Alichokifanya Chasambi walishakifanya Zimbwe na Che Malone

Alichokifanya Chasambi walishakifanya Zimbwe na Che Malone

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Huu uzi si wa kutetea upuuzi alioufanya Ladack Chasambi katika mechi ya jana kati ya Fountain Gate vs Simba. Huu uzi nia yake kuelezea maeneo mawili ambayo Simba imekuwa na tatizo nayo kwa muda mrefu. Nasisitiza, kosa moja halihalalishi makosa mengine.

Katika mechi kati ya Simba vs Yanga ambayo kipa alikuwa Ayoub Lakred (wenye kumbukumbu mtanikumbusha ni mechi ipi), Zimbwe alimrudishia Lakred mpira wa kasi na wa juu na bahati nzuri Lakred alikuwa na control nzuri akaweza kuuclear. Kosa la Chasambi halitofautiani sana na kosa hili. Kuna mchezaji mwingine juzijuzi aliwahi kumrudishia Camara mpira wa namna hii nadhani ni Che Malone. Hakuna ubaya kumrudishia kipa mpira, swali unarudisha mpira ulio na usalama gani kwa timu yako?

Turudi kwenye tatizo la msingi la Simba:
Ukweli ni kuwa tatizo la "backpasses" limekuwa sugu pale Simba. Wengi wanadhani tunaposema "backpass" ni mpaka mpira uende kwa kipa. Hamza akiupeleka mpira kwa Zimbwe unategemea tunaenda mbele, utashangaa naye anarudisha kwa Che Malone au anapiga pasi ya pembeni kwa Kagoma. Nahisi Kocha Mgunda ndiyo alililea hili tatizo, mchezaji kama Onyango alikuwa hapigi pasi ya mbele hata siku moja, ni ama atapiga pasi ya nyuma au ya pembeni.

Robertinho akaja akajaribu kulitibu kwa "direct football", kiasi alifanikiwa ila watu wakaanza kulalamika mpira wa "butua butua" ingawa mimi sikubaliani na lebo hiyo watu walioipa.

Tusimlaumu kocha Fadlu David kwa hili tatizo. Kabla Chasambi hajajifunga, alionekana kuwahimiza wachezaji wapeleke mpira mbele ila hawakumzingatia. Kabla ya goli alilofunga Kapombe kwenye mechi ya wiki iliyopita dhidi ya Tabora, Fadlu alionekana kuwahimiza wachezaji wapeleke mpira mbele maana walionekana kuchezea mpira eneo lao bila faida. Kwa hiyo tusiseme Fadlu ndiye anayewafundisha hili.

Sielewi kwa nini baadhi ya wachezaji wa Simba wakifanyiwa pressing wanapata kitete wanaona afadhali arudishe mpira nyuma kuliko kuupoteza. Hili lilikuwa tatizo sugu hadi mchezaji anaogopa kupoteza mpira hata akiwa zone ya adui. Mchezaji anaweza kutoka na mpira kwenye kona ya adui zikapigwa pasi kurudi nyuma hadi kwa golikipa wao. Wakati mwingine wakawa wanapeana pasi za kusakiziana ingawa hili tatizo naona limepungua sana.

Jinsi ya kulitatua hili tatizo:

Niliwahi kusema ni muhimu kuwarudisha wachezaji kwenye zoezi la "angaisha bwege" au kitaalam linaitwa "rondo" au "rondos" ambalo kwa mtazamo wangu wachezaji wengi wa kitanzania hawajajua maana ya zoezi hili. Wanadhani ni kazoezi ka kujifurahisha tu wakisubiri kocha awaite waendelee na mazoezi mengine ya maana. Ukifanyiwa pressing inabidi uwe na utulivu na ubunifu wa kujua jinsi ya kucheza na wenzio, hii ndiyo faida ya kwanza ya rondos.

Angalia timu kama Man City, Real Madrid au Barcelona ilee wamekuwa na wachezaji wenye ubunifu na utulivu wa aina hii. Rondo zao zinaweza kupigwa pasi hata 30. Angalia rondo zetu hata pasi 5 ni mtihani mkubwa.

Pia ukiona kuna ulazima wa kurudisha mpira kwa golikipa, walau basi rudisha mpira wa chini kabisa unaotambaa kwenye nyasi. Hili nalo mchezaji professional anahitaji akumbushwe?
 
