Alphonce Lusako: Nimenusurika kutekwa kwa madai ya kuwa Gaidi, sasa namuachia Mungu suala la usalama wangu

Alphonce Lusako: Nimenusurika kutekwa kwa madai ya kuwa Gaidi, sasa namuachia Mungu suala la usalama wangu

mirindimo

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2009
Posts
901
Reaction score
1,742
IMG_1374.jpeg

NIPO SALAMA ndugu zangu Baada ya TUKIO la KUWATOROKA Waliojiita POLISI, Pale Landmark Hotel, Ubungo, Dar es salaam. "Kama Magaidi Wanakamatwa kwa namna ile, Nadhani kuna shida kubwa kwa Vyombo Vyetu Vya dola. NITAELEZA kwa kina but in brief

Nikiwa na Kikao Kazi Landmark Hotel,Ubungo,Walikuja Watu Waliojitambulisha ni Polisi kutoka Makao Makuu, Wakiuliza nani anakisimu kidogo hapa, Tukawashangaa na kuwauliza nini akina nani? WAKADAI Wapo kazini Wao ni Polisi na kutuonyesha Vitambulisho haraka

Wakatuambia hapa Kuna GAIDI Kati yenu tunanamtafuta hapa, MWENYE simu ndogo atoe haraka, Mara kiongozi wa Msafara akapokea simu ya maelekezo Kwamba wote tupo under target. Tukaambiwa tupo Chini ya Ulinzi tangia sasa.

Wenzangu walipoanza kupiga simu kwa ndugu wakapokonywa haraka na kukatokea mzozo Mkubwa baina yetu na Wao, Nikafanikiwa KUWATOROKA kwa njia ya Makuti iliyopo kwenye Mtalo wa Maji na kuibukia Ubungo Darajani na kwenda sehemu salama kwangu

Nimearifiwa na Wakili Wangu, Kwamba Wenzangu Wawili (2) waliowekwa Chini ya Ulinzi na Walipelekwa Kituo cha Polisi chang'ombe na baada ya Mahojiano, Wameachiwa huru kwa hoja Kwamba Polisi Walikosea Target ya MAGAIDI

Hili si tukio la kwanza dhidi yangu, SIWEZI Nikapuuza hata kidogo dhamira yao, Nilipofukuzwa chuo, Nilivamiwa na Watu wa AINA HII na Wakajitambulisha kwa Staili hii hii, Bila WATU DDC, Dar es salaam, huenda ingekuwa HISTORIA

Nimeokoka kwenye tukio hili, sijui la kesho, Nasisitiza kwamba, MAGAIDI Hawawezi kukamatwa kwa namna ile, Najua tunachukua tafadhari kama Binadamu, Namwachia MUNGU Usalama Wangu tangu sassa.
 
Hold on.....
Wewe ni nani??
Picha ilio ambatanishwa kwenye huu uzi ni yanani??
Baada ya kujibiwa maswali hayo mawili, then mtuache wenyewe tutaunganisha dot.
 
Umekurupuka kutueleza tukio lako bila ya kufafanua wewe ni nani na kwa vipi hasa umehitilafiana na wanaokutafuta.
Unapokimbilia huku JF! Ni vema pia ukatoa short brief kuhudiana na nature ya tukio lako.Hii itasaidia kwa wale wanaotaka kukusaidia kwa namba moja ama nyingine basi wapate pa kuanzia.
 
Back
Top Bottom