Ally Sykes alipompatia kadi namba moja mwalimu Nyerere baada ya kutoka vitani 1943

Ally Sykes alipompatia kadi namba moja mwalimu Nyerere baada ya kutoka vitani 1943

britanicca

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2015
Posts
16,295
Reaction score
33,994
Picha hii ilipigwa mwaka 1943, wakiwa vitani, India (Vita ya pili ya dunia), hawa ni Moja ya watu muhimu sana katika uanzishwaji wa chama cha TANU. Kushoto ni Ally Sykes (17) ambaye ndiye alikuwa na Kadi No. 2 ya TANU na kulia ni kaka yake Abdulwahid Sykes (19), aliyekuwa na Kadi No. 3. Ikumbukwekwe kadi No. 1 ya TANU ni ya Julius Nyerere.

Kwa sababu ya uwezo wa kifedha ni Ally Sykes ndiye aliyenunua kadi 16 za mwanzo kabisa, kisha akazigawa, alimpatia Mwl. Julius Nyerere kadi No. 1, yeye akajipa No. 2 na kaka yake akampa kadi No. 3.

Alifanya hivo baada ya kujua kwamba Nyerere ana kipawa sana na ni mtu muhimu ambaye anaonekana kuwa mzalendo na aliyajua hayo baada ya Nyerere kumshirikisha kwamba ni bora kuwa na chama kilichoimara zaid kuliko kutegemea chama cha wafanyakazi

Britannica


Mkuu Britanicca, asante kwa picha, ila dataz na dates hazijakaa vizuri kwa sababu

  1. TANU ilianzishwa mwaka 7/7/1964 na ndio ile sherehe ya 77, sasa hizi habari za hawa Ndugu wawili watoto wa mpiganaji vita wa Kizulu, alioletwa nchini baada ya kuisha kwa WW 1, yanatokea wapi?!.
  2. Mwalimu Nyerere ndiye sio tuu ndiye alikuwa Mwenyekiti wa TANU, bali ndiye mwanzilishi wa TANU, sasa kitu uanzishe mwenyewe, halafu unatuletea story za kupewa kadi na Fulani simply because huyo fulani ndio amechapisha hizo kadi, haijakaa vizuri!.
  3. Ni kweli kina Sykes walikuwa na uwezo kifedha, but they were not the only ones, the richest kwenye Tanu aliuwa ni Mzee John Rupia.
  4. Naomba nikupe Angalizo, na wewe usijekuwa ni mmoja wa waliolishwa matango pori kuhusu uasisi wa TANU, maana iliwahi kusemwa humu kuwa hata huo uenyekiti wa TANU, Mwalimu alipewa na wale Wazee wa Kariakoo!.
  5. Iko historia nzuri sana ya TANU iliyoandikwa na Mmmalawi, William Kanyama Chiume (Kwacha) ambayo iliishia kwenye manuscripts, sijui ziliishia wapi, hazikuchapishwa mpaka leo, kilichobakia humu jf, ni watu kututupia picha hizi na zile na kulishana matango pori!.
TANU ni Mwalimu Nyerere, na Mwalimu Nyerere ni TANU!.
P


FB_IMG_1534319521120.jpg
 
Unataka kuwapa waislamu cha kusema, hapa waongo hakuna.cha Sykes wala.nini kadi hizo so kitu, muhim hali ya kupigania nchi kutoka moyoni
 
Hawa watu ni muhimu sana kuanzia.Nyerere, Sykes mpaka bibi titi ndo walikuwa wakombozi wa kweli, hakuna mkombozi mwingine hakika,
Hawa akina Lissu ni wanaharakati tu mbaya zaid wako radhi wawe upande mmoja na mgeni kukwamisha taifa,
Unaanziasha thread na id moja na hapo hapo unaingia na id nyingine kuchangia!
 
Hawa watu ni muhimu sana kuanzia.Nyerere, Sykes mpaka bibi titi ndo walikuwa wakombozi wa kweli, hakuna mkombozi mwingine hakika,
Hawa akina Lissu ni wanaharakati tu mbaya zaid wako radhi wawe upande mmoja na mgeni kukwamisha taifa,
Lissu usimsumbue tujadili haya bila kuhusisha chuki
 
Picha hii ilipigwa mwaka 1943, wakiwa vitani, India (Vita ya pili ya dunia), hawa ni Moja ya watu muhimu sana katika uanzishwaji wa chama cha TANU. Kushoto ni Ally Sykes (17) ambaye ndiye alikuwa na Kadi No. 2 ya TANU na kulia ni kaka yake Abdulwahid Sykes (19), aliyekuwa na Kadi No. 3. Ikumbukwekwe kadi No. 1 ya TANU ni ya Julius Nyerere.

