Anasema alikuwa hamjui Bashite ila sasa kamjua na anampenda sana.
Nakuuliza wewe Wema umemjua Bashite kwa vile unataka ufutiwe kesi. Kwanini upoteze utu wako kwa tamaa ya pesa.
Mbona akina Lulu wako gerezani, mbona akina Winnie Mandela walifungwa. Unashindwa hata kushauriana na mzazi wako. Mpaka mama analalamika kwenye vyombo vya habari.
Wakati kesi ilipokuwa hot mama hakulala kwa ajili yako. Na alisema ulimwambia BASHITE anakutaka.
Nakukuuliza tena. Hivyo leo umekubaliana na BASHITE?? Wema washukuru CHADEMA kwani bila akina Lisu, Kibatara. Bashite angekufunga na leo hii usingekuwa unayaongea hayo.
Bashite alishindwa kukufunga baada ya magwiji wa sheria kuingilia kati kesi yako. Ndio maana ukawa nje hadi leo unamkumbatia BASHITE. Sikiliza haya maneno yako