Alichonifanyia Trafiki huyu sitasahau

Alichonifanyia Trafiki huyu sitasahau

Post jina lake humu tuwapatie PCCB Makao Makuu watamfuatilia.
Cc; RPC Mwanza
Jana natoka zangu nyumbani nikiwa nimefunga mkanda wangu wa gari kama kawaida kwa ajili ya usalama wangu barabarani. Nimeendesha gari mpaka eneo la buzuruga stand iliyopo Nyakato Mwanza nikamuacha mwenzangu niliyekuwa naye ndani ya gari yangu.

Nikaondoka kupitia njia ya kutoka Buzuruga Stand kuelekea Kilimahewa ile nafika maeneo ya Sabato Darajani nikasimamishwa na na trafiki jina ninalo. Kisha kasogea kwenye gari yangu akaniomba leseni yangu na kuniuliza unajua kosa lako nikasema hapana.

Akasema kosa lako hujafunga mkanda wa gari na hapo toka nyumbani kwangu sijafungua mkanda kutoka kifuani kwangu nikamwambia askari mbona toka nyumbani kwangu sijafungua mkanda akasema ngoja nikuoneshe kuwa nina mamlaka kiukweli aliniandikia faini ya elfu thelathini kwa uonevu mkubwa lakini pia iliniuma sana nikajiuliza kumbe hata trafiki anaweza kukubambikia kosa niliumia sana mpaka leo sijasahau.

Na hapa nilipo nina deni la elfu thelathini la uonevu ninalotakiwa kulipa ndani ya wiki. Ndugu matrafiki hata kama mnapata bonasi kwenye hizo faini mnazotupiga kwa kutubambikia makosa Kwaresma hii mbadilike. Ushauri wenu faini sijailipa bado inaniuma sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole Mkuu mimi Imenitokea Wiki iliyopita ila Mimi nilimpa Mtu Lift wakati tu Anaingia kwenye Gari Trafic Akatokea Akaniandikia hapo hapo Faini Lengo La kuandika hapa Nakushauli Nenda Kalipe hilo deni Fastaaa Mimi nilikaa Siku tatu Sijalipa niliandikiwa Elfu Therethini Imagine nakwenda kulipa Eti imepanda imekuwa Elfu therathini na Saba na Mia Tano Hata Lisit ya Malipo ninayo hapa Sema Siwezi iweka kalipe Fasta Please.
Jana natoka zangu nyumbani nikiwa nimefunga mkanda wangu wa gari kama kawaida kwa ajili ya usalama wangu barabarani. Nimeendesha gari mpaka eneo la buzuruga stand iliyopo Nyakato Mwanza nikamuacha mwenzangu niliyekuwa naye ndani ya gari yangu.

Nikaondoka kupitia njia ya kutoka Buzuruga Stand kuelekea Kilimahewa ile nafika maeneo ya Sabato Darajani nikasimamishwa na na trafiki jina ninalo. Kisha kasogea kwenye gari yangu akaniomba leseni yangu na kuniuliza unajua kosa lako nikasema hapana.

Akasema kosa lako hujafunga mkanda wa gari na hapo toka nyumbani kwangu sijafungua mkanda kutoka kifuani kwangu nikamwambia askari mbona toka nyumbani kwangu sijafungua mkanda akasema ngoja nikuoneshe kuwa nina mamlaka kiukweli aliniandikia faini ya elfu thelathini kwa uonevu mkubwa lakini pia iliniuma sana nikajiuliza kumbe hata trafiki anaweza kukubambikia kosa niliumia sana mpaka leo sijasahau.

Na hapa nilipo nina deni la elfu thelathini la uonevu ninalotakiwa kulipa ndani ya wiki. Ndugu matrafiki hata kama mnapata bonasi kwenye hizo faini mnazotupiga kwa kutubambikia makosa Kwaresma hii mbadilike. Ushauri wenu faini sijailipa bado inaniuma sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi karibuni matrafic wamekuwa hush na waonevu sana na wenye magari, yaani kosa dogo la kuelekezana yeye anakimbilia kukuandikia faini, au hata kukubambikia kosa, me issue km Hy ilinikuta, sema nilikomaa akaona noma, ni wizi wa wazi kbs. Sjui ni nini kinachoendelea kwa hv sasa aisee.

Nahisi Labda hii miradi mikubwa inayoendelea nchini ambayo tunaifanya kwa pesa za ndani Labda itakuwa inachangia Hilo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyie mnaocomment humu mbona hampo makini?

Jamaa kaandika mwenyewe Tena karudia Mara mbili kuwa tokea ametoka nyumbani hajafunga mkanda na trafik alkuwa anamlazimisha kuwa jamaa kafunga mkanda haujafika kifuani ilihali jamaa mwenyewe alkua hajafunga kabisa mkanda tokea ametoka nyumbani kwake.
 
Back
Top Bottom