Ambao Hatusherekei Siku ya kuzaliwa(Birthday)

Wengi hawalifahamu hili
 
Mwanaume kusherehekea birthday ni uzwazwa
 
Mimi personal sijawai na sitowai,mke wangu kila mwaka anagombana nami kisa birthday yake...NI UPUUZI KIWANGO CHA LAMI
 
Labda wanawake ila mwanaume kusherehekea birthday ni uzwazwa na kama mwanaume unazima mishumaa na kumwagiwa maji lazima wanakubashite
sioni uzwazwa wowote hapo, naona ni njia ya kufurahia maisha tu, usiriaz unauweka pembeni once, fun kidogo mambo yanaendelea... labda akiwa obsessed sana na birthday hadi kuyapa kisogo majukumu muhimu hilo tatizo, ila birthday unazitumia kujenga bond na familia na marafiki,

Nashangaa kuwa mwanaume kuwa macho kuna faida gani? kunaongeza mafanikio zaidi? furaha zaidi? kupendwa? hakuna ushahidi mwanaume ukiwa kauzu ndio utafanikiwa kwenye hivyo vitu zaidi,
 
Mwanaume muafrika na ndevu zake anaimbiwa happy birthday, anapigiwa makofi, anazima mishumaa na kumwagiwa maji, lazima ni bashite.
 
Mimi hio siku nakua na majonzi nakutafakari kwamba ndio safari imeiva ya kuondoka dunian so sinaga raha automatically naanza kujihesabu vipi ntafikia mahala pema...
 
isitoshe unakuwa umezungukwa na wadau wa kike na kiume wanakuimbia huku unelifungua domo unasubiri kulishwa keki hepibesdei tuyuuu!
hepibesdei tuyuuu!
auoda yuu na!

hapana aisee..
Ha ha ha ha ha
 
Mimi nafikiri wengi wanao sheherekea siku zao za kizaliwa walizoeshwa huu utaratibu na wazazi wao. Hivyo basi ndio kinyume cha wale ambao hawasheherekei siku zao za kuzaliwa. Kwa hiyo sio jambo la kujuta wala kujiuliza ni kwa sababu gani unakosa hamasa ya kufanya sherehe ama tafrija fupi kwenye siku yako ya kuzaliwa.
NB; Wapo waliojifunza huu utaratibu ukubwani ila ni wachache. Kama una ufurahia huu utaratibu bado una nafasi ya kujizoesha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sijawahi kabisa kusherekea birthday na mara nyingi huwa nasahau mpaka siku inapita
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…