Ambao mna marafiki huwa mnawapataje?

Ambao mna marafiki huwa mnawapataje?

Evelyn Salt

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
70,916
Reaction score
141,437
Good morning jf....
Tusio na marafiki tukutane hapa😔

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, watu ambao wanaweza kushare ramani za maisha, watu ambao tunaweza kupanga safari kwenda vituo vya wahitaji tukawape misaada, watu ambao nikihitaji kumwagilia moyo najua wapo, watu ambao nikikwama najua watakuwepo, kina mama wenzangu huwa wana vyama umuhimu wa vyama naujua ila mi hata chama sijawahi kuwa nacho....naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
 
Wengi tunaowaona sio kwamba ni marafiki bali watu waliozoeana,na mazoea huja kupitia kusoma pamoja,kufanya kazi pamoja au kwenye mazingira yanayofanana na hayo!

Kupata rafiki ambae atakuthamini na kuwa mwaminifu kwako sio kazi rahisi yani hapo na maombi yahusike,bila hivyo it is better hapo ulivyo alone kuliko upate watu wataolazimisha downfall yako kilazima kabla ya muda!

Cha mwisho kama uko desperate sana jaribu kwenye vikoba huko utapata watu na ikitokea una shida basi hao wataambatana nawe,kama uko dar wafatilie buta vikoba hawa wana branches kila kona ya dar!
 
Mimi nazungumzia mitaji ya aina yote: Mahusiano mazuri na watu ni mtaji mkubwa mno.
Kupenda kushiriki na watu kwenye shida na raha ndiko kunaleta hata mtaji pesa.
Sema sasa ninyi Modern Women mnagunduaga haya siku yakishawakuta.
Ni kweli hili nimechelewa ila sio sana muda upo bado....nashukuru bado hayajanikuta 😃😃😃
 
Good morning jf....

Kuna hili swala nimekua nikijiuliza hivi karibuni, baada ya kuona sasa uzee umeanza kupiga hodi. Najiona umri umetangulia mbele halafu maisha ni kama nayaacha nyuma, ni kama naishi tofauti na umri wangu. Nimesogea umri wa kuozesha, kuondokewa na wapendwa (waliozeeka) na kukutana na mambo mengi ambayo nadhani yanahitaji watu....ila bahati mbaya sasa hao watu ndio sina.

Natamani kuwa na marafiki kuwa na watu, watu wa faida, watu ambao wanaweza kushare ramani za maisha, watu ambao tunaweza kupanga safari kwenda vituo vya wahitaji tukawape misaada, watu ambao nikihitaji kumwagilia moyo najua wapo, watu ambao nikikwama najua watakuwepo, kina mama wenzangu huwa wana vyama umuhimu wa vyama naujua ila mi hata chama sijawahi kuwa nacho....naishi mwenyewe mwenyewe tu hadi nawaza si nitakosa wa kunizika mie mwisho nizikwe na manispaa.

Wenye marafiki mnawapataje???
Jaribu kujichanganya na watu unaowaona ni potential kwako na ni wa kiwango chako nikimaanisha elimu muwe sawa, kipato, umri nakadhalika marafiki wapo wengi sana ishu ni wewe unatarget marafiki wa aina gani mfano mimi napenda marafiki wenye lugha ya pesa pesa mda wote kama upo interested karibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani marafiki zako wa zamani wako wapi? Au hawana faida? Sasa hivi marafiki zangu ni wale wale tulikua wote. Baada ya mahangaiko ya dunia, tumeungana tena.
Kweli hata mimi ni hivyo, marafiki wa zamani ndio tumerudi kuwa karibu, lakini pia kuna mtaji wa watu wa kazini kwake, majirani zake, sehemu yake ya kuabudia nk.
 
Kweli hata mimi ni hivyo, marafiki wa zamani ndio tumerudi kuwa karibu, lakini pia kuna mtaji wa watu wa kazini kwake, majirani zake, sehemu yake ya kuabudia nk.
Kazini sina marafiki 😂😂 nikifika nafanya kazi zangu zikiisha hata kama ni saa nne naleft, nipo kwenye kikundi cha vicoba kazini lakini sipo interested na hao watu wana umbea uliopitiliza, nipo tu kwasababu nna faida nacho sana
 
1. Majirani zako: kuna vikundi vya ujirani mwema.
2. Marafiki wa utotoni: hawa ni automatic wanakuwa marafiki tu, hata kama mlippteana, siku mkionana ni kupeana namba na kulianzisha.
3. Class/schoolmates: huko wasap grps mnatengeneza bond moja matata, kufungua vikundi vya kusaidiana nk
4. Watu wa ibadani(kanisani au msikitini): pqmoja na majungu ya watu wa Mungu lakini unaweza kupata wawili watatu na mkaendana na kuwa msaada kwa kila mmoja.
5. Ofisini: huko ndio sina la kusema, hata kama umejiajiri bado inawezekana sana.

Hii cycle mbona inatosha sana kutengeneza marafiki, tena wa faida kabisa.
 
Jaribu kujichanganya na watu unaowaona ni potential kwako na ni wa kiwango chako nikimaanisha elimu muwe sawa, kipato, umri nakadhalika marafiki wapo wengi sana ishu ni wewe unatarget marafiki wa aina gani mfano mimi napenda marafiki wenye lugha ya pesa pesa mda wote kama upo interested karibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ninajichanganya nao wapi yani nadhani pa kuanzia ndio sina
 
Back
Top Bottom