Kwa sababu ya uwezo wa kifedha ni Ally Sykes ndiye aliyenunua kadi 16 za mwanzo kabisa, kisha akazigawa, alimpatia Mwl. Julius Nyerere kadi No. 1, yeye akajipa No. 2 na kaka yake akampa kadi No. 3.

Alifanya hivo baada ya kujua kwamba Nyerere ana kipawa sana na ni mtu muhimu ambaye anaonekana kuwa mzalendo na aliyajua hayo baada ya Nyerere kumshirikisha kwamba ni bora kuwa na chama kilichoimara zaid kuliko kutegemea chama cha wafanyakazi
Britannica
View attachment 836469
Mkuu Britanicca, asante kwa picha, ila dataz na dates hazijakaa vizuri kwa sababu

  1. TANU ilianzishwa mwaka 7/7/1954 na ndio ile sherehe ya 77, sasa hizi habari za hawa Ndugu wawili watoto wa mpiganaji vita wa Kizulu, alioletwa nchini baada ya kuisha kwa WW 1, yanatokea wapi?!.
  2. Mwalimu Nyerere ndiye sio tuu ndiye alikuwa Mwenyekiti wa TANU, bali ndiye mwanzilishi wa TANU, sasa kitu uanzishe mwenyewe, halafu unatuletea story za kupewa kadi na Fulani simply because huyo fulani ndio amechapisha hizo kadi, haijakaa vizuri!.
  3. Ni kweli kina Sykes walikuwa na uwezo kifedha, but they were not the only ones, the richest kwenye Tanu aliuwa ni Mzee John Rupia.
  4. Naomba nikupe Angalizo, na wewe usijekuwa ni mmoja wa waliolishwa matango pori kuhusu uasisi wa TANU, maana iliwahi kusemwa humu kuwa hata huo uenyekiti wa TANU, Mwalimu alipewa na wale Wazee wa Kariakoo!.
  5. Iko historia nzuri sana ya TANU iliyoandikwa na Mmmalawi, William Kanyama Chiume (Kwacha) ambayo iliishia kwenye manuscripts, sijui ziliishia wapi, hazikuchapishwa mpaka leo, kilichobakia humu jf, ni watu kututupia picha hizi na zile na kulishana matango pori!.
TANU ni Mwalimu Nyerere, na Mwalimu Nyerere ni TANU!.
P
 
Mkuu Britanicca, asante kwa picha, ila dataz na dates hazijakaa vizuri kwa sababu

  1. TANU ilianzishwa mwaka 7/7/1964 na ndio ile sherehe ya 77, sasa hizi habari za hawa Ndugu wawili watoto wa mpiganaji vita wa Kizulu, alioletwa nchini baada ya kuisha kwa WW 1, yanatokea wapi?!.
  2. Mwalimu Nyerere ndiye sio tuu ndiye alikuwa Mwenyekiti wa TANU, bali ndiye mwanzilishi wa TANU, sasa kitu uanzishe mwenyewe, halafu unatuletea story za kupewa kadi na Fulani simply because huyo fulani ndio amechapisha hizo kadi, haijakaa vizuri!.
  3. Ni kweli kina Sykes walikuwa na uwezo kifedha, but they were not the only ones, the richest kwenye Tanu aliuwa ni Mzee John Rupia.
  4. Naomba nikupe Angalizo, na wewe usijekuwa ni mmoja wa waliolishwa matango pori kuhusu uasisi wa TANU, maana iliwahi kusemwa humu kuwa hata huo uenyekiti wa TANU, Mwalimu alipewa na wale Wazee wa Kariakoo!.
  5. Iko historia nzuri sana ya TANU iliyoandikwa na Mmmalawi, William Kanyama Chiume (Kwacha) ambayo iliishia kwenye manuscripts, sijui ziliishia wapi, hazikuchapishwa mpaka leo, kilichobakia humu jf, ni watu kututupia picha hizi na zile na kulishana matango pori!.
TANU ni Mwalimu Nyerere, na Mwalimu Nyerere ni TANU!.
P
Mkuu.kweli.ntaangalia.kweli.nilipotoa data hizo, lakin maelezo ya mwaka yalikuwa yame base sana kwa picha ilipigwa 1943, even if TANU ilianza 1954
 
