Ally kiba apata ajali

Ally kiba apata ajali

Barabara ya morogoro dar sio nzuri inaajari nyingi sana sijui kwanini?.Pole sana Al Kiba
 
Pole sana la mahabuba wangu,mungu yupo nasi utapona urudi home twende kwa bibi kigoma
 
ALI KIBA NA MADANSA WAKE WANUSURIKA KATIKA AJALI YA GARI!

Ali-Kiba.jpg


Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Ali Kiba pamoja na madansa wake alfajiri ya jana(Jumapili) wamenusurika vifo kufuatia kupata ajali ya gari katika eneo la Mikumi mkoani Morogoro walipokuwa safarini kutokea Mbeya kuelekea jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika gazeti la Nipashe ambazo BC imeweza kuzithibitisha kutoka kwa Ali Kiba mwenyewe,jumla ya watu saba wamejeruhiwa katika ajali hiyo huku watatu kati yao wamelazwa katika hospitali ya mkoa Morogoro.Ali Kiba ambaye aliumia mguuni na mkononi tayari ameruhusiwa kutoka hospitali na amesharejea nyumbani kwake Dar ambapo ameieleza BC kwamba anaendelea vyema. Ali Kiba alikuwa awe miongoni mwa wasanii waliotumbuiza katika tamasha la Serengeti Fiesta lililofanyikia CCM Kirumba Mwanza hapo jana.
Chanzo kamili cha ajali hiyo hakijawekwa wazi na polisi tayari wanachunguza.BC inawatakia wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo kupona haraka ili waweze kurejea katika kazi zao.


 
ALI KIBA NA MADANSA WAKE WANUSURIKA KATIKA AJALI YA GARI!

Ali-Kiba.jpg


Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Ali Kiba pamoja na madansa wake alfajiri ya jana(Jumapili) wamenusurika vifo kufuatia kupata ajali ya gari katika eneo la Mikumi mkoani Morogoro walipokuwa safarini kutokea Mbeya kuelekea jijini Dar-es-salaam.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika gazeti la Nipashe ambazo BC imeweza kuzithibitisha kutoka kwa Ali Kiba mwenyewe,jumla ya watu saba wamejeruhiwa katika ajali hiyo huku watatu kati yao wamelazwa katika hospitali ya mkoa Morogoro.Ali Kiba ambaye aliumia mguuni na mkononi tayari ameruhusiwa kutoka hospitali na amesharejea nyumbani kwake Dar ambapo ameieleza BC kwamba anaendelea vyema. Ali Kiba alikuwa awe miongoni mwa wasanii waliotumbuiza katika tamasha la Serengeti Fiesta lililofanyikia CCM Kirumba Mwanza hapo jana.
Chanzo kamili cha ajali hiyo hakijawekwa wazi na polisi tayari wanachunguza.BC inawatakia wote waliojeruhiwa katika ajali hiyo kupona haraka ili waweze kurejea katika kazi zao.


Jamani kinachowarudisha nyuma watanzania wengi hasa wenye vipaji ni baadhi ya watu wasiopenda maendeleo ya wenzao.
vipaji hulelewa na siyo huangamizwa.
tujiulize ni kwanini wasanii wengi watanzania huvuma na baadaye hupotea ama kwa kuacha gemu ama kupata ajali nakupoteza maisha, wana JF jaribuni kurudisha fikra zenu nyuma kidogo muangalie baadhi ya wasanii waliopoteza maisha au kuondoka kwenye gemu ni wale ambao walikuwa wakivuma sana na walikuwa ni wakiwango cha kimataifa.
nadhani aliyenielewa achangie kivyake ila mimi nimejaribu kuedit hii thread mara 12 na nikabakiwa na mistari hii tu.
ALI KIBA tupo pamoja dogo.
Ila kumbuka siyo wengi walifurahi ulipokuwa unakula bata na R KELLY.http://www.youtube.com/watch?v=STKvzYWm9GU
Nawakilisha.
 
ile barabara nyembamba sana.wakati wa kupishana gali zinatenganishwa na mstari.so kama hamna gari mbele gali inakuwa katikati.hizi barabara zipanuliwe na wawe wanafyeka nyasi ambazo zimelala barabarani.poleni wote mnaopatwa na matatizo barabarani.ni hayo tu.mia.
 
dah.....alitaka ku-run dunia!!!! pole dogo
 
Back
Top Bottom