Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu TPA, Deusdedit Kakoko aachiwa kwa dhamana baada ya TAKUKURU kukamilisha Uchunguzi dhidi yake kwa 98%

Hivi kwa nini nyinyi wabongo mnafurahia sana wenzenu waliwazidi nafasi kidogo wafungwe tu hata kama haijathibitika kama tuhuma zinazowahusu ni za kweli?
Mnamtia hatiani mtu kabla haijathibitika bila shaka yoyote kwamba katenda jinai, hizo roho zenu mbaya zitawafikisha wapi?
Kuna tatizo kwenye mifumo, kuna mianya inayosababisha baadhi ya watu wasio waaminifu kushiriki vitendo vya wizi, mianya hiyo haina budi kuzibwa ili fedha ya umma ibaki salama.
 
Kesi ya uhujumu uchumi kwa wengine haina dhamana ila wengine dhamana ipo...double standard

Hii kesi imeshaisha tàyari wameona upigaji uliofanyika mpaka Hayati kapiga hiyo pesa
 
Swadakta kabisa mkuu, na hii ni issue ya kimfumo zaidi kwenye nchi zinazojitambua, ambapo utakuta hapa ndio idara za usalama hufanya kazi kubwa kwa maslahi mapana ya taifa. Na ili kuepusha nchi kuongozwa na mtu ambaye hakutarajia kuwa Rais, endapo Rais aliyepo atashindwa kuendelea na majukumu yake au kufariki, basi watarudi kwenye uchaguzi mkuu. Sijui kwanini Tz hatukurekebisha hii sheria!!!
 
Kwani DPP anashindwa nini kusema kesi ipo au hakuna? 2% inachukua miaka mingapi ? Wengi walio jela sasa wanasubiria DPP consent mbona hawapati dhamana ? Why Kakoko? Au Mama nae anaogopa akitoka watu wake kusumbuliwa bila msaada ? Mfumo wa kulindana ....kama nyuma kuna mtu mwenye kinga?
 
Magufuli aliupata uRais kwa Zali/hakujiandaa. Samia naye ameupata Urais kwa zali pia, hakujiandaa.
Tuendapo ni Mungu anajua.
Wanaojiandaa wanakuwa wabaya sana kwani ni wanasiasa wenye kutegemea kundi kubwa la watu. Huwa wameshatengeneza mgawanyiko kabla hata hawajaapishwa.
 
Wanaojiandaa wanakuwa wabaya sana kwani ni wanasiasa wenye kutegemea kundi kubwa la watu. Huwa wameshatengeneza mgawanyiko kabla hata hawajaapishwa.
Kikwete ni jibu sahihi(?)...; ni kama nauliza huku nikitoa mfano halisi!

Lakini niseme hapa, siyo wote; na hata kama wakiwa na "kundi kubwa la watu" kwamba viongozi hao hawawezi kuongoza vizuri kwa kutumia maono yao.
Kuwa na kundi/makundi ni lazima kwenye siasa, na sio lazima hayo makundi yawe ni kwa ubaya/upigaji tu.

Kiongozi mzuri ataunda kundi la watu wanaokubaliana na maono na matarajio yake juu ya anayotaka kuyafanya akiwa kiongozi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…