Aliyetaka kushindana na Ndugai aenguliwa, yeye si mbunge

Aliyetaka kushindana na Ndugai aenguliwa, yeye si mbunge

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema amemuengua Bonaventura Peter Ndekenja wa chama cha NRA aliyemtumia baruapepe akieleza nia yake ya kutaka kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye si mbunge.

“Yeye si mbunge hivyo chama chake kilipaswa kuwasilisha jina lake Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuthibitisha kama anakidhi vigezo vya kuwa mbunge. Kwa kutofanya hivyo, ndugu Ndegenja amekosa sifa,” amesema Kagaigai.

Sababu nyingine iliyomwondoa mtiania huyo aliyeamua kujaribu bahati yake, Kagaigai amesema baruapepe yake ilimfikia saa 12 jioni badala ya saa 10 jioni, muda wa mwisho kuwasilisha maombi ya kuwania uspika.

Alipopewa muda wa kujieleza mbele ya wapiga kura wake, Ndugai anayewakilisha Jimbo la Kongwa amesema atatenda haki kwa kila mbunge katika uongozi wake.

Jumla ya wabunge 263 wamepewa karatasi za kupiga kura ama kumchagua au kumkataa Ndugai kuwa mkuu wa mhimili huo wa dola.

Ndugai anapigiwa kura kuwania muhula wa pili wa kuliongoza Bunge hilo huku akiwa na uzoefu wa kuwa Naibu Spika kwa muhula mmoja pia.
 
Kigezo cha kuwa qualified kuwa member of parliament ni kipi zaidi ya kujua kusoma na kuandika?

Wamempendelea Ndugai, wanaogopa ushindani kama kawaida yao.
 
Mkuu huo siyo mkutano wa Bunge Bali Ni makada wa CCM wanaendelea na shughuli zao Bungeni.

Tegemea baada ya zoezi la Kura kumalizika Job ndugai na Tulia ackson Wamepitishwa kwa mpitisho wa kishindo.

#Tanzania ya Kijani.
 
Bunge la gizani.

Hivi safari hii mtaonyesha bunge live jinsi mnavyopitisha sheria kandamizi na kupiga mapambio kwa 'malaika mkuu.'?
 
Supika sio lazima awe mbunge!
Ni kweli Spika si lazima awe mbunge, ila kama anayegombea nafasi hiyo si mbunge kuna utaratibu wa kufuata, chama chake kinapeleka jina lake NEC ili wajiridhishe kama ana sifa za kuwa mbunge ndio NEC waliidhinishe jina lake kugombea uspika.

Kwa maelezo hayo hapo juu, huyu mtu hakutimiza sharti hilo kama ilivyodaiwa na bwana Kigaigai mbali na kuwa maombi yake yalifika nje ya muda ulioruhisiwa.
 
Ni kweli Spika si lazima awe mbunge, ila kama anayegombea nafasi hiyo si mbunge kuna utaratibu wa kufuata, chama chake kinapeleka jina lake NEC ili wajiridhishe kama ana sifa za kuwa mbunge ndio NEC waliidhinishe jina lake kugombea uspika.

Kwa maelezo hayo hapo juu, huyu mtu hakutimiza sharti hilo kama ilivyodaiwa na bwana Kigaigai mbali na kuwa maombi yake yalifika nje ya muda ulioruhisiwa.

Sifa ya kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika, hayo mengine kuhusu muda wa maombi ni porojo.... lengo ni 'bila kupingwa' hata kama mteule angepata kura zote.
 
Itoshe tu kusema kuwa NRA walikwishatumiwa na CCM wakati wa uchafuzi mkuu - kuwawekea mapingamizi wapinzani wa kweli. Sasa watawala wamekwishapata walichokuwa wanatafuta, NRA hawahitajiki tena. Ni mpaka 2025! NRA watulie sasa. Hawahitajiki tena.
Ni kweli Spika si lazima awe mbunge, ila kama anayegombea nafasi hiyo si mbunge kuna utaratibu wa kufuata, chama chake kinapeleka jina lake NEC ili wajiridhishe kama ana sifa za kuwa mbunge ndio NEC waliidhinishe jina lake kugombea uspika.

Kwa maelezo hayo hapo juu, huyu mtu hakutimiza sharti hilo kama ilivyodaiwa na bwana Kigaigai mbali na kuwa maombi yake yalifika nje ya muda ulioruhisiwa.
 
Ni kweli Spika si lazima awe mbunge, ila kama anayegombea nafasi hiyo si mbunge kuna utaratibu wa kufuata, chama chake kinapeleka jina lake NEC ili wajiridhishe kama ana sifa za kuwa mbunge ndio NEC waliidhinishe jina lake kugombea uspika.

Kwa maelezo hayo hapo juu, huyu mtu hakutimiza sharti hilo kama ilivyodaiwa na bwana Kigaigai mbali na kuwa maombi yake yalifika nje ya muda ulioruhisiwa.
Sikuona sababu ya msingi ya kumuengua, nadhani kuna tatizo kubwa sana la kuogopa ushindani sijui kwa nini,maana wao ndiyo majority bungeni lakini bado wanaogopa ushindani!!
 
Tujiandae kuona ushenzi katika kiwango cha juu.
 
Wa sisiem majimboni 264 na viti maalum sisiem 94, CDM 19. CUF sijui 3??

Sio kweli mkuu umechanganya idadi na hata jana nilisikia Jiwe mwenyewe akijichanganya kuhusu wabunge wake
Majimbo Tanzania Bars 214
Pemba 18
Unguja 32
Jumla ya majimbo yote ndo 264
CCM imeshinda majimbo 256 tu
Chadema jimbo 1
ACT Wazalendo majimbo 4
na CUF majimbo 3)
Halafu viti maalum CCM 94 na Chadema 19
 
Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema amemuengua Bonaventura Peter Ndekenja wa chama cha NRA aliyemtumia baruapepe akieleza nia yake ya kutaka kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu yeye si mbunge.

“Yeye si mbunge hivyo chama chake kilipaswa kuwasilisha jina lake Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuthibitisha kama anakidhi vigezo vya kuwa mbunge. Kwa kutofanya hivyo, ndugu Ndegenja amekosa sifa,” amesema Kagaigai.

Sababu nyingine iliyomwondoa mtiania huyo aliyeamua kujaribu bahati yake, Kagaigai amesema baruapepe yake ilimfikia saa 12 jioni badala ya saa 10 jioni, muda wa mwisho kuwasilisha maombi ya kuwania uspika.

Alipopewa muda wa kujieleza mbele ya wapiga kura wake, Ndugai anayewakilisha Jimbo la Kongwa amesema atatenda haki kwa kila mbunge katika uongozi wake.

Jumla ya wabunge 263 wamepewa karatasi za kupiga kura ama kumchagua au kumkataa Ndugai kuwa mkuu wa mhimili huo wa dola.

Ndugai anapigiwa kura kuwania muhula wa pili wa kuliongoza Bunge hilo huku akiwa na uzoefu wa kuwa Naibu Spika kwa muhula mmoja pia.
HAPA nakubali mgombea uspika ambae sio mbunge lazima chama kupeleka jina nec ,theni nec inatoa barua yakumkubali kabla ya hatua zingine kufuata
 
Back
Top Bottom