Aluta continua dk. Slaa

Ntaramuka

Senior Member
Joined
May 2, 2008
Posts
169
Reaction score
27
Kwa heshima, upendo na imani, nampongeza DK. W. Slaa kwa juhudi zake mbalimbali na zinazoonekana katika kuwapigania watanzania, hakika huyu ndiye mzalendo number moja wa nchi hii iliyojaa mafisadi.

Slaa amepata changamoto nyingi sana katika lupiga vita ufisadi, lakini kikubwa ni jinsi alivyozomewa na MAFISADI WA CCM jana baada ya kikao cha bunge. MAFISADI HAWA WA CCM wanamshutumu kwa kupinga malipo makubwa saaana wanayoyapata wabunge ambayo ni tofauti na watumishi wengine wa nchi hii kama waalimu, askari, madaktari, wahadhiri nk.

Wanasema ati anatafuta ummarufu wa kisiasa!!! Slaa ni mwanasiasa na kazi yake ni kuwatetea wangonge masikini wa kitanzania, sasa hili likimpa umaarufu dhambi iko wapi?

Binafsi nasema ALUTA CONTINUA DK. SLAA, tuko pamoja.
 
Tuko pamoja mkuu. Uzuri mmoja mwenyewe hababaiki kwa kuzomewa kwani anajua analolifanya. Si unakumbuka ya Mwembe Yanga!
 
aluta continua dk slaa...

Hata ile ya mengi jana bado kwa slaa kiujasirii (bila unafiki) hafikiii...

Baba slaaa mbele kwa mbele
 
Wakati umefika na sisi tukiona magari ya wabunge tuwazomee. Maana wenyewe ndio wameonyesha kuwa ukipingana na mwenzio katika hoja unamzomea. Nadhani watu waanzie kesho pale mnadani maili mbili wanapokwenda kupata nyama choma.
 
Wakati umefika na sisi tukiona magari ya wabunge tuwazomee. Maana wenyewe ndio wameonyesha kuwa ukipingana na mwenzio katika hoja unamzomea. Nadhani watu waanzie kesho pale mnadani maili mbili wanapokwenda kupata nyama choma.

Tuanze kuwazomea Wabunge wa CCM popote pale tutakapowaona maana baadhi yao ni mafisadi na watetezi wa mafisadi. Dr Slaa usivunjike nguvu asilimia kubwa ya Watanzania tuko bega kwa bega nawe katika vita dhidi ya mafisadi.
 
wakati umefika na sisi tukiona magari ya wabunge tuwazomee. Maana wenyewe ndio wameonyesha kuwa ukipingana na mwenzio katika hoja unamzomea. Nadhani watu waanzie kesho pale mnadani maili mbili wanapokwenda kupata nyama choma.

nadhani kuzomea haitoshi labda wapigwe mawe kama kibaka maana hawanatofauti nao
 
Dr. Slaa ninakukumbusha kauli moja ya iliyosemwa na mwandishi wa kitabu cha shairi maarufu kama AN ENEMY OF THE PEOPLE ( Henrick Ibsen ) alisema na nanukuu. "The stronget man is the who stands alone".

Mheshimiwa Dr. Slaa, mtetezi wetu wanyonge sisi tunakuhakikishia kuwa kama mtu uliyeamua kupambana moja kwa moja na ufisadi huna jinsi ya kukwepa kusimama peke yako. Tuko pamoja nawe katika hili.
Wakuguse waone!!

Usiogope wala usirudi nyuma. ' Mungu wa haki yuko pamoja nawe!!!

DAIMA MBELE
NA HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE
 
Wakuu, hilo ni kweli na naungana nanyi asilimia mia moja, Inabidi wananchi tuwazomee hao wabunge kwa kumzomea shujaa wetu kisa katoboa siri wanavo tunyonya!

Nadhani kila wakipita tukiwazomea kama ile ya 'Zitto na buzwagi' akili zitawarudia, Ila nashauli tutafute ka kibwagizo kazuri ka kuwazomea nako ili wajue tumechukizwa sana na wanayo tutendea, yaani badala ya kututetea wanyonge wanabaki kutetea matumbo yao! Watunzi leteni kibwagizo safi cha kufikisha ujumbe murua wa kuwazomea nao!

BARAVO DR SLAA, TUPO NAWE BABA HATA KWA MAOMBEZI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…