kwanza mimi si shabiki wa timu wala mtu. mimi naheshimu na napenda kazi nzuri.
hivi huyu jamaa hanaga watu wa kumshauri. msanii mkubwa kama yeye anatoa nyimbo mbovu mpaka unashangaa, management inaruhusu vipi nyimbo mbovu kama hela itoke eti ndio nyimbo mpya.
ishu sio kutaka ashindane. Maua sama, Aslay wanatoa nyimbo kali wanashindana na nani? kila akifanyacho hakina uelekeo. kaanzisha kinywaji, hata maendeleo yake hakieleweki. promo ya hiyo biashara zero. Mara kasajiliwa na team hata kucheza hatuoni yaani amekuwa kama mtu wa kutapa tapa. Afanyi kitu asilimia mia kikaeleweka. Kiukweli ana asset kubwa sana ya mashabiki waliyenaye bega kwa bega ambayo hata wasanii wengine wanatamani lakini anawaangusha sana. itafika steji watamchoka.
sasa kulikuwa na lebo rockstar4000 leo tena naona kuna kingsmusic sijui.
huyu jamaa ni msanii mzuri ila watu wanaomzunguka hawamtakii mema. haiwezekani mtu wako wa karibu anaaribu soko lake na nyie mkawa mnamwangalia tu..