuwatumikia vema.

Hata hivyo mtazamo mkubwa uliopo ni Ali Hapi kuanza kutengeneza network hapo kijijini na Kiomboi Mjini ambako ameshapata namba za Viongozi wa CCM katika Kata 7 ambazo anategemea kuanza nazo katika kujitambulisha vizuri akitarajiwa kuleta upinzani mkali dhidi ya Dkt. Mwigulu ndani ya Chama.

Ali Hapi alisikika akitamaka wazi kuwa yeye ni muumini wa vipindi viwili vya ubunge zaidi ya hapo Mbunge huyo anakuwa hana jipya.

Hili linaonekana wazi kuwa lilikuwa ni ndogo dhidi ya Dkt. Mwigulu ambaye ameshatumikia vipindi vitatu katika Jimbo la Iramba.
 
Hekima imuelekeza ama kurudi shambani ama kuanzisha biashara nyingine 🐒
kupambana na mwigulu Iramba ni kujitesa mwenyewe na kutokujithamini mwenyewe 🐒
 
😁😁😁 ngoja nicheke kwanza....

Mwigulu Nchemba kwao ndio kama mfalme anapendwa mpaka na watoto wadogo namwambia nini?.. pesa anazo anaweza wachukua wapiga kura na kuwasafirisha waende popote wanapotaka.. yeye ana nini huyo kijana? Kaanza kupajua kiomboi baada ya kutumbuliwa ndio kujifanya mkulima..

Mwigulu bado anahitajika singida
 
😁😁😁 ngoja nicheke kwanza....

Mwigulu Nchemba kwao ndio kama mfalme anapendwa mpaka na watoto wadogo namwambia nini?.. pesa anazo anaweza wachukua wapiga kura na kuwasafirisha waende popote wanapotaka.. yeye ana nini huyo kijana? Kaanza kupajua kiomboi baada ya kutumbuliwa ndio kujifanya mkulima..

Mwigulu bado anahitajika singida
Singida chini ya mwigulu kuna maendeleo gani zaidi ya kununua timu za kubadili majina ?
 
hekima imuelekeza ama kurudi shambani ama kuanzisha biashara nyingine [emoji205]
kupambana na mwigulu Iramba ni kujitesa mwenyewe na kutokujithamini mwenyewe [emoji205]
Kwanini mkuu
 
Ally Hapi ni vema aende Kondoa,umesema anatokea ukoo wa Ugula,bila shaka Mwalimu Ugula mama yake mkubwa!
 
Sema kweli lakini ubunge ulitakiwa kua na limit ya mihura, mihura miwili tu unaachia wengine nao waonyeshe wana nini. Sasa mtu anataka kila siku awe yeye tu! Huo unakua ubinafsi sasa
 
Back
Top Bottom