Ali Kamwe ataweza kushindana na Sandaland na Azam FC Mahakamani?

Ali Kamwe ataweza kushindana na Sandaland na Azam FC Mahakamani?

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Mpaka SASA Kamwe anadiwa bilioni kumi na nne; Huyu jamaa ataweza kweli kushindana na Sandaland na Azam mahakamani?

Azam FC imempatia taarifa rasmi Afisa Habari wa Yanga SC, Haji Ally Kamwe, kudai fidia ya TZS 10,000,000,000 kwa tuhuma za kuichafua klabu hiyo kwa madai ya kuzima taa uwanjani ili kumzuia Prince Dube kufunga magoli.

Azam FC inadai kuwa kauli hiyo ilitolewa hadharani na Kamwe kupitia vyombo vya habari, na imesababisha madhara makubwa, ikiwemo kupoteza mahusiano ya kibiashara na wadau wake.

Klabu hiyo imetoa muda wa siku 14 kwa Kamwe kutengua kauli zake hadharani, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Azam FC imeeleza kwamba itaendelea kulinda brand yake dhidi ya mtu yeyote au taasisi itakayojaribu kuichafua kwa njia yoyote ile.

Kamwe amekuwa akijulikana kwa kauli zake za moto, lakini suala hili linaweza kuwa hatua mpya kwa migogoro na vilabu vikubwa nchini.
 
Upepo wa ujinga umeingia mjini!

Tukifukua makaburi ya Zaka za Kazi NCHI nzima itanuka case!

Waziri mwenye zamana aingilie kati huu upuuzi!
 
Ujinga ujinga mwingi sana nchi hii,na bahati mbaya sana hakuna msafi Bongo wote wananuka...............
 
Mpaka sasa timu za Azam na Yanga zimejitokeza Hadharani Kutoa kusudio la Kushitaki...!

Simba yenyewe bado ....!

SandaLand ni taasisi ya kibiashara inajipigania...!

Hatujui Madai Ya Simba yatakuwaje..? Mwanasheria wa Simba asije Muiga mwenzie Patrick wa Yanga.

Wasemaji acheni Kidomodomo..!
 
Mpaka SASA Kamwe anadiwa bilioni kumi na nne; Huyu jamaa ataweza kweli kushindana na Sandaland na Azam mahakamani?

Azam FC imempatia taarifa rasmi Afisa Habari wa Yanga SC, Haji Ally Kamwe, kudai fidia ya TZS 10,000,000,000 kwa tuhuma za kuichafua klabu hiyo kwa madai ya kuzima taa uwanjani ili kumzuia Prince Dube kufunga magoli.

Azam FC inadai kuwa kauli hiyo ilitolewa hadharani na Kamwe kupitia vyombo vya habari, na imesababisha madhara makubwa, ikiwemo kupoteza mahusiano ya kibiashara na wadau wake.

Klabu hiyo imetoa muda wa siku 14 kwa Kamwe kutengua kauli zake hadharani, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Azam FC imeeleza kwamba itaendelea kulinda brand yake dhidi ya mtu yeyote au taasisi itakayojaribu kuichafua kwa njia yoyote ile.

Kamwe amekuwa akijulikana kwa kauli zake za moto, lakini suala hili linaweza kuwa hatua mpya kwa migogoro na vilabu vikubwa nchini.
Sandaland ni mshamba wa kiha ,hana jipya ,anadondoshwa tu mahakamani.
 
Sandaland hana kesi; ni kiki tu. Iliyodhalauriwani jezi siyo Kampuni ya Sandaland. Halafu kughadaru bidhaa siyo defamation hata siku moja. Ndiyo maana hata Consumer Report hutoa ranking za bidhaa mbalimbali wakionyesha bidhaa zenye ubora mzuri na zile zisizokuwa na ubora.

Azam FC nao hawana kesi, ni kiki tu. Kutoa maoni ya kumtuhumu mtu yeyote siyo defamation mpaka kuwe na tamko la kuonyesha kuwa mtoa maoni hayo ana uhakika kuwa mtu anayetumiwa alifanya jambo analotuhumiwa nalo. Mtamkaji anakuwa anafanya defamation akitegemea ama kunufaika na tamko hilo au kumdhuru mtuhumiwa kwa tamko hilo.
 
Back
Top Bottom