Ali Msham, Julius Nyerere na Wanachama wa TANU Tawi la Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa 1954

Ali Msham, Julius Nyerere na Wanachama wa TANU Tawi la Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa 1954

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
ALI MSHAM, JULIUS NYERERE NA WANACHAMA WA TANU WA TAWI LA MTAA WA JARIBU MAGOMENI MAPIPA 1954

Watoto wa Ali Msham walizihifadhi picha hizo hapo chini kwa zaidi ya miaka 60.

Miongo sita imepita hadi picha hizi kufika mikononi kwangu na ndiyo ikawa sababu ya historia ya Ali Msham mzalendo aliyefungua moja ya matawi ya kwanza ya TANU yaliyokuwa na nguvu kufahamika.

Nyumba palipofunguliwa tawi hili Mtaa wa Jaribu ipo hadi leo na wanae wanaishi katika nyumba hii.

Kwa namna ya kushangaza nyumba hii imekuwa kivutio cha wanahabari wengi wakifika pale kuitazama.

Kinachowavutia khasa ni kuwa hapa katika nyumba hii Mama Maria alikuwa na duka lake dogo akiuza mafuta ya taa wakati yeye na mumewe walipohamia Magomeni Maduka Sita.

Kumuondolea Mama Maria adha ya kwenda Kariakoo ambako alikuwa na duka lake la kwanza la mafuta ya taa Mtaa wa Mchikichi na Livingstone, Ali Mshama alimfungulia duka hapo nyumbani kwake.

Pamoja na duka hili la Mama Maria Ali Msham alifungua shule ya TAPA upande mmoja wa nyumba yake wasome watoto wadogo wa masikini (shule hizi zilizokuwa zikimilikiwa na Tanganyika African Parents Association (TAPA) zilitoa mchango mkubwa kwa watoto kusoma ambao wazazi wao walikuwa na kipato cha chini).

Ukiangalia picha ya Mtaa wa Jaribu ulivyokuwa miaka 60 iliyopita utaona nyumba zimeishia Mtaa wa Idirisa kwa sasa na kuanzia hapo kwenda mbele ni vichaka, minazi na mkorosho.

Nyakati za jioni maghrib ikiingia sehemu hiyo ilikuwa kiza.

Ali Msham alimpa kazi mmoja wa wanae jina lake Abdallah Omari Likonda kuwa anamsindikiza Mama Maria na kumbebea vitu vyake hadi nyumbani kwake.

Abdallah Omari Likonda yu hai na sasa ni mtu mzima anaishi Mvuti Chanika.

Picha ya kwanza kulia ni Ali Msham na Julius Nyerere ni huyo kakaa nyuma ya meza akiwa na wanachama wa TANU.

Siku hii Ali Msham alimkaribisha Nyerere tawini ili amkabidhi samani aliyochonga kwa ajili ya ofisi yake New Street.

Picha ya pili kushoto inamuonyesha Ali Msham aliyekaa kati shati jeusi na wanachama wa tawi la TANU Magomeni, picha inayofuatia ni siku wanachama wa walipokusanyika kwenye tawi kufanya dua kwa ajili ya safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955.

Picha ya mwisho ni hapo tawini Magomeni inamuonyesha kulia Sheikh Suleiman Takadiri, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU, kushoto ni John Rupia na katikati aliyeshika tama ni Zuberi Mtemvu; Julius Nyerere haonekani amezibwa na John Rupia.

332112372_599925598313032_3498421326076876075_n.jpg
332112873_753509626177609_6597540364776209818_n.jpg
332112349_151152337834294_8621908047897599770_n.jpg
330762057_727534922208468_4238563135424968807_n.jpg
 
J.K.Nyerere alikua na kipawa sana kuwaunganisha watanzania sio suala dogo.
 
J.K.Nyerere alikua na kipawa sana kuwaunganisha watanzania sio suala dogo.
Jiwe...
Nyerere yeye ndiye aliyeunganishwa kwanza hapa Dar es Salaam na wenyeji wa mji.

Kawakuta watu wako pamoja katika TAA na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Watu maarufu waliompokea anza na Sykes brothers na jamaa zao Dossa Aziz, John Rupia kisha wafanyabiashara wa Soko la Karikoo na akina Shariff Attas na Mshume Kiyate.

Njoo viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Ali Mwinyi Tambwe, Iddi Faizi Mafungo, Jumbe Tambaza, Mwinjuma Mwinyikambi Iddi Tosiri.

Abdul na Dossa wakimfikisha kwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir na Khalifa wa Tariqa Qadiriyya.