Tatizo la back pass limekuwepo Simba muda mrefu, Mgunda alikuwa na falsafa ya ball litembee kulikuwa hakuna back pass.
Tangu Fadilu aje tatizo limekuwa kubwa na Kama sio umahili wa kipa Sasa hivi tungekuwa tumefungwa magoli ya namna hiyo zaidi ya 10.
Onyangi hakuwa na tatizo la back pass na hata makosa yake ni ama amezidiwa speed au kutoa penati.
Mavambo, Hamza, Kagoma, che Malone ni vinara wa back pass hata Mwenda wakati yupo Simba alikuwa na tatizo Hilo..
Katika hiyo mechi toka kipindi cha kwanza Simba walikuwa wakifika lango la adui wanarudisha mpira Hadi kwa kipa lakini Kama walienda mapumziko na wakarudia mfumo huohuo ni wazi ilikuwa mbinu ya kocha.
 
Huu uzi si wa kutetea upuuzi alioufanya Ladack Chasambi katika mechi ya jana kati ya Fountain Gate vs Simba. Huu uzi nia yake kuelezea maeneo mawili ambayo Simba imekuwa na tatizo nayo kwa muda mrefu. Nasisitiza, kosa moja halihalalishi makosa mengine.

Katika mechi kati ya Simba vs Yanga ambayo kipa alikuwa Ayoub Lakred (wenye kumbukumbu mtanikumbusha ni mechi ipi), Zimbwe alimrudishia Lakred mpira wa kasi na wa juu na bahati nzuri Lakred alikuwa na control nzuri akaweza kuuclear. Kosa la Chasambi halitofautiani sana na kosa hili. Kuna mchezaji mwingine juzijuzi aliwahi kumrudishia Camara mpira wa namna hii nadhani ni Che Malone. Hakuna ubaya kumrudishia kipa mpira, swali unarudisha mpira ulio na usalama gani kwa timu yako?

Turudi kwenye tatizo la msingi la Simba:
Ukweli ni kuwa tatizo la "backpasses" limekuwa sugu pale Simba. Wengi wanadhani tunaposema "backpass" ni mpaka mpira uende kwa kipa. Hamza akiupeleka mpira kwa Zimbwe unategemea tunaenda mbele, utashangaa naye anarudisha kwa Che Malone au anapiga pasi ya pembeni kwa Kagoma. Nahisi Kocha Mgunda ndiyo alililea hili tatizo, mchezaji kama Onyango alikuwa hapigi pasi ya mbele hata siku moja, ni ama atapiga pasi ya nyuma au ya pembeni.

Robertinho akaja akajaribu kulitibu kwa "direct football", kiasi alifanikiwa ila watu wakaanza kulalamika mpira wa "butua butua" ingawa mimi sikubaliani na lebo hiyo watu walioipa.

Tusimlaumu kocha Fadlu David kwa hili tatizo. Kabla Chasambi hajajifunga, alionekana kuwahimiza wachezaji wapeleke mpira mbele ila hawakumzingatia. Kabla ya goli alilofunga Kapombe kwenye mechi ya wiki iliyopita dhidi ya Tabora, Fadlu alionekana kuwahimiza wachezaji wapeleke mpira mbele maana walionekana kuchezea mpira eneo lao bila faida. Kwa hiyo tusiseme Fadlu ndiye anayewafundisha hili.

Sielewi kwa nini baadhi ya wachezaji wa Simba wakifanyiwa pressing wanapata kitete wanaona afadhali arudishe mpira nyuma kuliko kuupoteza. Hili lilikuwa tatizo sugu hadi mchezaji anaogopa kupoteza mpira hata akiwa zone ya adui. Mchezaji anaweza kutoka na mpira kwenye kona ya adui zikapigwa pasi kurudi nyuma hadi kwa golikipa wao. Wakati mwingine wakawa wanapeana pasi za kusakiziana ingawa hili tatizo naona limepungua sana.

Jinsi ya kulitatua hili tatizo:

Niliwahi kusema ni muhimu kuwarudisha wachezaji kwenye zoezi la "angaisha bwege" au kitaalam linaitwa "rondo" au "rondos" ambalo kwa mtazamo wangu wachezaji wengi wa kitanzania hawajajua maana ya zoezi hili. Wanadhani ni kazoezi ka kujifurahisha tu wakisubiri kocha awaite waendelee na mazoezi mengine ya maana. Ukifanyiwa pressing inabidi uwe na utulivu na ubunifu wa kujua jinsi ya kucheza na wenzio, hii ndiyo faida ya kwanza ya rondos.

