Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Hamjambo wote!
Kuna watu wanafurahisha Sana.
Ati wanamshangaa na kumsimanga Azizi Ki kwa kutoa Mahari 30m na Ng'ombe 30 na kumshutumu na kumkejeli kwamba ni mshamba sijui kanunua gazeti la Juzi, sijui ganda la Muwa la Jana, oooh! Jamaa kaoa single mother kwa gharama kubwa. Yaani blah blah!
Sisi Watibeli hatuoni tofauti yoyote ya Mtu aliyetoa Mahari Milioni 30 au Milioni 100 na Yule ambaye ametoa Mahari ya Laki Nane. Wote ninyi mpo kundi Moja.
Wakati Mnamshangaa mwenzenu kwa kutoa Milioni 30 Sisi Watibeli ndio tunashangaa zaidi kwa nini mnatoa hizo Mahari. Kwa kweli ni Moja ya mambo ambayo yanawafanya wanadamu wawe viumbe wenye Vioja.
Mwanamke yeyote aliyetolewa Mahari bila kujali nafasi yake. Ni binadamu aliyethaminishwa kama bidhaa Fulani.
Mtu hatolewi MAHARI
Mtu hajawahi kutolewa MAHARI
Na ndio maana wanaume wengi hawatolewi MAHARI kwa Sababu wao ni WATU.
Mahari ni biashara ya kumnunua binadamu mwingine ili aje awe chini ya Miliki yako.
Wenyewe watoa Mahari ukiwaambia kuwa wanafanya biashara ya kuuza na kununua binadamu wakike. Wanakukatalia. Sio biashara
Alafu Muda huohuo ukienda kutoa Mahari(kununua mwanamke) utasikia wakijadili thamani ya huyo Mwanamke.
Ooh! Binti yetu ni mweupe! Mzuri na tumemlea vizuri.
Tumemsomesha hivyo utatoa Milioni tano.
Alafu vile vianamke visivyo na mvuto wowote vitauzwa hata kwa Laki Tatu au Milioni Moja. Kwamba vina thamani ndogo ukilinganisha na wale mabinti warembo wenye rangi yenye kuvutia machoni au Waliosoma na kuwa na elimu Kubwa.
Ukiwauliza wanaokataa Hamisa Mobeto kwa nini asitolewe hiyo Milioni 30 na Ng'ombe 30 Sababu wanazotoa utagundua ni Kwa nini Watibeli hatutoi Mahari na Wala Binti zetu hawatolewi MAHARI(hawauzwi)
Sio HAKI kuuza binadamu Wala sio HAKI kununua binadamu lakini sio HAKI ikiwa binadamu hao wanautu ndani Yao.
Haya ngoja tuendelee kushangaana
Kuna watu wanafurahisha Sana.
Ati wanamshangaa na kumsimanga Azizi Ki kwa kutoa Mahari 30m na Ng'ombe 30 na kumshutumu na kumkejeli kwamba ni mshamba sijui kanunua gazeti la Juzi, sijui ganda la Muwa la Jana, oooh! Jamaa kaoa single mother kwa gharama kubwa. Yaani blah blah!
Sisi Watibeli hatuoni tofauti yoyote ya Mtu aliyetoa Mahari Milioni 30 au Milioni 100 na Yule ambaye ametoa Mahari ya Laki Nane. Wote ninyi mpo kundi Moja.
Wakati Mnamshangaa mwenzenu kwa kutoa Milioni 30 Sisi Watibeli ndio tunashangaa zaidi kwa nini mnatoa hizo Mahari. Kwa kweli ni Moja ya mambo ambayo yanawafanya wanadamu wawe viumbe wenye Vioja.
Mwanamke yeyote aliyetolewa Mahari bila kujali nafasi yake. Ni binadamu aliyethaminishwa kama bidhaa Fulani.
Mtu hatolewi MAHARI
Mtu hajawahi kutolewa MAHARI
Na ndio maana wanaume wengi hawatolewi MAHARI kwa Sababu wao ni WATU.
Mahari ni biashara ya kumnunua binadamu mwingine ili aje awe chini ya Miliki yako.
Wenyewe watoa Mahari ukiwaambia kuwa wanafanya biashara ya kuuza na kununua binadamu wakike. Wanakukatalia. Sio biashara
Alafu Muda huohuo ukienda kutoa Mahari(kununua mwanamke) utasikia wakijadili thamani ya huyo Mwanamke.
Ooh! Binti yetu ni mweupe! Mzuri na tumemlea vizuri.
Tumemsomesha hivyo utatoa Milioni tano.
Alafu vile vianamke visivyo na mvuto wowote vitauzwa hata kwa Laki Tatu au Milioni Moja. Kwamba vina thamani ndogo ukilinganisha na wale mabinti warembo wenye rangi yenye kuvutia machoni au Waliosoma na kuwa na elimu Kubwa.
Ukiwauliza wanaokataa Hamisa Mobeto kwa nini asitolewe hiyo Milioni 30 na Ng'ombe 30 Sababu wanazotoa utagundua ni Kwa nini Watibeli hatutoi Mahari na Wala Binti zetu hawatolewi MAHARI(hawauzwi)
Sio HAKI kuuza binadamu Wala sio HAKI kununua binadamu lakini sio HAKI ikiwa binadamu hao wanautu ndani Yao.
Haya ngoja tuendelee kushangaana