Ally's Bus mchukulieni hatua huyu mbeba mizigo yenu pale Shekilango

Ally's Bus mchukulieni hatua huyu mbeba mizigo yenu pale Shekilango

Ambakucha

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2019
Posts
317
Reaction score
520
Wadau za Jumapili? Jana nikiwa na ndugu yangu tulipeleka mzigo pale Shekilango kwenye ofisi za Bus la Ally's. Kulitokea sitofahamu kati ya mbeba mizigo mmoja na abiria ambaye na yeye alipeleka mzigo.
Kilichonisikitisha, ni mzozo wao kusimamiwa na matusi kutoka kwa mbeba mizigo huyo kwenda kwa mteja huyo.

Mbeba mizigo alifikia hatua ya kumwambia mteja aulize yeye ni nani pale? Na anaweza kumfanyia kitu kibaya mteja huyo.

Mbeba mizigo huyo ni mrefu, mwembamba ana mwonekano wa 'hana cha kupoteza.'

Kisa; mteja alifika na Bajaj akitaka kushusha mzigo wake. Staff wa Ally's akamwonesha mahali pa kusimamisha Bajaj ili ashushe mzigo wake. Wakati huohuo mbeba mizigo alikuwa analiita basi litoke. Kwa hiyo Bajaj ikafunga njia. Ndipo mbeba mizigo akamuwakia mteja bila kujua mteja alielekezwa na staff.
 
Wafanyakazi wa ofisi za mizigo makampuni ya mabasi ni vilaza hawajui kama hiyo mizigo ndipo kula yao ilipo hata pale Abood kuna aliyepo ofisi za mizigo opposite na ubungo plaza pale engen oil station kwa ndani kule ni mkaka maji ya kunde jina sijawahi kumkariri ana kiburi na nyodo balaa anafoka ovyo tu
 
Wafanyakazi wa ofisi za mizigo makampuni ya mabasi ni vilaza hawajui kama hiyo mizigo ndipo kula yao ilipo hata pale Abood kuna aliyepo ofisi za mizigo opposite na ubungo plaza pale engen oil station kwa ndani kule ni mkaka maji ya kunde jina sijawahi kumkariri ana kiburi na nyodo balaa anafoka ovyo tu
Pale wapo wawili. Kuna mdada white na kaka mmoja kama mpema flani hivi.

Oya, wanajiona wamepatia sana. Yaani sema kwakua kila siku 2 lazima nikatume mzigo pale uwa nafunika kombe.
 
Wafanyakazi wa ofisi za mizigo makampuni ya mabasi ni vilaza hawajui kama hiyo mizigo ndipo kula yao ilipo hata pale Abood kuna aliyepo ofisi za mizigo opposite na ubungo plaza pale engen oil station kwa ndani kule ni mkaka maji ya kunde jina sijawahi kumkariri ana kiburi na nyodo balaa anafoka ovyo tu
Kumbe unaendaga pale Abood! Mbona sikuonagi?
 
Unafanya uwekezaji mkubwa na wa gharama kisha unaweka stuff wasio na customer service nzuri na darasa la sefuli
Kwenye mabasi 90% wafanyakazi wote ni vilaza anzia hadi madreva na makonda, mkata tiketi, huduma nzuri tulipata Kwa scandinavia, Zainabus, sumry ndio walikua na lugha adhimu kidogo, hayo mavilaza mengine kwenye hizo kampuni unaweza kulia, kama umehudumiwa na watu wa mabasi pale kenya na Rwanda au Uganda, Tanzania unaona hawa jamaa takataka, wanajihisi na wao ni matajiri wakati matajiri wao ni wanyenyekevu Kwa wateja
 
Kwenye mabasi 90% wafanyakazi wote ni vilaza anzia hadi madreva na makonda, mkata tiketi, huduma nzuri tulipata Kwa scandinavia, Zainabus, sumry ndio walikua na lugha adhimu kidogo, hayo mavilaza mengine kwenye hizo kampuni unaweza kulia, kama umehudumiwa na watu wa mabasi pale kenya na Rwanda au Uganda, Tanzania unaona hawa jamaa takataka, wanajihisi na wao ni matajiri wakati matajiri wao ni wanyenyekevu Kwa wateja
Sasa hivi Shabiby,Kimbinyiko,Ngasere wanajua customer care vizuri
 
Eeh lakini kwa namna unavyoandika humu, nikikuona nitakugundua.

Halafu itakuwa ni wewe ulikodi bajaji yangu toka Mawasiliano hadi pale Abood-Shekilango then ukaaambiwa uende Ofisi za pale Engen nikakupeleka. Ukanipa buku 5.
Ulitaka kunitoa roho hapo kwenye kukodi bajaji, ila sasa ulipofika kwenye kukupa buku 5😂😂nimeshusha pumzi, huyo sio mimi, siwezi kutoa hiyo hela kwa umbali mfupi namna hiyo😅😅😅 labda niwe mgonjwa tena mahututi kiasi chake
 
Ulitaka kunitoa roho hapo kwenye kukodi bajaji, ila sasa ulipofika kwenye kukupa buku 5😂😂nimeshusha pumzi, huyo sio mimi, siwezi kutoa hiyo hela kwa umbali mfupi namna hiyo😅😅😅 labda niwe mgonjwa tena mahututi kiasi chake
Wewe🤣🤣. Toka Mawasiliano-Shekilango huwa tunatoza 3k(nimekupa code kunifahamu).

Ulipofika Shekilango, ukaaambiwa mzigo haupo pale, so kufika ukanipa 5k kiroho safi.
 
Wadau za Jumapili? Jana nikiwa na ndugu yangu tulipeleka mzigo pale Shekilango kwenye ofisi za Bus la Ally's. Kulitokea sitofahamu kati ya mbeba mizigo mmoja na abiria ambaye na yeye alipeleka mzigo.
Kilichonisikitisha, ni mzozo wao kusimamiwa na matusi kutoka kwa mbeba mizigo huyo kwenda kwa mteja huyo.

Mbeba mizigo alifikia hatua ya kumwambia mteja aulize yeye ni nani pale? Na anaweza kumfanyia kitu kibaya mteja huyo.

Mbeba mizigo huyo ni mrefu, mwembamba ana mwonekano wa 'hana cha kupoteza.'

Kisa; mteja alifika na Bajaj akitaka kushusha mzigo wake. Staff wa Ally's akamwonesha mahali pa kusimamisha Bajaj ili ashushe mzigo wake. Wakati huohuo mbeba mizigo alikuwa analiita basi litoke. Kwa hiyo Bajaj ikafunga njia. Ndipo mbeba mizigo akamuwakia mteja bila kujua mteja alielekezwa na staff.
Hakuna njia nyingine ya kusafirisha huo mzigo? Utamaduni wa wahumu wa vyombo vya usafiri hasa mabasi Bongo kuona wateja wao ni watu duni upo sana. Ulianza kipindi cha ukosefu wa mabasi ya kusafiria, hivyo waliokuwa na mabasi na wafanyakazi wao wakazoea kunyenyekewa.
 
Back
Top Bottom