Aliaga anakwenda kuchukua pesa zake za mafao hakurudi!

Aliaga anakwenda kuchukua pesa zake za mafao hakurudi!

Hahaaaaa, kama mazuri. Nimemkunbuka mzee mmoja nilimkutaga huko Kilolo anaitwa Upemba. Jamaa baada ya kustaafu na alikiwa mkuu qa Idara akazitumbua zote. Zilipoisha akawa amezeeka zaidi ya Baba yake mzazi na akakimbilia Mwanza kwa mkewe. Hawa wazee waandaliwe kushika pesa nyingi baada ya kustaafu.
 
Miezi minne iliyopita kuna mzee aliondoka hapa kijiji cha masakata wilayani tunduru kuelekea jijini dar es salaam 'jiji la maraha.

kwenda kushughulikia miamala ya pesa zake za mafao baada ya kuhudumu serikalini kwa kipindi kirefu,
Mzee aliondoka mwezi wa tano mwaka huu kwa kumuaga bi mkubwa kuwa atarejea baada ya wiki moja.

Pia kukiwa na shabaha ya kurudi na pesa za kuwekea sawa mashamba yao,
,kweli alifika mjini akakutana na mwanawe mkubwa wa kike aliyemsaidia kurahisisha shughuli zake za kibenki.

Huyo mwanawe naye kidogo alihamdulillah anahudumu kwenye wizara moja nyeti,
Baada ya kuchukua maokoto mzee aliweza kutupa kiasi cha pesa kwa bi mkubwa baada ya hapo,
mzee hakupatikana tena si kwa simu wala salamu .
Watu walihangaika vituo vya polisi na mahospitalini ,mochwari ,baa zote na vijiwe vya kahawa ,ikawa hakuna majibu.

Cha kushtusha ni jana mzee amepatikana huko mbezi kwenye nyumba moja amefungiwa na binti mmoja umri wa mwanawe ,akiwa hana hata wasiwasi na hajui kama watu wanahangaika wala kaacha bi mkubwa huko home.

Mzee amekamata remote hana hata mashaka bi mdogo amemmwagia udambwi dambwi juu ya meza,
baada ya kumkuta hapo palizuka vurumai kubwa nguo kuchanika ili kumtoa mzee pale nyumbani kwa bi mdogo.

Huku mzee akiapa kutaka kuwaachia radhi watoto wake na bi mdogo akitaka kuwafungulia mashtaka watoto wa mzee kumletea fujo nyumbani kwake!

Angalizo :wazee wasiachwe peke yao kwenda kufanya miamala wasije angukia kwenye mikono isiyo salama!


Aua wafungue branch huko, ukishafika huu mji basi, Kama una mafao watakula na wewe, yakiisha utasukumwa kwa mkeo.
 
Wazee wastaafu wanatia aibu sijui ni nin huwa kinawapata
Kuna mzee kastaafu kachukua chombo kipya kibichi kabisa kamzalisha mtoto kamjengea nyumba na kumfungulia duka
Mke wake alivyoona visa vinazidi mzee harudi nyumban
Kaamua kuondoka kwao na watoto nao wakafuata nyuma
Mzee kabaki na kimada wake wanatamba mtaani
Pesa zimeisha sasa ameshauza nyumba moja aliyoanza nayo maisha na mkewe , viwanja na nyumba ya familia inapigwa mnada
zikiisha kabisa najua ataanza kumtafuta mke ambaye kwasasa yupo kwa watoto wenye kazi zao patachimbika hawana hamu na baba yao
Wanaume baadhi yenu huwa mnapatwa na nin mkisha pata mafao yenu ya uzeeni au balehe huanza upya
 
Wazee wastaafu wanatia aibu sijui ni nin huwa kinawapata
Kuna mzee kastaafu kachukua chombo kipya kibichi kabisa kamzalisha mtoto kamjengea nyumba na kumfungulia duka
Mke wake alivyoona visa vinazidi mzee harudi nyumban
Kaamua kuondoka kwao na watoto nao wakafuata nyuma
Mzee kabaki na kimada wake wanatamba mtaani
Pesa zimeisha sasa ameshauza nyumba moja aliyoanza nayo maisha na mkewe , viwanja na nyumba ya familia inapigwa mnada
zikiisha kabisa najua ataanza kumtafuta mke ambaye kwasasa yupo kwa watoto wenye kazi zao patachimbika hawana hamu na baba yao
Wanaume baadhi yenu huwa mnapatwa na nin mkisha pata mafao yenu ya uzeeni au balehe huanza upya
Mkulima mmoja walaji wengi tuwakinge wazee na maharamia!
 
Angalizo :wazee wasiachwe peke yao kwenda kufanya miamala wasije angukia kwenye mikono isiyo salama!
Duh yaani nihangaike peke yangu mwisho wa siku unigande kwenye kuchukua mafao yangu,mbona wasinigande wakati wa kwenda kazini?

Acha mzee ale jasho lake,ni upuuzi kumpangia mtu namna ya kutumia mali alotafuta kwa jasho lake
 
Kwa kuwa hii ni chai na kwa kuwa mzee hakusaidiwa kuzitafuta hizi hela ni zake ana haki ya kutumia atakavyo na kwa kuwa mzee ni mtu mzima mwenye akili timamu na kwa kuwa kinachowasukuma watoto kupagawa ni kudhania wangepata mgao na wameukosa na kwa kuwa hatujui maisha aliyokuwa anaishi mzee kabla hajatoka home kwenda daslam pengine alikuwa ana nyanyasika as usual kwa wanaume wakishastaafu na kwa kuwa mzee kapatikana akiwa salama haumwi na hajadhurika labda tu maokoto yamekata basi naomba nisichangie huu uzi
 
Kwa kuwa hii ni chai na kwa kuwa mzee hakusaidiwa kuzitafuta hizi hela ni zake ana haki ya kutumia atakavyo na kwa kuwa mzee ni mtu mzima mwenye akili timamu na kwa kuwa kinachowasukuma watoto kupagawa ni kudhania wangepata mgao na wameukosa na kwa kuwa hatujui maisha aliyokuwa anaishi mzee kabla hajatoka home kwenda daslam pengine alikuwa ana nyanyasika as usual kwa wanaume wakishastaafu na kwa kuwa mzee kapatikana akiwa salama haumwi na hajadhurika labda tu maokoto yamekata basi naomba nisichangie huu uzi
Labda edo kumwembe anaweza kuwa na hii taarifa maana ni kijiji chao!
 
Back
Top Bottom