Aliyenishauri niingie kwenye kilimo cha parachichi hapa Njombe aliniingiza chaka, nimepoteza fedha na muda

mwanyaluke

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2015
Posts
704
Reaction score
2,435
Nimekuwa mkulima wa parachichi kwa miaka mingi, lakini sijawahi kuona pesa inayosemekana ipo kwenye zao hili. Kila mwaka nakutana na sababu zile zile za changamoto za soko.

Baada ya kutafakari kwa muda mrefu, nimeamua rasmi kufyeka parachichi na kubadilisha mwelekeo wa kilimo changu. Nitatumia ardhi hiyo kufuga ng’ombe na mbuzi, huku nikibaki na kilimo cha viazi ambacho kimekuwa na faida kwangu.

Kwa wasiojua, nimewekeza sana kwenye kilimo cha parachichi. Shamba langu lipo vizuri, nimetumia mbolea za asili na chumvi, nimefanya installation ya mfumo wa umwagiliaji, na kutumia madawa kama boron na copper, pamoja na booster zinazotumika hata na wakulima wa Afrika Kusini. Pamoja na juhudi hizo zote, bado sijapata mafanikio niliyotarajia.

Nimeangalia pia maisha ya wakulima wenzangu—labda wao wananufaika, lakini kwangu hali ni tofauti. Naamini tatizo kubwa lipo kwenye soko la parachichi nchini Tanzania. Serikali imeweka tozo nyingi ambazo zinadhoofisha biashara hii, na wanaofaidika zaidi ni madalali kutoka Kenya.
 
Pole sana mkuu umefanya kwa muda gani?
 
Sijui kama naweza ni kaamini kwamba kilimo kinawexa kunitoa ki maisha kilimo kinatoa wale walio toka kimaisha kitambo wenye mitaji mikubwa isio pungua 100m kwa 1bn, ila wenye vihera vya kuungauga kilimo ni hateri sanaa kukumaliza, mkulima ntafanya kilimo kama pastime ila sio kibiashara.
 
pole sana mkuu mafanikio sio rahisi kwenye sehemu zote jipange upya na utambue wapi ulikosea ili urekebishe sikushauri uache hiyo kazi bali utambue mapungufu na ujipange upya jifunze kupitia makosa ufanikiwe ukiingia kwenye issue nyengine kwa sasa ni sawa na kuanza moja tu,
 
Nasita kukuamini katika hili kwa sababu zifuatazo:

1. Hujaelezea hali halisi ya kilimo chako ikiwemo management hadi sokoni, hii inatia shaka kwamba huna taarifa hizo


2. Hujaelezea changamoto za awali ulipo anza, ulipo zoea na mwishoni unapo ghairi kuendelea


3. Hujaelezea mikakati uliyochukua kutatua changamoto husika na zikashindikanika kutatua...mfano hapo nimeona umesema tozo za serikali na madalali wa kenya, je tozo ni kiasi gani kwa kilo ww unavuna kilo ngapi na usione faida. Je dalali Mkenya anakuaje dalali njombe umejaribu kulifikia soko direct ili mzigo wako usioite kwa dalali ikashindikana?


4. Parachichi huku mtaani ni moja ya tunda bei iko juu sana na kwa sasa ni machache, parachichi doogo ni 300, kisha 500, 700 hadi 1000 kwa eneo nilioo sio mjini ni mbali nje na mji wa halmashauri.

Kwa sababu hizo hapo juu nachelea kusema thread yako haina ukweli na kama ina ukweli basi ww huna usimamizi wa karibu na project zako, unatumia sana simu kupata taarifa na kutoa maelekezo kwa vijana au wasimamizi na kuishia kuona hasara kila mara.

"THE BEST INVESTMENT katika biashara au project yako ni KITI chako cha kukali"

Best investmnt in your business is your chair (uwepo wako kila mara).

Alamsiki Amigo...
 
Hata kwa mtaji mdogo unatoka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…