Ama kweli magwiji wa siasa wameshika hatamu, hakuna mjadala unaodumu

Ama kweli magwiji wa siasa wameshika hatamu, hakuna mjadala unaodumu

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Ile kauli ya 'anaupiga mwingi' inaweza kuwa na ukweli kuliko tunavyodhani. Yaani ni mchakamchaka wa kufa mtu.

Ikitokea tu kuna mjadala wa moto unaendelea basi ndani ya siku mbili tatu unakua umezimwa kwa matukio mengine ya moto zaidi

Mara hawa wanadai Katiba Mpya huku Sabaya anakamatwa, kule bei ya mafuta inapanda, huku Diallo anamsimanga mwendazake, mara sijui tozo za miamala zimepanda, sijui wagonjwa wa corona wako kwenye oxygen, haujakaa sawa soko Kariakoo limeungua, sijui nani huko katuma picha zake za uchi. Ni matukio mfululizo, full throttle.

Vichwa vya wadanganyika viko fully occupied 24/7. Choir master anaonekana anaimudu kweli kazi yake. Miluzi kila kona yaani mbwa kachanganyikiwa kabisaaa.

CHADEMA msipokuwa makini mtakuwa mnadandia hoja mpya na kujadili matukio kila siku, maana ma producer wa matukio wanafanya kazi overtime.
 
Tanzania haijawahi kukaukiwa na breaking news....
Ni mwendo wa breaking news kila kukicha.

Lakini enzi za mwendazake alikua hadi analazimika kwenda kanisani kupiga politics 😀😀

Huyu mama hata matukio ya kuapisha watu na uzinduzi wa miradi ni machache sana lakini wanatuzungusha vichwa kama pia
 
Kutokana na Wabongo kupenda matukio, umbea na kufurahia matatizo ya wengine, ukiwa mwanasiasa mzuri kama JK nchi hii unaweza kufanya lo lote na likapita. Ajabu sana!

Ila nikiri tu. Mama anaupiga mwingi sana yaani!
Ni kweli, yaani tunashika hili halijaisha limekuja lile. Utaona tu hili la moto kariakoo na uzembe wa fire sijui manispaa litapotea kama utani.
 
Ni mwendo wa breaking news kila kukicha.

Lakini enzi za mwendazake alikua hadi analazimika kwenda kanisani kupiga politics 😀😀

Huyu mama hata matukio ya kuapisha watu na uzinduzi wa miradi ni machache sana lakini wanatuzungusha vichwa kama pia
Anaupiga mwingi. She is very smart na circle yake ina watu sahihi.
 
Back
Top Bottom