Mkuu Britanicca, asante kwa picha, ila dataz na dates hazijakaa vizuri kwa sababu

  1. TANU ilianzishwa mwaka 7/7/1964 na ndio ile sherehe ya 77, sasa hizi habari za hawa Ndugu wawili watoto wa mpiganaji vita wa Kizulu, alioletwa nchini baada ya kuisha kwa WW 1, yanatokea wapi?!.
  2. Mwalimu Nyerere ndiye sio tuu ndiye alikuwa Mwenyekiti wa TANU, bali ndiye mwanzilishi wa TANU, sasa kitu uanzishe mwenyewe, halafu unatuletea story za kupewa kadi na Fulani simply because huyo fulani ndio amechapisha hizo kadi, haijakaa vizuri!.
  3. Ni kweli kina Sykes walikuwa na uwezo kifedha, but they were not the only ones, the richest kwenye Tanu aliuwa ni Mzee John Rupia.
  4. Naomba nikupe Angalizo, na wewe usijekuwa ni mmoja wa waliolishwa matango pori kuhusu uasisi wa TANU, maana iliwahi kusemwa humu kuwa hata huo uenyekiti wa TANU, Mwalimu alipewa na wale Wazee wa Kariakoo!.
  5. Iko historia nzuri sana ya TANU iliyoandikwa na Mmmalawi, William Kanyama Chiume (Kwacha) ambayo iliishia kwenye manuscripts, sijui ziliishia wapi, hazikuchapishwa mpaka leo, kilichobakia humu jf, ni watu kututupia picha hizi na zile na kulishana matango pori!.
TANU ni Mwalimu Nyerere, na Mwalimu Nyerere ni TANU!.
P
Nadhani mkuu maelezo yanaeleza kwamba pamoja na picha kupigwa mwaka 1943, lakin TANu baadae ndo ilianza, ila mwaka wa picha kupigwa ni mwaka 1943, japo TANu ni 1954
 
Hivi kweli mwalim Nyerere alikuwa hana hata pesa ya kununua/kulipia kadi ya uanachama wa TANU?...

Bahati nzuri sana mama Maria yupo, anayafahamu vizuri sana taarifa nyingi za mpenzi, mumewe na baba watoto wake...

Itabidi tuanze kumuuliza..

Nachelea baadae roho wa upotoshaji atapotosha sana Historia ya Mwalim Nyerere!
 
Picha hii ilipigwa mwaka 1943, wakiwa vitani, India (Vita ya pili ya dunia), hawa ni Moja ya watu muhimu sana katika uanzishwaji wa chama cha TANU. Kushoto ni Ally Sykes (17) ambaye ndiye alikuwa na Kadi No. 2 ya TANU na kulia ni kaka yake Abdulwahid Sykes (19), aliyekuwa na Kadi No. 3. Ikumbukwekwe kadi No. 1 ya TANU ni ya Julius Nyerere.

Kwa sababu ya uwezo wa kifedha ni Ally Sykes ndiye aliyenunua kadi 16 za mwanzo kabisa, kisha akazigawa, alimpatia Mwl. Julius Nyerere kadi No. 1, yeye akajipa No. 2 na kaka yake akampa kadi No. 3.

Alifanya hivo baada ya kujua kwamba Nyerere ana kipawa sana na ni mtu muhimu ambaye anaonekana kuwa mzalendo na aliyajua hayo baada ya Nyerere kumshirikisha kwamba ni bora kuwa na chama kilichoimara zaid kuliko kutegemea chama cha wafanyakazi

Britannica





View attachment 836469
Britannica,
Post nzima haikukaa vyema kuanzia kichwa cha habari.
Historia ya TANU huwezi kuiandika kwa mistari miwili.

Historia ya TANU inaanza na African Association mengi
yalipita hadi kufikia kuasisiwa TANU mwaka wa 1954.

Hiyo picha hapo juu inatka katika Nyaraka za Sykes na
mimi ndiye niliyeitia mtandaoni ili watu waione na wasome
historia ya TANU.

