Ally anaokota dodo chini ya mwarobaini

Ally anaokota dodo chini ya mwarobaini

Ngonepi

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2013
Posts
1,872
Reaction score
1,207
Kwa wafuatiliaji wenzangu wa hawa celebrity wetu local nadhani tutakubaliana kwamba kwa upande wa Bongo fleva Diamond na Ally wako on top kwenye social media kuliko wabongofleva wengine!

Tuna historia ya wote wawili hawa tangu mwanzo wao wa game hili mpaka walipo leo, tumejionea juhudi za kila mmoja katika kusaka mafanikio yao ya leo mpaka walipo!!

Wana juhudi kwa kweli hili halina ubishi.

Tukija kwenye hiki kinachoonekana kama beef, hapa ndipo ninapoona kwa biashara za miaka hii za kutengeneza matukio na hasa waliotengeneza hii "biif" bwana Ally ana kila sababu ya KUWASHUKURU kwa sababu hii kitu imemsaidia sana tena sana!!

Si "biif" ya kupelekea vita lakini kwa kweli imesaidia sana kumfanya Ally aendelee kuwapo hewani hata kama yeye mwenyewe hafanyi (au hana uwezo) juhudi kubwa kupigania mafanikio zaidi.

Kwa upana zaidi wanaosaidiwa na juhudi za Diamond ni wengi mno kibiashara ambao kwa nnje wanaonekana kama wanampinga lakini huku wakipiga hela kutoka kwa mashabiki wasiopenda mafanikio ya Mtandale Diamond!!
Hapa kuna bwana Shigongo Eric anayefaidika sana pia, huku Wema pia akiongezea kutunisha mfuko wa bw Eric ambaye kwa sasa aameongeza bidhaa nyingine magazetini inaitwa Zari.

Niwape pole tu wasanii wengine wa Bongo flava muonyeshao juhudi kubwa sana kazini kwenu lakini hazionekani na kila siku ameendelea Ally kulinganishwa na Mondi hata kama mnamzidi kwa mbaali sana.

Pole Jux, pole Ben paul pole pia Barnaba na wengineo.

#Ngonepi.
 
Mkuu kwani mambo ya team bado yapo??? Acha kuturudisha enz za jk
Dah enzi za j.k raha sana kushinda jukwaa la king kiba team kiba wakasusa et mods wanafuta comment zao [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Samahani ndugu...
Hivi Ali Kiba na Ben Pol nani anamzidi mwenzake kimziki..!?
Mkuu Ali kiba na Ben pol style yao ya muziki ni tofauti kwahiyo kila mmoja yuko vizuri kwa style yake Ila melody ya kiba iko so unique asee sijaona bongo hii, namkubali Ben tho
 
Habari za hivi nimechoka kuzisikia na kuzisoma pia.
#Zimechosha
 
ni kweli
umeongea kweli [emoji122][emoji122]
kiba beef linambeba
hana mziki wa kuwazini kina ben pol na wasanii wengine wenye juhudi
 
ni kweli
umeongea kweli [emoji122][emoji122]
kiba beef linambeba
hana mziki wa kuwazini kina ben pol na wasanii wengine wenye juhudi
Wanamwacha kwa mbali mno!!
 
Kiba moto wake hamna wa kuuzima bongo hii.. CC Mondi
Mwambie huyo
Mnamatatizo ya AKILI...
Ni vema mkaendelea kumfananisha huyo Ali Kiba na Bwana Dangote ingawa kimafanikio ni DHAMBI kubwa sana kuwafananisha hao watu...
Sio Diamond wala huyo Ali Kiba...
Wote wawili wameachwa mbali sana Kimuziki na Ben Pol..!
Ali Kiba yuko overrated lakini ni MZEMBE...
Diamond Platnumz ni MJANJA..!
 
inasikitisha sana kumlinganisha msanii mkongwe na msanii mchanga .
Kinachombeba domo ni management yake Tu
Siyo kipaji wala nini
Ally anasail kwenye muziki kwa miaka mingi zaidi ya domo bila hata management na anapiga mpunga domo babu tale akiacha kumpa support kwenye management lazima.umkute tandale anauza mihogo
Kwani Tale hajawahi kumsimamia msanii mwengine tofauti na Diamond..!?
Pia Ali Kiba hana management..!?
Pia suala la kusail kwenye game miaka mingi ndio kigezo cha kusema Ali ni mkali kuliko Diamond..!!?
Ali amesail muda mrefu kwenye game...
Sawa ni kweli..!
Lakini amefanya nini mpaka sasa..!?
Who is the icon of Tanzania in Music industry..!?
Acha chuki za KIJINGA mkuu..!
Ila sikubishii kwamba Ali Kiba ni mkali kimuziki kushinda Diamond..!
Pia ni haki yako kuamini hivyo..!
Mwisho; Diamond akirudi tandale kuuza mihogo wewe utakua Sinza Ambiance unafanya ile biashara Mbadala..!
 
Back
Top Bottom