Kanisa liljiweka mbali sana na harakati za kupigania uhuru.

Huwezi kupata hata picha moja Nyerere yuko na viongozi wa kanisa.

Tafuta.

Hakukuta watu wa Dar-es-Salaam wako vitani wanagombana.

Baba yangu hakuwa katika kundi la vijana wanasiasa lakini alimjua Nyerere nyumbani kwa Abdul Sykes.

Kisha Mwalimu akaenda majimboni.
Safari yake ya kwanza alikwenda Morogoro akiongozana na Zuberi Mtemvu.

Baada ya hapo Lindi akiongozana na Ali Mwinyi Tambwe na alifatwa hapa Dar es Salaam na Ali Mnjawale na SAlum Mpunga.

Ukienda majimboni kote historia ni kama hii.

Lindi kapokelewa na wana mji akina Suleiman Masudi Mnonji, Yusuf Chembera, Mussa Lukundu, Salum Mpungana na Ali Mnjawale.

Tanga akina Hamisi Kheri, Mohamed Kajembe.
Historia yote hii imo katika kitabu cha Abdul Sykes.

Leo hatuhitaji kudhania kuwa labda ilikuwa hivi au vile.
 
LENGO LA MADA

Mzee Mohamed Said Kwa kifupi sema hivi Ili ueleweke:-

Uhuru wa nchi hii umepiganiwa na Wazee wa kiislam, Wazee wa mji, Waswahili wa hasa Kariakoo

Nyerere Mgalatia Mkatoliki hakufanya chochote alikuta kila jambo limeratibiwa

Inaudhi sana Wazee wetu wa Kiislam Wazalendo hawatajwi kama wapigania Uhuru wa nchi hii [emoji23][emoji23][emoji23]

Wamesahaulika


Wabillah Tawfiq,
 
Nyerere kafika Dar kawakuta hao wazee wako kwenye harakati za kudai uhuru ndio wakamkaribisha kwenye chama,alivyopata uhuru akawageuka
Akawageukaje? Msaada tafadhali
 
J.K.Nyerere alikua na kipawa sana kuwaunganisha watanzania sio suala dogo.
Weeeeeh, Toa Ukristo wako hapa

Uhuru wa nchi hii umepiganiwa na Waislam TU

Hata hiyo meza hapo aliyechonga ni Ali Msham, alimchongea Nyerere afanyie shughuli za TANU

Ukijifanya msomi na mjuaji tunakuletea picha tulizopigwa Marekani na London za miaka ilee ilihali wewe hujafika huko bado [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wewe mzee ni shida sana!Mdini sana!

Luka...
Hakuna Uislam hapo kama dini bali nasahihisha historia ambayo iliwafuta Waislam kama wazalendo waliokuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nikisomesha historia ya TANU huwaambia wanafunzi wangu wakawasome Dr. Kwegyir Aggrey na Kleist Sykes katika Dictionary of African Biography (2011).

Kisha nawaambia wakamsome Kleist Sykes katika "Modern Tanzanians," (1973).

Kisha nawaambia wakamsome tena Kleist Sykes katika: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) "The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, (1998).

Huu ndiyo utangulizi wangu wa historia ya TANU.
 
Nyerere kafika Dar kawakuta hao wazee wako kwenye harakati za kudai uhuru ndio wakamkaribisha kwenye chama,alivyopata uhuru akawageuka
Nyerere kafika Dar, kakaribishwa na hao wenyeji wanaotajwa na ndugu yetu Mohamed. Ndani ya mwaka mmoja kagombea urais wa TAA na kumbwaga mwenyeji Abdul Sykes kwenye sanduku la kura.

Swali langu kwako na kwa Mohamed, hizo kura alizopata Nyerere kushinda urais wa TAA alipigiwa na wakristo au wazanaki wenzake?

Wajumbe wa mkutano wengi walikuwa haohao waislam, nini kiliwazuia kumchagua muislam mwenzao?
 
Nyerere kafika Dar, kakaribishwa na hao wenyeji wanaotajwa na ndugu yetu Mohamed. Ndani ya mwaka mmoja kagombea urais wa TAA na kumbwaga mwenyeji Abdul Sykes kwenye sanduku la kura.

Swali langu kwako na kwa Mohamed, hizo kura alizopata Nyerere kushinda urais wa TAA alipigiwa na wakristo au wazanaki wenzake?