Angalia timu kama Man City, Real Madrid au Barcelona ilee wamekuwa na wachezaji wenye ubunifu na utulivu wa aina hii. Rondo zao zinaweza kupigwa pasi hata 30. Angalia rondo zetu hata pasi 5 ni mtihani mkubwa.

Pia ukiona kuna ulazima wa kurudisha mpira kwa golikipa, walau basi rudisha mpira wa chini kabisa unaotambaa kwenye nyasi. Hili nalo mchezaji professional anahitaji akumbushwe?
Bado nitalaumu benchi la ufundi.Ni bora kubutua mpira mbele,au kutoa nje kuliko kurudisha mpira nyuma.

Kurudisha mpira nyuma unapaswa uwe na wachezaji wengi wenye ball control na nguvu ya kumiliki mpira ili ukuanzisha mashambulizi,usinyanga'anywe kirahisi mpira

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ni suluhu kila siku maneno siku ikitokea mkafungwa na ken gold lazima mtaua mtu .
 
Bado nitalaumu benchi la ufundi.Ni bora kubutua mpira mbele,au kutoa nje kuliko kurudisha mpira nyuma.
Goli alilosababisha Hussein Kazi kwenye derby alijaribu kupiga mbele mpira ukawa blocked Yanga ikapata goli. Ndiyo maana nasisitiza utulivu ndiyo unahitajika na wachezaji wajue jinsi ya kujiposition vizuri kupokea mipira kutoka kwa wenzao. Wapunguze kitete pale wanapofanyiwa pressing.

Mimi mchezaji kama Zimbwe akipokea mpira nimeshakariri atafanya nini kwa asilimia 90. Ataangaza mbele kama anatafuta mtu wa kumpasia ila atageuka na kumpa mchezaji wa nyuma yake au wa pembeni.
 
Tatizo la back pass limekuwepo Simba muda mrefu, Mgunda alikuwa na falsafa ya ball litembee kulikuwa hakuna back pass.
Tangu Fadilu aje tatizo limekuwa kubwa na Kama sio umahili wa kipa Sasa hivi tungekuwa tumefungwa magoli ya namna hiyo zaidi ya 10.
Onyangi hakuwa na tatizo la back pass na hata makosa yake ni ama amezidiwa speed au kutoa penati.
Mavambo, Hamza, Kagoma, che Malone ni vinara wa back pass hata Mwenda wakati yupo Simba alikuwa na tatizo Hilo..
Katika hiyo mechi toka kipindi cha kwanza Simba walikuwa wakifika lango la adui wanarudisha mpira Hadi kwa kipa lakini Kama walienda mapumziko na wakarudia mfumo huohuo ni wazi ilikuwa mbinu ya kocha.
Pitia goli alilojifunga Chasambi na lile alilofunga Kapombe mechi na Tabora utaona Fadlu alikuwa anawaambia wachezaji wapeleke mpira mbele.

Kocha kufundisha kuanza nyuma siyo kosa ila wachezaji wanasahau nia ya kufanya hivyo ni nini. Kama umeshavuta wachezaji wawili hadi watatu wa timu pinzani hiyo inatosha kupiga pasi ndefu. Inawezekana wachezaji wa mbele hawajiposition vizuri kiasi kwamba mabeki wanachelewa kupeleka mpira mbele maana hawaoni nani yupo kwenye nafasi nzuri.

Kuna tatizo lingine niliwahi kuligusia siku moja. Camara siyo mzuri kwenye kupiga mipira mrefu. Mipira yake mingi inaenda nje, inapitiliza hadi kwa golikipa wa upande wa pili au haiendi kwenye mchezaji aliye kwenye nafasi nzuri. Hii inarudi nilichosema kuwa labda wachezaji wa kati na mbele hawajiposition vizuri kuwapa nafasi mabeki na golikipa kuwapa mipira.
 
Ukiangalia vizuri ile video ya goli, Chasambi alidhamiria kutufunga...

Ile haikua pasi, maana Camara hakua golini mda huo na chasambi alikua na nafasi ya kupiga pass ya kumlenga kipa...

