Alphabeti ya Kiswahili.

Lunanilo

JF-Expert Member
Joined
Feb 15, 2008
Posts
370
Reaction score
14
Salamu marafiki.

Nimekuwa nikisoma mabandiko kadhaa katika ukumbi. Nimeona kuwa kuna watu wana tabia ya kufupisha maneno kama kusikia basi nakadhalika kwa kueka herufi "c" badala ya herufi "s". Kitu kinachonishangaza utaona kuwa mtu anaadika bac akimaanisha kuwa ni kifupisho cha basi au "kuckia" badala ya "kusikia".
Kwa ulewa wangu mimi "c" siyo "si" kwa kiswahili

c ni Che .

Ni maoni yangu kuwa japokuwa tumeathiriwa na lugha ya kupelekeana habari kwa kutumia simu zetu za mikononi, ukatishaji wa maneno unaweza ukabadilisha maana ya neno na hata kupotosha lugha yetu.

Shukrani.
 
Unataka kumfundisha mtu anayetafuta lughamkato ya mitaani iliyotokana na text messaging systems alifubete ya Kiswahili wakati wafuatiliaji wengi wa kiswahili wa kawaida hawaijui?

Nia yao si kufuata istilahi na nahau iliyojaa ulimbwende yakinifu, nia ni kufupisha maneno kwa gharama yoyote ile itakayotokea kwa kiswahili.Kama unamaka kwa hili maka useme unamakia hili, lakini usitake kuwafundisha njia mjarab ya kuboronga Kiswahili.
 
mi nadhani lugha yoyote duniani ni lazima ipitie kwenye misukosuko na mara nyingi matokeo yake ni eidha lugha kufa kabisa au kupanuka zaidi, kiswahili ni mchanganyiko wa lugha nyingi (kichina, hindi, english, kireno, arab,jerumani, kibantu nk), na matatizo makubwa ya kiswahili ni kukosa alfabeti zake, yaani namaanisha herufi ambazo ni tofauti na hizi za kiingereza ambazo ni za kilatini, kwa kukosa huko herufi za kiswahili kumepelekea kiswahili kuwa na muingiliano mkubwa wa kimatamshi wa kiherufi na kiingereza.
 


Lugha zote zisokuwa, mwisho wake hujifia
kiswahili kinakuwa, mwenzetu kakumbushia
Paukwa pia pakawa, misemo ya asilia
Shukurani we Kituko, kutukumbusha kwa hilo
 
 
 
Wakuu nadhani watu wengi huwa wanatumia maneno kwa ufupisho wakati yakiwa hayana maana kamili kama wanavyotaka hasa kwenye text messages kwa simu za mkononi..unaweza kuwa umebaki na pesa ya kuandika msg moja na unaona inaishia bila kueleweka basi pale ndo vifupisho vinapoanzia..sasa tabu ni pale haki hiyo inapomuathiri mtu na kuendelea kutumia hata pale pasipostahili.
 
Asante Dingiswayo. Umeelewa ninachokisema. Ukiandika katika hati mkato za mawasiliano ya simu za mkononi na rafiki zako haidhuru sana . Lakini unapoandika mada nyingine au insha kwa maoni yangu haipendezi sana. mawasiliano ya watu katika hati mkato ni juu yao wenyewe, ninakwamishwa nikiona kuwa hiyo tabia inaendelea katika mawasiliano mengine, hasa unapowasiliana na watu wasiokufahamu.

siku njema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…