Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Vijana NCCR Mageuzi aliyeripotiwa kupotea aokotwa Porini akiwa Mahututi

Kama Magufuli wakati wake hakufanya hayo matendo kwa mkono wake lakini akalaumiwa, kwanini huyu wa sasa nae asilaumiwe?
Kipi cha kuwachochea au kuwashawishi watu kufanya hivyo? Watu wana hasira na Magufuli na wanachukizwa nae kuliko wanavyochukia hayo maovu yake wanayoyarudia kila siku.
 

Mamlaka za uchunguzi na ukamataji zilizo mikononi mwenu zikashindwa kufanya lolote? Au nani aliwajibishwa Kwa kushindwa kuwajibika?

Mengine haya waambieni ndege.
 
Tatizo nikuwa watanzania wana macho ya kumuona raisi lakini hawaii akunaga mwanasiasa msafi masikni yake magufuri mlimpaka kila aina ya uchafu na bado mnaendelea kwakua awa wana siasa wengine ni malaika naona ni mzimu wa magu bado unateka watu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hamjui siasa nyie
 
Kwani wewe unatakaje
Nataka Samia nae awajibike kwenye uongozi wake kama ilivyokuwa kwa Jiwe, mauwaji yoote na kila utekaji katika awamu ya tano tuliambiwa ni Jiwe kila makosa ya serikali tuliambiwa ni Jiwe hivyo na Samia nae iwe hivyo sio kwamba kwenye mazuri ndio anasifiwa Samia ila makosa na mabaya Samia hahusiki. Sasa huyo Samia amekuwa Mungu kwamba kazi zake hazina makosa?
 
Maisha yenyewe haya yamesha tuteka tayali mbona niku uana sasa huko kheeeeeeeeh 🤔🤔🤔🤔
 
Vipi wale vijana waliopotea pale Kariakoo Samia vipi hahusiki hapo? N vipi yule askofu mstaafu wa Angalikani Mwanza alipatikana amefariki na mwili wake kutubwa ziwani Samia hahusiki? Nyinyi ni kikundi cha wapuuzi tu matukio yako miaka y
wabongo bana..we unawajua wale vijana walikua nan
 
Wewe ndo utuambia maana kazi zenu kushabiki ujinga wa serkali hii kwa kila jambo!
ndio nakuambia sasa sio kila jambo ulete ushabiki wa kisiasa..hujui wale wat ni kina nan .wako wapi na kwa sababu gani.na sio kila mtu humu ni mshabiki wa u ccm na uchadema ..huo ujinga wengine hatujabarikiwa
 

Viongozi wa upinzani waue wanachama wao kisha serikali iwakalie kimya. Kama wanawabambikizia kesi, ingekuwa wamefanya hivyo kweli si ndio ilikuwa sehemu ya kufanya kweli?
 
Haya ruksa kamuwajibishe sasa. Tatizo tunaposema kuwa tunahitaji Katiba Mpya nyie mnabeza kuwa hilo takwa la Chadema wala siyo la Watanzania,mnasema wananchi wanataka barabara,shule na hospital,sasa niambie kwa Katiba hii ambayo inampa Rais mamlaka ya umungumtu unawezaje kumuwajibisha Samia? Tukubali kwamba tunahitaji Katiba Mpya ambayo itawapa wananchi kupitia wawakilishi wao yaani Bunge mamlaka ya kuisimamia Serikali na kumuwajibisha Rais. Japo Katiba iliyopo inatamka uwezo huo wa Bunge lakini kiuhalisia muundo wa Bunge lenyewe la CCM tupu unalinyang'anya hilo Bunge uwezo huo kwani wabunge wa CCM wakikaa kama kamati wanalazimishwa kuwa upande wa Serikali muda wote wawapo Bungeni ambaye hawezi kutii agizo hilo arudishe kadi ya CCM kwa maana ya kuacha ubunge.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…