Lakini akapiga shuti ambalo alikua na hakika Camara hatolifikia, na hata ukiangalia body Language yake jinsi shuti lilivyokuwa linaenda utagundua alidhamiria kufunga...
 
Ukiangalia vizuri ile video ya goli, Chasambi alidhamiria kutufunga...

Ile haikua pasi, maana Camara hakua golini mda huo na chasambi alikua na nafasi ya kupiga pass ya kumlenga kipa...

Lakini akapiga shuti ambalo alikua na hakika Camara hatolifikia, na hata ukiangalia body Language yake jinsi shuti lilivyokuwa linaenda utagundua alidhamiria kufunga...
Hilo lililotokea wala halijanishtua saana. Wiki kadhaa zilizopita alivyotoa kauli ya Max kuna kitu nilikisema na kingine nikamezea.
 
Ukiangalia vizuri ile video ya goli, Chasambi alidhamiria kutufunga...

Ile haikua pasi, maana Camara hakua golini mda huo na chasambi alikua na nafasi ya kupiga pass ya kumlenga kipa...

Lakini akapiga shuti ambalo alikua na hakika Camara hatolifikia, na hata ukiangalia body Language yake jinsi shuti lilivyokuwa linaenda utagundua alidhamiria kufunga...
Kweli jema 99 hufutwa na kosa 1 tu, huyo huyo Chasambi anayeonekana kadhamiria kujifunga ndiye huyo huyo kaitafutia Simba goli la kuongoza kwa kuanzisha haraka mpira wa faulo haraka haraka wakati refa hakuamuru na wala ukuta haukuwekwa
 
Kabla Chasambi hajajifunga kuna goli haramu lilitangulia, lile lililofungwa na Ateba chini ya ushirikiano wa refa njaa fulani.

Anyway iko hivi Chasambi kafunga lile goli unconsciously... najua hata yeye huko aliko anajishangaa.

Ni MUNGU alimtumia Chasambi ili ujumbe ufike kwa mamlaka husika kwamba Uonevu michezoni haufai.

Wewe ulishaona wapi Own Goal ya aina ile....kwa Umbali wa zaidi ya Yards 40!

Haya sasa ikawa 1-1 dakika ya 75'
Baada ya hapo mpira si uliendelea.
Walifanya nini.
Kila mipango iliyoendelea baada ya hapo iliharibika katika mazingira ya kushangaza..
Kuna mpira uliwakuta Wachezaji wawili wa Simba wakiwa peke yao na kipa wakashindwa kufunga, tena mmoja wao akajikuta anaokoa shuti la mwenzake..
We huoni uhusika Mola.
 
Huu uzi si wa kutetea upuuzi alioufanya Ladack Chasambi katika mechi ya jana kati ya Fountain Gate vs Simba. Huu uzi nia yake kuelezea maeneo mawili ambayo Simba imekuwa na tatizo nayo kwa muda mrefu. Nasisitiza, kosa moja halihalalishi makosa mengine.

Katika mechi kati ya Simba vs Yanga ambayo kipa alikuwa Ayoub Lakred (wenye kumbukumbu mtanikumbusha ni mechi ipi), Zimbwe alimrudishia Lakred mpira wa kasi na wa juu na bahati nzuri Lakred alikuwa na control nzuri akaweza kuuclear. Kosa la Chasambi halitofautiani sana na kosa hili. Kuna mchezaji mwingine juzijuzi aliwahi kumrudishia Camara mpira wa namna hii nadhani ni Che Malone. Hakuna ubaya kumrudishia kipa mpira, swali unarudisha mpira ulio na usalama gani kwa timu yako?

Turudi kwenye tatizo la msingi la Simba:
Ukweli ni kuwa tatizo la "backpasses" limekuwa sugu pale Simba. Wengi wanadhani tunaposema "backpass" ni mpaka mpira uende kwa kipa. Hamza akiupeleka mpira kwa Zimbwe unategemea tunaenda mbele, utashangaa naye anarudisha kwa Che Malone au anapiga pasi ya pembeni kwa Kagoma. Nahisi Kocha Mgunda ndiyo alililea hili tatizo, mchezaji kama Onyango alikuwa hapigi pasi ya mbele hata siku moja, ni ama atapiga pasi ya nyuma au ya pembeni.

Robertinho akaja akajaribu kulitibu kwa "direct football", kiasi alifanikiwa ila watu wakaanza kulalamika mpira wa "butua butua" ingawa mimi sikubaliani na lebo hiyo watu walioipa.

