Alichoandika Mnyika: Maneno ya Ntobi si msimamo wa Kamati kuu Wala CHADEMA na mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti huyo yako chini ya Kanda

Bezecky

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
494
Reaction score
897
Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Bw Emmanuel Ntobi licha ya kutojibiwa chochote na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Tundu Lissu kwa muda mrefu Sasa bado ameendelea na kumdhihaki, kumdhalilisha na kumtweza utu wake kinyume kabisa na Katiba, kanuni na miongozo ndani ya CHADEMA .

Katibu Mkuu wa CHADEMA Bw.John John Mnyika alipoulizwa na Wanachama wa CHADEMA mitandaoni kama anachokifanya Mwenyekiti wa Shinyanga kama ni msimamo wa Kamati kuu au CHADEMA,

Kwa haraka Katibu Mkuu huyo alimjibu Mwanachama huyo kuwa huo si msimamo wa Kamati kuu Wala CHADEMA na mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti huyo yako chini ya Kanda na anamshangaa kwanini Emmanuel Ntobi anaendelea kutamba kwa kutweza wengine utu wao hadharani tena mitandaoni Waziwazi bila kuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu.

Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA ya mwaka 2006 kosa alilolifanya BW. Emmanuel Ntobi adhabu yake ni kufutwa Uongozi au Kufukuzwa Uanachama au vyote kwa pamoja,

Hata hivyo aliyekuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Kaskazini Bw Godbless Lemma amesisitiza pia hatua zinapashwa kuchukuliwa ili kuepa visasi na majibizano ya kukidhalilisha chama na wanachma



 
Huyu dogo Mimi Nilikuwa nashangaa anvyoendekeza uchawa huku akitukana Lissu bila sababu zozote za msingi nadhani huyu avuliwe uongozi
 
Huyu mpaka Sasa anaishi kwa kaka yake at the age 40 ni aibu sana pengine ndio maana haoni umuhimu wa watu makini
 
kumbe ni kapuuzi hakujui kufanya siasa
Hata wale kina Nyerere, boni, kilewo, ni washamba. kuna steji za kiuongozi ukifika hutakiwi kuwa emotional kiasi kile. Sio busara kuonesha hisia za kichawa kwenye hali kama ya sasa chadema . Kiongozi lazima uoneshe ukomavu flani wa kuweza kutulia kwanza ukisubiri lolote lijalo.

kwa mfano: Mbowe akisema hatogombea, wao watafanyaje. Bila shaka watateseka sana. In some situations, neutrality is a better choice!

YESU NI BWANA&MWOKOZI
 
Hajatukana hata katoa maoni yake ambaye wengi hawayapendi
Ukimkosoa au ukimpinga lisu unaonekana mbaya alafu mda huo huo wanahubiri democrasia

Unavyogombania nafasi kupingwa ni kawaida
hapo kwenye jina lissu towa weka mbowe maana lissu ndo kwanza anagombea ila mbowe kawa kwenye kiti miaka 20 huko
 
Wao wanauhakika kua boss wao lazima anagombea …so ni ngumu wao kuacha kutuma makombora ya kinyesi.
 
Mbona heading na alivyosema Mnyika ni vitu viwili tofauti.

Sijaona sehemu Mnyika kaagiza avuliwe uanachama.
 
Hivi watu wanajua matusi au ni mahaba tu..mtu kusema jamaa hawezi kuwa kiongozi hata wa mtaa ni tusi??? Mbona Mama Samia watu wanasema zaidi ya hayo, mkiulizwa mnasema ndo demokrasia hiyo, lkn kwa Lissu mtu anasemwa anatukanwa.
Kuwa kiongozi mkubwa sio lele mama..lazima mawe yalushwe tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…