Kinyonyoke
JF-Expert Member
- Oct 4, 2016
- 3,498
- 13,138
Majina ya vijana wanaotakiwa kujiunga na mafunzo ya JKT yametangazwa.
Kutangazwa kwa majina haya kumezirudisha nyuma kumbu kumbu zangu yapata miaka miwili sasa.
Tulikuwa Range(Mazoezi ya ulengaji shabaha).Taratibu zote zilizingatiwa kwa umakini wa hali ya juu sana lakin ilipofika zamu yetu (Combania C Coy) kutokana na muda kwenda sana na uchovu makamanda walipungukiwa na umakini kabisa.
Anyway to cut a long story short jamaa aliekuwa pembeni yangu..mikono yake ilikuwa imelegea sana kama mlenda.Sasa wakati anafyatua risasi, SMG yake iliyumba na kuja uelekeo wangu(haikunilenga moja kwa moja lakini kama tu angeligeuka hatua chache ingekuwa story tofauti!) ila risasi ilitua mita kadhaa tu mbele yangu huku ganda la risasi likinichabanga usoni na kuniachia maumivu kiasi.Nilikata moto!
Vijana waende JKT, hawatajutia.Pia mtu anaweza kula shavu MS kama ilivyotokea kwa mshikaji wangu.Who knows?
Kutangazwa kwa majina haya kumezirudisha nyuma kumbu kumbu zangu yapata miaka miwili sasa.
Tulikuwa Range(Mazoezi ya ulengaji shabaha).Taratibu zote zilizingatiwa kwa umakini wa hali ya juu sana lakin ilipofika zamu yetu (Combania C Coy) kutokana na muda kwenda sana na uchovu makamanda walipungukiwa na umakini kabisa.
Anyway to cut a long story short jamaa aliekuwa pembeni yangu..mikono yake ilikuwa imelegea sana kama mlenda.Sasa wakati anafyatua risasi, SMG yake iliyumba na kuja uelekeo wangu(haikunilenga moja kwa moja lakini kama tu angeligeuka hatua chache ingekuwa story tofauti!) ila risasi ilitua mita kadhaa tu mbele yangu huku ganda la risasi likinichabanga usoni na kuniachia maumivu kiasi.Nilikata moto!
Vijana waende JKT, hawatajutia.Pia mtu anaweza kula shavu MS kama ilivyotokea kwa mshikaji wangu.Who knows?