Uchaguzi 2020 Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Manyovu, Albert Obama akamatwa na TAKUKURU kwa kugawa Rushwa

Mbona watia nia wa ccm wanakamatwa sana kwa kutoa rushwa? Kuna kitu gani kinaendelea jamani?
Ipo hivi,wale wote ambao mkulu hawataki ndio wamekuwa walengwa,na hii imeshatolewa list kabisa. Hutasikia TAKUKURU ikikamata Dk. Mpango,Prof. J. Ndalichako,Prof. Kabudi, na wengineo wanakuwa "backed up" na mukulu.
 
Mkuu watu wanakamatwa na vidhibiti kabisa unasema ni njama kweli.?
Mkuu idawa ,huo ndio ukweli. CCM wote ni watoa rushwa,ila kama haupo upande wa mukulu,na yeye ana mtu anayemuhitaji unapambana naye,kifuatacho ni kutumia fimbo hiyo ya TAKUKURU.
 
Watoa rushwa hawawezipita.majina yao yapo.wanadhani CCM ya sasa ni ile ya zamani.
 
Ngoma Ikilia Sana Mwishowe Hupasuka!!!
 
Majuto ni mjukuu mkono shavuni,na mpunga wenyewe hadharani
 
Majuto ni mjukuu mkono shavuni,na mpunga wenyewe hadharani
Kwanini wanaokamatwa na rushwa ni ccm tu, shangaa et TAKUKURU wanaikomalia chadema kwa matumizi mabaya. Na ukitaka kujua kuwa wako juu ya sheria yataisha kimya kimya, hivi bado mnamkumbuka aliyekamatwa na rundo la bunduki ?. Shangaa wakiambiwa wanafanya biashara ya kununua madiwani na wabunge wanakuja juu. Hawa jamaa hawana uwezo wa kushawishi zaudi ya kununua na porice
 
Hili Bunge limejaa wabunge maskini sana na ccm imejaa watu wenye njaa zisizoelezeka.

Hivi kweli inaingia akilini mbunge unatoa rushwa ya shilling 10000/= kweli !!!!

Wajumbe wa ccm nao wanauza maisha ya wananchi miaka mitano kwa shillingi 10000/= !!!!!!.

πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Kwa nini utoe rushwa kama.unaamini umeitendea haki.nafasi yako?
Halafu linatoa 10,000 halionekani tena hadi 2020.ajiandae tu kulima chikichi
 
TAKUKURU (M) Kigoma imemkamata aliyekua Mbunge wa Bihigwe (CCM) Albert Ntabaliba maararufu kama Obama, kwa tuhuma za kugawa rushwa kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa jimbo kata ya Mnanila. TAKUKURU pia imekamata wajumbe 21 ambao kila mmoja alikua amegawiwa rushwa ya TZS 10,000/= na Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Buhigwe kwa maelekezo ya Obama.

Aidha mbunge huyo amesalimisha kwa maafisa wa TAKUKURU kiasi cha TZS 2,000,000/= alizokutwa nazo wakati akiendelea na kikao hicho ambazo zinadaiwa kulenga kuwahonga viongozi wilaya wa chama hicho. Katika jimbo hilo Obama anachuana na makada wenzie 17 akiwemo Waziri wa fedha Dr.Philip Mpango, ambapo mmoja wao atapewa nafasi ya kugombea ubunge kupitia chama hicho.!
 
Hio ni nafasi ya bwana Mpango, na huyu Dr. Atafute kazi nyingine. Wana CCM sijui kwa nini wanaamini katika rushwa kuliko kitu chochote!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…