Tusimlaumu kocha Fadlu David kwa hili tatizo. Kabla Chasambi hajajifunga, alionekana kuwahimiza wachezaji wapeleke mpira mbele ila hawakumzingatia. Kabla ya goli alilofunga Kapombe kwenye mechi ya wiki iliyopita dhidi ya Tabora, Fadlu alionekana kuwahimiza wachezaji wapeleke mpira mbele maana walionekana kuchezea mpira eneo lao bila faida. Kwa hiyo tusiseme Fadlu ndiye anayewafundisha hili.

Sielewi kwa nini baadhi ya wachezaji wa Simba wakifanyiwa pressing wanapata kitete wanaona afadhali arudishe mpira nyuma kuliko kuupoteza. Hili lilikuwa tatizo sugu hadi mchezaji anaogopa kupoteza mpira hata akiwa zone ya adui. Mchezaji anaweza kutoka na mpira kwenye kona ya adui zikapigwa pasi kurudi nyuma hadi kwa golikipa wao. Wakati mwingine wakawa wanapeana pasi za kusakiziana ingawa hili tatizo naona limepungua sana.

Jinsi ya kulitatua hili tatizo:

Niliwahi kusema ni muhimu kuwarudisha wachezaji kwenye zoezi la "angaisha bwege" au kitaalam linaitwa "rondo" au "rondos" ambalo kwa mtazamo wangu wachezaji wengi wa kitanzania hawajajua maana ya zoezi hili. Wanadhani ni kazoezi ka kujifurahisha tu wakisubiri kocha awaite waendelee na mazoezi mengine ya maana. Ukifanyiwa pressing inabidi uwe na utulivu na ubunifu wa kujua jinsi ya kucheza na wenzio, hii ndiyo faida ya kwanza ya rondos.

Angalia timu kama Man City, Real Madrid au Barcelona ilee wamekuwa na wachezaji wenye ubunifu na utulivu wa aina hii. Rondo zao zinaweza kupigwa pasi hata 30. Angalia rondo zetu hata pasi 5 ni mtihani mkubwa.

Pia ukiona kuna ulazima wa kurudisha mpira kwa golikipa, walau basi rudisha mpira wa chini kabisa unaotambaa kwenye nyasi. Hili nalo mchezaji professional anahitaji akumbushwe?
Huwezi kupita bila Wenye akili kukuunga mkono. Niliwahi kusema Back pass masters wako Simba na kiongozi wao ni Debora Mavambo. Simba inatumia Mudarefu mno kuhamisha shambulizi toka sehemu moja kwenda nyingine lakini majanga.
 
Upo sawa kabisa,kuna kocha alishawah tuelekeza katika mazoezi ya soka kuwa mpira ukisha fika katikati ya uwanja au karibu na katikati tufanye kila tunaloweza mpira uende mbele na sio kurudi nyuma,
Back passes kwa timu yetu ishakuwa tatizo hata faida yake bado ni ndogo maana inafikaga mahala wakirudisha kwa camara anabutua mbele bas,
Bado sijaona faida ya back passes wanazokuwa wanacheza zaidi ni hasara tu
 
Dogo aliturn afu aka'curve... Ni bahati mbaya ya kiwango cha juu
 
Kuna dogo mwingine wa Morogoro aliwahi kutoa pasi kwa thaban kamusoko kwenye derby...

Naye alijifanya ni bahati mbaya ila ilikuja kujulikana amepewa pesa...

Wachezaji wa kitanzania ni tatizo sana, wengi hawajitambui.
 
Kuna dogo mwingine wa Morogoro aliwahi kutoa pasi kwa thaban kamusoko kwenye derby...

Naye alijifanya ni bahati mbaya ila ilikuja kujulikana amepewa pesa...

Wachezaji wa kitanzania ni tatizo sana, wengi hawajitambui.
Kwa hiyo kapewa pesa na hakuna aliyeshitakiwa kwa upangaji wa matokeo?
 
MLEZI WA TATIZO LA BACK PASSES NI COACH FADLU DAVIDS HAIWEZEKANI TIMU KILA MECHI INAPIGA BACK PASSES HALAFU COACH HAUCHUKUI HATUA YOYOTE UNASHIKA KIUNO TU.
 
Back
Top Bottom