Glenn
JF-Expert Member
- May 23, 2015
- 69,329
- 164,730
Ukubali ukatae Manara pekee, narudia manara pekee ndiye mhamasishaji bora wa wakati wote.Wewe ndio afisa habari wa Yanga, wewe ndio unatakiwa upite kwenye media zote ushawishi wanaYanga waende disband kuishangilia Yanga mwanzo mwisho, kazi hiyo unaiweza vizuri sana.
Wewe umeaminiwa na taasisi kubwa ya michezo nchini, Yanga, wananchi wanakukubali sana wewe.
Wakati wanaYanga wanajiuliza nani semaji baina yako na Manara wananchi walikuwa pamoja na wewe mwanzo mwisho.
Gusa achia twende kwao ni wewe ndio umeifanya kazi hiyo hadi bendi za muziki nazo zinaimba.
Sasa hivi wewe una followers wengi kutokana na wananchi kukuelewa sana ndugu yangu.
Lakini hili la kumruhusu Manara akusemee kwenye media zote ahamasishe watu kwenda uwanjani huku kesho akienda Wasafi kuhamasisha, u napoteza mvuto kaka.
Kipi kimekufanya ushindwe kwenda kwenye media kuhamasisha na umemuachia zungu pori?
Wengi watashindwa kwenda uwanjani kwa sababu huyo zungu pori akihamasisha na watu wakijaa uwanjani badala ya kupongeza mashabiki na wenzake kwa kazi kubwa walioifanya, anaanza kujisifia yeye kuwa ndio amejaza watu uwanjani.
Jiandae kaka huo ni mwanzo, anytime huyo mwarabu wa nguruka atachukua nafasi hiyo.
Manara ameongeza sana hamasa ya mpira nchini.
Uache unafiki kijana