Aliye Juu Mngoje Chini ! ??

Goodrich

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2012
Posts
2,091
Reaction score
1,178
Tangu nilipokuwa shule, mara ya kwanza kusikia msemo Aliye juu mngoje chini nilitatizika sana.
Sikuelewa mtunzi wa msemo huu alikuwa na kinyongo, wivu au kukata tamaa.
Hata hivyo niliishia kuamini kuwa muasisi wa msemo huo alijikubali kuwa yeye ni wa daraja la chini siku zote.

Nadhani msemo ungependeza kama ungekuwa;
Aliye Juu Mfuate Juu au
Aliye Juu Muulize Kafikaje nawe ufike Juu.

Sijui wenzangu mnaonaje?
 
Yaani kuntu kabisa, Alie juu mfuate huko huko juu, au mie huwa nina mawazo mengine kama mtu anakuudhi sana , ana madharau kwa kuwa anajiona yeye matawi ya juu basi huwa nasema ALIE JUU NITAKUTANA NAE KATI KATI WAKI YEYE ANASHUKA MIMI NAPANDA... lakini hii mara nyingi huwa inatokea kama mtu yupo juu anakuvuruga na kukutolea dharau other wise ALIE JUU MUOMBEE MUNGU AMZIDISHIE NA WEWE AKUPE ZAIDI.
 

He was right, why should you waste resources for something that nature/somebody/(somewhere) will provide it for free
 
He was right, why should you waste resources for something that nature/somebody/(somewhere) will provide it for free

Kwa hiyo umekaa chini unamsubiri. Fanya kazi, uwe kama yeye !
 
Be Nice to the People on your way up as you might meet them on your way down
 
Thats the problem. You are focused on the way down !!!
 
Mh...msemo huu ulikuwa fundisho kwa wale waliopata madaraka ulani na wanayatumia vibaya/kuumiza wenzao.
Hivyo, ni kumbusho tu kwa wale wanaoonewa (waliochini) kwa usihangaike kumloga, kumkaidi, kupoteza muda wako kujaribu kumshusha..,mwisho wa siku atarudi chini tu kwani wazungu wanasema, "Corruption may take you to the top, but it takes character to keep you there"
Haimanishi, ukae chini unamgoja ashuke halafu basi. Kwani pia walisema, "mvumilivu hula mbivu" na "mchumia juani hulia kivulini" endelea kuchumia huko juani kwani ama kwa hakika wakati atakaposhuka, Mungu atakupandisha kwa halali...
 
safi huo ni mtazamo wako mzuri sana, lakini tambua kuwa hiyo ni methali na methali huwa na lugha ficho iliyobeba hekima ndani yake katika lugha ya kiswahili kuna maana mbali mbali kwa baadhi ya maneno au sentensi kuna maana ya msingi na ile ambayo mzungumzaji huibaini, maana halisi ya aliyejuu ................ ni kwamba mfano watu wawili wenye nguvu wanapigana basi mmoja lazma ashuke/awe mpole kuepusha utata zaidi, hivyo ashuke na kumsubiri ashuke (apunguze hasira wataelewana)
Haya ndio maono yangu wewe Je?
 

ndugu yangu hiyo ni misemo ya hekima na tunu ya lugha yetu adhimu ya kiswahili, tafsiri yake si ya moja kwa moja kama wengi wanavyofikiri ipo mingine mingi tu kama chelewa ufike,fimbo ya mbali,mtaka cha uvunguni, asifiaye mvua ,nk nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…