Naweka hapo chini niliyoandika katika kitabu cha Abdul
Sykes kuhusu kadi za TANU:

''Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake. Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika. Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion. Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie. Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000. Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa. Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama. Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo. Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7. Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Tosiri kadi nambari 25.''

''Mtemvu alimuelezea Ally kwa ufupi juu ya mkutano wao na Nyerere Morogoro mjini na aliomba apewe mara moja kadi 200 za TANU. Ally aliwaandikia na kuwapa kadi za uanachama wa TANU, Mtemvu na Tambwe na akamwambia mdogo wake Abbas, awaalike wote wawili kwenye mkutano wa uzinduzi wa tawi la TANU la Dar es Salaam ambao ulikuwa ufanyike Jumamosi iliyofuata. Uongozi wa TANU ulipokuwa ukijitayarisha kwa mkutano wa uzinduzi, Ally Sykes alikuwa tayari amekabidhiwa barua ya uhamisho kutoka Dar es Salaam kwenda Korogwe. Kwa hakika hasa, Ally alipewa barua hiyo wiki mbili tu baada ya kuundwa kwa TANU. Hii ilikuwa mara ya pili Ally kupewa uhamisho kama adhabu yake ya kupambana na utawala wa kikoloni.''

''Familia yangu ilifahamiana na Dome Budohi, mmoja wa wanaharakati kutoka Kenya. Wakati ule wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa akiishi Dar es Salaam. Budohi alikuwa mmoja wa wazalendo walioasisi TANU na kadi yake ya uanachama ni nambari 6 aliyopewa Julai 1954.''

''Mwezi June, makao makuu ya TAA yalitangaza kamati yake ya utendaji: J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, Katibu wa pamoja wa muhtasari; Wajumbe wa kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.''

Hii ndiyo historia ya TAA 1953 kuelekea TANU 1954.
Nadhani suala la kadi sasa limeeleweka pamoja na
historia ya TANU.
 
Mkuu Britanicca, asante kwa picha, ila dataz na dates hazijakaa vizuri kwa sababu

  1. TANU ilianzishwa mwaka 7/7/1954 na ndio ile sherehe ya 77, sasa hizi habari za hawa Ndugu wawili watoto wa mpiganaji vita wa Kizulu, alioletwa nchini baada ya kuisha kwa WW 1, yanatokea wapi?!.
  2. Mwalimu Nyerere ndiye sio tuu ndiye alikuwa Mwenyekiti wa TANU, bali ndiye mwanzilishi wa TANU, sasa kitu uanzishe mwenyewe, halafu unatuletea story za kupewa kadi na Fulani simply because huyo fulani ndio amechapisha hizo kadi, haijakaa vizuri!.
  3. Ni kweli kina Sykes walikuwa na uwezo kifedha, but they were not the only ones, the richest kwenye Tanu aliuwa ni Mzee John Rupia.
  4. Naomba nikupe Angalizo, na wewe usijekuwa ni mmoja wa waliolishwa matango pori kuhusu uasisi wa TANU, maana iliwahi kusemwa humu kuwa hata huo uenyekiti wa TANU, Mwalimu alipewa na wale Wazee wa Kariakoo!.
  5. Iko historia nzuri sana ya TANU iliyoandikwa na Mmmalawi, William Kanyama Chiume (Kwacha) ambayo iliishia kwenye manuscripts, sijui ziliishia wapi, hazikuchapishwa mpaka leo, kilichobakia humu jf, ni watu kututupia picha hizi na zile na kulishana matango pori!.
TANU ni Mwalimu Nyerere, na Mwalimu Nyerere ni TANU!.
P
Sykes Mbuwane aliletwa na Mjeruman ,akapoteza uhai wakati wanatoa kupigana na Mkwawa.Kleist Sykes mwanaye alilelewa na Mwalimu Plantan na huyo ndo baba wa a Abdulwahd,Ally na Abas Sykes.Hawa watu ni muhimu katika historia ya nchi yetu.
 
sijaona historia ya hovyo kama ya tanganyika
yaani historia nzima tangu primary hadi university mpambanaji pekee ni nyerere tu
ajabu sana yaan huyu mtu alikua yeye ndo rais,makamu yeye, katibu yeye 😁😁
WATANZANIA TUITAFUTE HISTORIA YETU
 
Back
Top Bottom