Wajumbe wa mkutano wengi walikuwa haohao waislam, nini kiliwazuia kumchagua muislam mwenzao?
Mimi ni Christian ila Nyerere simkubali,matatizo yote tuliyonayo ya kiuchumi, Chanzo ni yeye, katumia resources zetu kukomboa nchi za kusini,katumia resources zetu kupigana vita ya Uganda
 
Mimi ni Christian ila Nyerere simkubali,matatizo yote tuliyonayo ya kiuchumi, Chanzo ni yeye, katumia resources zetu kukomboa nchi za kusini,katumia resources zetu kupigana vita ya Uganda
Umetoka nje ya mada, labda ufungue uzi mwingine kwa hayo malalamiko yako dhidi ya Nyerere. Kinachojadiliwa hapa ni

"Ali Msham, Julius Nyerere na Wanachama wa TANU Tawi la Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa 1954"​

 
Umetoka nje ya mada, labda ufungue uzi mwingine kwa hayo malalamiko yako dhidi ya Nyerere. Kinachojadiliwa hapa ni

"Ali Msham, Julius Nyerere na Wanachama wa TANU Tawi la Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa 1954"​

Kwanza huyo ni Muislam, Mnafiki sana angalia comments zake kwenye mada zingine
 
Mimi ni Christian ila Nyerere simkubali,matatizo yote tuliyonayo ya kiuchumi, Chanzo ni yeye, katumia resources zetu kukomboa nchi za kusini,katumia resources zetu kupigana vita ya Uganda
Acha UNAFIQ we Muislam
 
Nyerere kafika Dar, kakaribishwa na hao wenyeji wanaotajwa na ndugu yetu Mohamed. Ndani ya mwaka mmoja kagombea urais wa TAA na kumbwaga mwenyeji Abdul Sykes kwenye sanduku la kura.

Swali langu kwako na kwa Mohamed, hizo kura alizopata Nyerere kushinda urais wa TAA alipigiwa na wakristo au wazanaki wenzake?

Wajumbe wa mkutano wengi walikuwa haohao waislam, nini kiliwazuia kumchagua muislam mwenzao?
Gagnija,
Julius Nyerere "hakumbwaga," Abdul Sykes katika uchaguzi wa TAA 1953.

Kwa Dar-es-Salaam ile ya 1950s Nyerere asingeweza kupambana na Abdul kwa vyovyote.

Uchaguzi huu nimeueleza hapa mara nyingi kuhusu Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe walipokwenda Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu kujadili namna ya kumtia Nyerere katika uongozi wa juu wa TAA.

Ali Mwinyi Tambwe alikuwa Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (,Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Judith Listowel katika kitabu chake, "The Making of Tanganyika," ameeleza kuwa Nyerere alishinda kwa.kura chache.

1678739946850.png

Mkakati wa viongozi wa TAA na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilikuwa TANU iongozwe na Mkristo ili kuzimua Uislam uliogubika harakati za kupambana na ukoloni.

Hofu ilikuwa kuzuia TANU kuonekana chama cha Waislam na harakati za kudai uhuru ni harakati za Waislam.

Hii ingesababisha kukosekana kwa umoja wa wananchi wote dhidi ya ukoloni.

Lskini kubwa ilikuwa kuzuia kuundwa chama ambacho Wakristo watajitambulisha kuwa ndiyo chama chao.
 
Kwenye nyuzi zako unaitaja sana hii "Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika", iliishia wapi? Au lilikuwa tawi la EAMWS. Sikuwahi kuisikia, labda kwakuwa nilikuwa naishi kijijini miaka hiyo.
 
Kwenye nyuzi zako unaitaja sana hii "Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika", iliishia wapi? Au lilikuwa tawi la EAMWS. Sikuwahi kuisikia, labda kwakuwa nilikuwa naishi kijijini miaka hiyo.
Gagnija,
Wazee wetu waliunda African Association 1929 na 1933 wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Viongozi wa African Association ndiyo hao hao walikuwa viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Jengo la Al Jamiatul Islamiyya lilikuwa New Street na Stanley na ndipo ilipokuwa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School.

Al Jamiatul Islamiyya ilikuwa inajitegemea haikuwa tawi la EAMWS.

Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika pamoja na jumuiya nyingine za Kiislam zilipigwa marufuku pamoja na EAMWS 1968.

1678730827086.jpeg

1678740045537.jpeg

Jengo na iliyokuwa shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika leo ni mali ya Serikali (TAMISEMI)​
 
Mzee wangu story zako zimenifanya nijue vitu ambavyo nilikuwa sijui japo nakaa magomeni mapipa mtaa wa magomeni kwa miaka mingi.
 
Back
Top Bottom