Ambao hatuna Magari tukutane hapa!

Duh! Ngoja niunde kwanza mzunguko mzuri wa fedha
Hilo ndio suala la msingi mkuu,
Ukiwa na good circulation ya hela gari yeyote unanunua. Hata nyumba unajenga kabisa. Na hii ndio formula matajiri wanatumia kuwa hapo walipo.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] pale ambapo jamaa hali ngumu lakin anajarbu kujipa.moyo
 
[emoji23][emoji23][emoji23] pale ambapo jamaa hali ngumu lakin anajarbu kujipa.moyo
hahahahha sasa unadhani tutafanyaje mkuu kama sio kufanya 'sizitaki mbichi hizi' kama hali ni tata kiasi hicho.
taboo zinaanzaga hivyo hivyo eti mjamzito asile nyama sijui inasababisha mtoto kuwaje kumbe hali haziruhusu tunajifariji tu.
 
nilibahatika kupata gari katika umri mdogo na gari zuri kwa wakati huo lakini sikufikiria kujenga zaidi ya kuzunguka viwanja nikishindana na majokofu ya bar na majiko yake!
wakati huo ratiba yangu ilikuwa vizuri
  1. jumatatu urojo ilala kwa kuwa mwishoni mwa wiki nimekulakula hovyo
  2. jumanne nitakaa millenium tower opposite sikumbuki kunaitwaje tena au naweza sogea rose garden nikichoka nampitia wife sinza saloon nikimbebesha kuku wa kuzunguka
  3. jumatano hugo house mchemsho wa kuku
  4. alhamisi DDC kondoa kulikuwa na mishkaki usipime
  5. ijumaa naanza na changombe village mchana lunch kabla ghorofa halijaanguka kisha tabata kwa mshikaji anakijiwe cha kiti moto
  6. jumamosi kazi kidogo kisha tunaamia biashara club
  7. jumapili vikao vya harusi msimbazi liverside wakati wa kurudi unapitia temeke chips kuku au opposite na liki hotel kuna kuku wa kuchoma.
baada ya gari kupata ajali washkaji wakakatika kwanza kama yalivyo maji nikarudia ubaridi wangu na ndipo nikakumbuka viwanja vyangu kimoja nikaanza kukijenga.
kwa hiyo wenye magari wanahitajika kuwa makini kwa mazingira wanayoishi hapo nimeruka tafrija za kujifisha na vidada!
 
Wenye magar mabovu tuna comment WAP ..?
 
asante kwa mchango wako mweshimiwa mbunge na mwakilishi wa wote wasio na magari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…